Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 36,351
- 23,757
Ndugu zangu Watanzania,
Kwa hakika tumepata Rais ,tumepata kiongozi imara,tumepata nahodha hodari,tumepata jemedari shupavu. Watanzania Tumepata Amiri Jeshi Mkuu Shupavu , Madhubuti na Shujaa kwelikweli. Tuna kila sababu ya kujivunia kuwa Na Rais Samia kitini. Tuna kila sababu ya kusema asante Mungu kwa kutupatia Rais Samia.
Hotuba yake ya leo Imewakosha na kuwagusa Sana watanzania. Ni hotuba iliyoonyesha sisi ni Taifa huru na tupo tayari kulinda ,kutetea na kupigania uhuru wetu dhidi ya mtu au Taifa lolote lile ambalo linaweza kutaka kutweza au kutudhalilisha kwa namna yoyote ile. Mama na Rais wetu ameonyesha ya Kuwa anatambua wajibu wake muhimu kama Amiri Jeshi Mkuu katika kulinda katiba na Taifa letu.
Rais Samia ametoa Hotuba ambayo imejibu maswali yote kwa uhodari mkubwa sana. Haina swali ambalo limeachwa. Chochote kilichozungumzwa na viongozi wa dini waliojivika uwanaharakati kama akina Kitima amewajibu vizuri sana . Amejibu kwa ufasaha mkubwa sana hoja za upinzani ,asasi za kiraia matamko ya kimataifa na kila kitu kilichozungumzwa iwe ni kwenye mitandao ya kijamii ama magazeti ama mitaani ameweza kujibu kila neno kwa neno.
Ameonyesha ni kiongozi ambaye anafuatilia na kujua kila kitu kinachofanyika ndani na nje ya Nchi kinachohusu Na Kugusa Nchi yetu. Ndio sababu amejibu kila kitu na kila jambo lililozungumzwa na watu ama taasisi ama Nchi ama jumuiya.
Kwa hakika ameonyesha uimara na utayari wa kuliongoza Taifa letu kwa moyo wa uzalendo mkubwa sana. Ametukosha watanzania kwa namna alivyo onyesha kutokuwa tayari kuona Taifa letu likidhalilishwa ama kusimangwa na yeyote yule awaye.
Ameonyesha anakwenda kujenga Taifa la aina gani na uongozi wake utakuwa wa aina gani. Ameonyesha kutanguliza mbele maslahi ya watanzania na kuwa tayari kusikiliza sauti za watu wote katika meza ya mazungumzo na kwa njia ya amani. Ameonyesha kukunjua mkono wa amani na maridhiano kama ilivyo kawaida yake. Kwa hakika Mama ameendelea kuonyesha ni chaguo la Mungu aliyeinuliwa kwa mkono wa Mungu kuliongoza Taifa letu.
Mama amefungua mioyo ya watanzania na kuwapatia matumaini. Amewafuta machozi waliokuwa maumivu na wakibubujikwa na machozi ya huzuni. Ameliunganisha Taifa kwa kauli na maneno yake. Amewapa nguvu na ujasiri wa kufanya kazi na shughuli za maendeleo watanzania pasipo hofu wala wasiwasi..
Ametuhakikishia watanzania uhakika wa kuendelea kutamalaki kwa Amani na utulivu na usalama wa kutosha katika Taifa letu kama Muendelezo wa mbegu iliyo pandwa na waasisi wa Taifa letu.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kwa hakika tumepata Rais ,tumepata kiongozi imara,tumepata nahodha hodari,tumepata jemedari shupavu. Watanzania Tumepata Amiri Jeshi Mkuu Shupavu , Madhubuti na Shujaa kwelikweli. Tuna kila sababu ya kujivunia kuwa Na Rais Samia kitini. Tuna kila sababu ya kusema asante Mungu kwa kutupatia Rais Samia.
Hotuba yake ya leo Imewakosha na kuwagusa Sana watanzania. Ni hotuba iliyoonyesha sisi ni Taifa huru na tupo tayari kulinda ,kutetea na kupigania uhuru wetu dhidi ya mtu au Taifa lolote lile ambalo linaweza kutaka kutweza au kutudhalilisha kwa namna yoyote ile. Mama na Rais wetu ameonyesha ya Kuwa anatambua wajibu wake muhimu kama Amiri Jeshi Mkuu katika kulinda katiba na Taifa letu.
Rais Samia ametoa Hotuba ambayo imejibu maswali yote kwa uhodari mkubwa sana. Haina swali ambalo limeachwa. Chochote kilichozungumzwa na viongozi wa dini waliojivika uwanaharakati kama akina Kitima amewajibu vizuri sana . Amejibu kwa ufasaha mkubwa sana hoja za upinzani ,asasi za kiraia matamko ya kimataifa na kila kitu kilichozungumzwa iwe ni kwenye mitandao ya kijamii ama magazeti ama mitaani ameweza kujibu kila neno kwa neno.
Ameonyesha ni kiongozi ambaye anafuatilia na kujua kila kitu kinachofanyika ndani na nje ya Nchi kinachohusu Na Kugusa Nchi yetu. Ndio sababu amejibu kila kitu na kila jambo lililozungumzwa na watu ama taasisi ama Nchi ama jumuiya.
Kwa hakika ameonyesha uimara na utayari wa kuliongoza Taifa letu kwa moyo wa uzalendo mkubwa sana. Ametukosha watanzania kwa namna alivyo onyesha kutokuwa tayari kuona Taifa letu likidhalilishwa ama kusimangwa na yeyote yule awaye.
Ameonyesha anakwenda kujenga Taifa la aina gani na uongozi wake utakuwa wa aina gani. Ameonyesha kutanguliza mbele maslahi ya watanzania na kuwa tayari kusikiliza sauti za watu wote katika meza ya mazungumzo na kwa njia ya amani. Ameonyesha kukunjua mkono wa amani na maridhiano kama ilivyo kawaida yake. Kwa hakika Mama ameendelea kuonyesha ni chaguo la Mungu aliyeinuliwa kwa mkono wa Mungu kuliongoza Taifa letu.
Mama amefungua mioyo ya watanzania na kuwapatia matumaini. Amewafuta machozi waliokuwa maumivu na wakibubujikwa na machozi ya huzuni. Ameliunganisha Taifa kwa kauli na maneno yake. Amewapa nguvu na ujasiri wa kufanya kazi na shughuli za maendeleo watanzania pasipo hofu wala wasiwasi..
Ametuhakikishia watanzania uhakika wa kuendelea kutamalaki kwa Amani na utulivu na usalama wa kutosha katika Taifa letu kama Muendelezo wa mbegu iliyo pandwa na waasisi wa Taifa letu.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.