Hotuba ya Rais mpya kijana wa Senegal

Hotuba ya Rais mpya kijana wa Senegal

Mzungu huwa habagazwi waziwazi namna hii , huyu rais kaanza kwa mihemko. Alipaswa kuwaminya kimya kimya.

Senegal haiko huru kiuchumi, bidhaa nyingi sana zinatoka kwa hao wazungu ikiwa ni pamoja na France.

Kwa hotuba hii kali dhidi ya France tayari huyu rais anaandaa anguko lake ama kifo chake. Wazungu siyo wa mchezo mchezo.

Watamtafuta kwa msosi, kwa tiba, kwa mtutu, kwa sumu, kwa kutumia marafiki zake, nguo zake, gari lake, n.k. Nina hakika hatatoboa.
Wewe ndiye mwoga wa wazungu..

Ukitaka kumshinda shetani, ni lazima uuvae ujasiri wa kumpinga na kumfyatulia mbali huko..

Kwa sababu literally, Ibilisi/shetani alishashindwa lakini hutumia udhaifu wa mwanadamu anaoudhihirisha kwa woga na hofu kumkandamiza..

Ukiushinda WOGA na HOFU (fear of unknowns) na ukam - face shetani, atakukimbia..

Na kumbuka, shetani/ibilisi ni roho. Huwezi kumwona shetani mwenyewe physically isipokuwa hujidhihirisha kwa matendo yake kupitia kwa binadamu. Serikali ya Ufaransa ndie shetani mwenyewe. Kijana (Rais wa Senegal) kajitoa na kumkabili shetani kama inavyopaswa kuwa. Nikuambie kitu, kuwa, huyo alishashindwa tayari..

Unachokitoa wewe hapa toka ktk uvungu wao moyo wako ni udhihirisho pia kuwa hata wewe Sexless una roho ya ibilisi ndani yako na inayosaidia kuendeleza uwepo wa matendo maovu ya serikali ya Ufaransa (makao ya shetani) dhidi ya wananchi wa Senegal..

ACHA WOGA NDUGU. MPINGE SHETANI NAYE ATAKUKIMBIA.
 
Wadau kwenye kikao cha mwisho si tulikubaliana kuwa miaka 44 ni Mzee.......au wanasiasa hawaguswi na kifungu hicho
 
Nyerere alikuwa mtu wa hotuba hotuba lakini kwenye uchumi na maendeleo aiseeh au basi
 

Mzungu huwa habagazwi waziwazi namna hii , huyu rais kaanza kwa mihemko. Alipaswa kuwaminya kimya kimya.

Senegal haiko huru kiuchumi, bidhaa nyingi sana zinatoka kwa hao wazungu ikiwa ni pamoja na France.

Kwa hotuba hii kali dhidi ya France tayari huyu rais anaandaa anguko lake ama kifo chake. Wazungu siyo wa mchezo mchezo.

Watamtafuta kwa msosi, kwa tiba, kwa mtutu, kwa sumu, kwa kutumia marafiki zake, nguo zake, gari lake, n.k. Nina hakika hatatoboa.
wAkati nikiangalia na kusikiliza hii hotuba kilichonijia kichwani ndio ulichoandika hapa. Anatakiwa kuwa makini sana.
 
wAkati nikiangalia na kusikiliza hii hotuba kilichonijia kichwani ndio ulichoandika hapa. Anatakiwa kuwa makini sana.
Ni kweli mkuu. Wazungu wanakera, lkn style ya kuwaondoa haipaswi kuwa ya wazi na kejeli namna hii. Maana wameshikilia mifumo yote ya dunia, huyu Faye atawakwepaje?

Mugabe aliwatukana waziwazi wazungu lkn nchi yake ilifika mahala ikawa kama jehanamu kwa ugumu wa maisha.
 
Hiyo ni speech ya jamaa mwanaharakati wa Chad tokea mwaka jana inatembea kwenye media wala siyo Rais wa Senegali...wadau mnashindwa kuona ni sura mbili tofauti.
 
Hiyo ni speech ya jamaa mwanaharakati wa Chad tokea mwaka jana inatembea kwenye media wala siyo Rais wa Senegali...wadau mnashindwa kuona ni sura mbili tofauti.
Umefuatilia hiyo link YouTube?

Ebu tuwekee hiyo uliyoiona tujiridhishe.
 
Back
Top Bottom