Hotuba ya Mhe Moh Dewji: April 25, 2009

Hotuba ya Mhe Moh Dewji: April 25, 2009

Sioni kama alichofanya ni kibaya kwani ametatua matatizo ya kimsingi katika kuwawezesha wananchi wake kujiendeleza. Ametatua ya dharura (chakula cha msaada) na ya long-term (elimu, maji na afya). Kilichopo ni wananchi wamsaidie kutunza visima vya maji na watumie fursa hiyo kuwapeleka watoto wao kwenye shule hizo za upili. Naamini baadaye familia kadhaa zitanufaika na long-term investment ya Mheshimiwa huyu. Labda kwa nyongeza aibane serikali ktk huduma ambazo anaona hawezi ku-walk alone.

Kiongozi kumbe watokea Singida! Teh teh teh teh Ukija mjini njoo na wale kuku wa kienyeji (Kuchi)
 
Hongera Mh. Dewji! Mambo kama haya hii ndiyo wapiga kura wanataka kusikia siyo "mafanikio" ya kusaidia kupitisha Miswada na Sheria za Ruzuku na Madini bungeni (Ordinary folks don't relate to such crap)

Mkuu, unajua hiyo ndiyo kazi ya mbunge, kutunga sheria. Miswada hii ndiyo inatakiwa kumletea maendeleo mwananchi. Siyo milioni 500 za kutoka mfukoni mwa mtu binafsi. Uchumi wa sasa si imara, Je Mh. Mo akifilisika itakuwaje? Na vipi majimbo yale ambayo hayana wafanyabiashara matajiri kama wabunge wao? Kuna wabunge walikuwa walimu tu wa shule kama Mudhihir Mudhihir, wasipotegemea miswada na sheria na kugawa keki ya Taifa wananchi wao wataendelea vipi? Hapa ndiyo maana wananchi wanachagua viongozi kwa kuangalia nani kamwaga pilau nyingi zaidi na kutoa doti za kanga nyingi zaidi. Ubaya wa kupokea kila kitu matokeo yake ndiyo kama hayo, ametoa Tractor na halijatumika.
 
..nadhani Mbunge ashirikishe zaidi wananchi kwa kazi za kujitolea.

..pia ahakikishe hizi shule wanazojenga zinapatiwa vifaa vya kufundishia,maktaba za uhakika, na waalimu.
 
nadhani kweli kluna haja ya kutenganisha siasa na biashara iwapo tutanata kuwepo kwa ushindani wa haki katika siasa. Katika mazingira kama haya, ni wangapi wataweza kushindana na mtu kama huyu?
 
Duh, jamani lakini mkuu wangu anatisha!.. kuwa na fedha au tajiri sii sababu ya kufanya yote haya ni MOYO wa kuipenda nchi na wananchi wako.
 
Mimi nina tatizo na sababu hasa ya Mh. Mohamed Dewji kuutafuta ubunge - ili iweje ? Ili atoe misaada, ili atoe posho au ili awekeze kwenye sekta ya watu ? Je bila kuwa mbunge kitu gani kingemzuia kuwasaidia wananchi wa Singida kama anavyofanya lakini kama tajiri na mfanya biashara. Watu kama Bill Gates sijasikia wakiingia kwenye siasa ili waweze kutoa misaada. Je, hawa matajiri wa Bongo, wanatafuta nini hasa kwenye siasa ? Jibu nafikiri wote tunalo.
 
Mkuu, unajua hiyo ndiyo kazi ya mbunge, kutunga sheria. Miswada hii ndiyo inatakiwa kumletea maendeleo mwananchi. Siyo milioni 500 za kutoka mfukoni mwa mtu binafsi. Uchumi wa sasa si imara, Je Mh. Mo akifilisika itakuwaje? Na vipi majimbo yale ambayo hayana wafanyabiashara matajiri kama wabunge wao? Kuna wabunge walikuwa walimu tu wa shule kama Mudhihir Mudhihir, wasipotegemea miswada na sheria na kugawa keki ya Taifa wananchi wao wataendelea vipi? Hapa ndiyo maana wananchi wanachagua viongozi kwa kuangalia nani kamwaga pilau nyingi zaidi na kutoa doti za kanga nyingi zaidi. Ubaya wa kupokea kila kitu matokeo yake ndiyo kama hayo, ametoa Tractor na halijatumika.


Kwame Nkrumah:

Hakuna ubaya kama anavyofanya havivunji sheria na katiba ya nchi. Hapa JF, mara nyingi FMES anasema kuwa Mwalimu alikuwa anatoa pesa mfukoni kuwapelekea wanafunzi kama JK. Je mfanyabiashara kufanya hivyo kuna ubaya gani?

Charity starts at home. Mbunge ambaye anashindwa kutoa chochote kusaidia watu wake, basi hataweza kutunga sheria za kuwasaidia watu wake.
 
Mimi nina tatizo na sababu hasa ya Mh. Mohamed Dewji kuutafuta ubunge - ili iweje ? Ili atoe misaada, ili atoe posho au ili awekeze kwenye sekta ya watu ? Je bila kuwa mbunge kitu gani kingemzuia kuwasaidia wananchi wa Singida kama anavyofanya lakini kama tajiri na mfanya biashara. Watu kama Bill Gates sijasikia wakiingia kwenye siasa ili waweze kutoa misaada. Je, hawa matajiri wa Bongo, wanatafuta nini hasa kwenye siasa ? Jibu nafikiri wote tunalo.

Bill Gates hakutaka kuzitumia haki zake za kiraia lakini sio kweli kuwa utajiri wake umemkataza kuingia kwenye siasa.

Mayor wa New York City ni Billionare na ni mwanasiasa. Hivyo utajiri haumnyimi mtu haki zake za kikatiba.
 
NImrod mkono na mohamed dewji ni wabunge wa mfano....hata mkiwaita mafisadi .....ni wabunge wangapi mafisadi ...they never give back to the people...
 
Zakumi,
Zaidi ya hapo wanasiasa karibu wote Marekani ni matajiri wakubwa hata wale wa chama cha Domokratic..Muhimu tunarudi palepale Watu na mazingira, sisi maskini tunapopata tajiri wa kufanya haya makubwa ya faida kwa wananchi kwa muda mrefu tuanza ku question malengo yake baada ya kushiba. Ndio hapo naposhindwa na Watanzania.
 
Duh, jamani lakini mkuu wangu anatisha!.. kuwa na fedha au tajiri sii sababu ya kufanya yote haya ni MOYO wa kuipenda nchi na wananchi wako.

Duh nimejaribu kujumlisha hizo namba mpaka kalukuleta yangu ikaganda. Sijawahi kuona namba yenye sifuri nyingi hivyo...

Anyway, Mo iwe anafanya hivi ili kujilinda, kutafuta kura 2010, au vyovyote vile, lakini ukweli unabaki kuwa angalau yeye anaonyesha jitihada zake kwa vitendo katika masuala ya maendeleo ya jimbo lake.

Kuna njia mbalimbali katika usaidiaji wa jamii. Amini usiamini, kumwaga hela ni njia moja wapo.

Fisadi anayelalia hela mchagoni na yule anayemega theluthi ya maburungutu yake na kuwagawia jirani, yupi afadhali?
 
Quemu,
Mtu kama huyu nitaampa kura yangu kila siku ya uchaguzi...amaadam sii fisadi na analipa kodi ya shughuli zake zake mwenyewe.
 
Zakumi,
Zaidi ya hapo wanasiasa karibu wote Marekani ni matajiri wakubwa hata wale wa chama cha Domokratic..Muhimu tunarudi palepale Watu na mazingira, sisi maskini tunapopata tajiri wa kufanya haya makubwa ya faida kwa wananchi kwa muda mrefu tuanza ku question malengo yake baada ya kushiba. Ndio hapo naposhindwa na Watanzania.


Mkandara:

Kufanya biashara ni profession kama vile kuwa mwalimu, mganga au mtu yoyote.

Na ni concept mbaya kufikiria kuwa mfanyabiashara ni lazima awe mwizi, fisadi au asiyeweza kuwa mwanasiasa mwadilifu.

Na kama mfanyabiashara anakuwa fisadi, mwizi anafanya hivyo kwa kushirikia na waalimu, wakurugenzi, wakulima, mapolisi.
 
..lakini hawa Mohamed Enterprise si walikuwa wanatuhumiwa kuingiza na kuuza mchele mbovu nchini?

..nakumbuka kulikuwa na mjadala mkali sana bungeni miaka ile. hivi mmesahau maelezo ya mheshimiwa Semindu Kisange Pawa bungeni kuhusu mchele wa Mohamed Enterprise?

..halafu kuna kifo cha Dr.Fupi, aliyekuwa Mkemia Mkuu wa serikali wakati ule. wako wanaodai kifo chake kilitokana na maamuzi yake kuhusu sakata ya mchele huo mbovu.

..hivi kuna anayefahamu kesi ile ilikwisha ktk mazingira yapi?
 
..lakini hawa Mohamed Enterprise si walikuwa wanatuhumiwa kuingiza na kuuza mchele mbovu nchini?

..nakumbuka kulikuwa na mjadala mkali sana bungeni miaka ile. hivi mmesahau maelezo ya mheshimiwa Semindu Kisange Pawa bungeni kuhusu mchele wa Mohamed Enterprise?

..halafu kuna kifo cha Dr.Fupi, aliyekuwa Mkemia Mkuu wa serikali wakati ule. wako wanaodai kifo chake kilitokana na maamuzi yake kuhusu sakata ya mchele huo mbovu.

..hivi kuna anayefahamu kesi ile ilikwisha ktk mazingira yapi?

Ni vizuri ukataja ni mwaka gani tuhuma hizi zilitokea,je zilitokea wakati MO akiwa MD wa Mohammed Enterprises? ama zilitokea MO akiwa MP wa Singida?.Pia ni vema tukalenga zaudu katika nini MO kachangia katika kuwasaidia wananchi wake wa Singida(kulingana na hiyo hotuba hapo juu) badala ya hizo tetesi hapo juu kuhusu Mchele mbovu na kifo cha Dk. Fupi.Binafsi nampongeza sana MO kwa haya aliyoyafanya kwa wananchi waliomchagua,bora huyu anawakumbuka wananchi wake kuliko wale wengine ambao baada ya kuchaguliwa huwatelekeza wananchi wao na baadaye kuja kurudi na kuwahadaa kwa khanga,fulana,pombe na pilau ama wale wanaoutumia Ubunge kujinufaisha wao na familia zao

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni,muacheni MO aajisifu atakavyo maana kwa hayo aliyoainisha hapo juu anastahili KUJIFYAGILIA(lol).I wish jimboni kwangu tungekuwa na Mbunge wa sampuli hii
 
..lakini hawa Mohamed Enterprise si walikuwa wanatuhumiwa kuingiza na kuuza mchele mbovu nchini?

..nakumbuka kulikuwa na mjadala mkali sana bungeni miaka ile. hivi mmesahau maelezo ya mheshimiwa Semindu Kisange Pawa bungeni kuhusu mchele wa Mohamed Enterprise?

..halafu kuna kifo cha Dr.Fupi, aliyekuwa Mkemia Mkuu wa serikali wakati ule. wako wanaodai kifo chake kilitokana na maamuzi yake kuhusu sakata ya mchele huo mbovu.

..hivi kuna anayefahamu kesi ile ilikwisha ktk mazingira yapi?

Jokakuu:

Kulikuwa na kesi moja kuhusu unga wa ngano uliooza. Kesi hii ilikwenda kwa Mrema na bungeni. Kwenye kesi hiyo Mohamed enterprise ilikuwa victim ya extortion ya tapeli mmoja ambaye nina undugu naye. Siwezi kutoa details zaidi kwa sababu zangu mwenyewe.

Kama unayozungumzia hiyo kesi, basi kuna mambo mengi sana yalikuwemo. Lakini utapeli ulitia chumvi kwa kiasi fulani.
 
Kwame Nkrumah:

Hakuna ubaya kama anavyofanya havivunji sheria na katiba ya nchi. Hapa JF, mara nyingi FMES anasema kuwa Mwalimu alikuwa anatoa pesa mfukoni kuwapelekea wanafunzi kama JK. Je mfanyabiashara kufanya hivyo kuna ubaya gani?

Charity starts at home. Mbunge ambaye anashindwa kutoa chochote kusaidia watu wake, basi hataweza kutunga sheria za kuwasaidia watu wake.

Umetoa mfano wa Bloomberg. NYC ina matatizo mengi sana ya kifedha, mwaka jana kwa mfano, hela ya kusafisha snow iliisha kabla ya wakati, walimu wanakimbia inner city schools kwa sababu hawalipwi vizuri, police wengine wa NY wanaondoka kwenda PD za miji ya jirani wanakolipwa vizuri zaidi. Yote haya ni matatizo ambayo Bloomberg angeyatatua kwa kutoa tu hata robo ya utajiri wake lakini hajafanya hivyo, kwa sababu siyo njia muafaka ya kutatua tatizo. Leo MO anajenga mashule, mahospitali, visima nk, ikitokea akaamua kutogembea tena, au kushindwa uchaguzi na akaja mbunge hohehahe itakuwaje?
Dawa ni kufanya kazi bungeni kama alivyoomba kura kuwakilisha wananchi. Yeye si fisadi, lakini atunge sheria kwamba hela zote zilizoibwa na akina Chenge zirudishwe na mikataba mbali mbali ya kifisadi isainiwe upya. Akifanya hivyo zitapatikana hela nyingi za kujenga shule, barabara, visima na mahospitali na yeye hatatoa hela mfukoni mwake, badala yake hela zake atatanua biashara zake zaidi, ataajiri watu wengi zaidi na atalipa kodi zaidi. hivi ndivyo atakavyoleta maendeleo.
 
Kiongozi kumbe watokea Singida! Teh teh teh teh Ukija mjini njoo na wale kuku wa kienyeji (Kuchi)
Hapana Mkuu, wala sitokei Singida. Kuna mtu humu amesema mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, ni sawa kabisa. Tatizo linaweza kuwa ni ushindani usio fair, lakini kwa kuwa kila mshindani anataka aingie ulingoni ili kuleta maendeleo, basi hayo aliyofanya Mh. si haba !!
 
Zakumi,Balantanda,

..I dont remember the exact details, lakini suala la Mohamed Enterprise lilifika mpaka Bungeni.

..Wabunge machachari kama Semindu Kisange Pawa walikuwa mstari wa mbele kufuatilia suala la uingizwaji nchini wa mchele mbovu.

..pia kulikuwa na kesi mahakamani, na inasemekana mashahidi kama watano hivi walikufa kabla hawajatoa ushahidi wao. Mkemia Mkuu wa serikali, Dr.Fupi naye alifariki, na kuna watu wanahisi alifanyiwa kitu mbaya.

..Jamii Forums ni jungu kuu hili, kwa hiyo nahisi kwamba tunaweza kupata ukweli wa kilichojiri wakati wa sakata/kashfa ile.

NB:

..kashfa hii ilitokea miaka ya 1990 -- 1994.
 
Zakumi,Balantanda,

..I dont remember the exact details, lakini suala la Mohamed Enterprise lilifika mpaka Bungeni.

..Wabunge machachari kama Semindu Kisange Pawa walikuwa mstari wa mbele kufuatilia suala la uingizwaji nchini wa mchele mbovu.

..pia kulikuwa na kesi mahakamani, na inasemekana mashahidi kama watano hivi walikufa kabla hawajatoa ushahidi wao. Mkemia Mkuu wa serikali, Dr.Fupi naye alifariki, na kuna watu wanahisi alifanyiwa kitu mbaya.

..Jamii Forums ni jungu kuu hili, kwa hiyo nahisi kwamba tunaweza kupata ukweli wa kilichojiri wakati wa sakata/kashfa ile.

NB:

..kashfa hii ilitokea miaka ya 1990 -- 1994.

Basi si vizuri kumhusisha Mohammed na tuhuma hizi(kuziweka tuhuma hizi kwenye habari hii ni sawa na kumhusisha moja kwa moja na tuhuma hizi) maana kipindi zinatokea dogo alikuwa zake shule na kampuni(kama sikosei) ilikuwa chini ya baba yake mzee Ghulam Dewji,kumhusisha Mohammed na tuhuma hizi ni kumuonea tu...Cha msingi ni kumpongeza kwa haya aliyowafanyia wananchi wake,ni tofauti kabisa na wabubge wengi(hasa wa CCM)
 
Back
Top Bottom