Hotuba ya JK leo vipi?

Hotuba ya JK leo vipi?

Hotuba za , " ninawajua mafisadi nawapa muda wajirekebishe, " hotuba za sampuli hiyo zinatija gani hadi kupoteza muda wa kuziulizia?
 
Mimi nadhani kuna makundi hapa, la kwanza limemgeuza j.k kama mwigizaji, ndio maana wanaulizia kwa hamu sana hayo maigizo yake, kundi lingine la mambumbu wasiojua ulimwengu uko wapi lakini nao wanahaki ya kusubiria. Kundi lingine ni la watu makini sana na hawahitaji hata hayo maigizo yake.
 
Mimi nadhani kuna makundi hapa, la kwanza limemgeuza j.k kama mwigizaji, ndio maana wanaulizia kwa hamu sana hayo maigizo yake, kundi lingine la mambumbu wasiojua ulimwengu uko wapi lakini nao wanahaki ya kusubiria. Kundi lingine ni la watu makini sana na hawahitaji hata hayo maigizo yake.

Uko sawa kabisa mkuu. Nchi hii isengekuwa huu ukandamizwaji unaofanywa na hawa Mabwanyenye, kuna watu wangekuwa matajiri sana kwa kuwa-impersonate hawa madubwana yaliyo serikalini. Hayana tija yeyote. Kila siku ni vituko na vioja.
 
MIMI NASUBIRI 2015, NIMECHOKA KUSIKILIZA HADITHI ZA KUKU KUMNYONYESHA MWANAE
Movie ilianzia na kaulimbiu ya kutuletea maisha bora kwa kila mtanzania, alipoingia ikulu tumeona nani amepata maisha bora!! je ni machinga, wakulima, wachimba madini wadogo au hawa wanaojiita wawekezaje na vibaraka wao (wazee wa10%)?
Katika ku-edit movie sindiyo ikaingizwa kilimo kwanza, kwa mara ya kwanza tukashuhu jinsi watu walivyoanzisha kilimo kikubwa kwenye mahoteli kwa kuendesha mikutano, makongamano na semina kisha watu wakajichukulia posho zao wenzangu na mimi tukaishi kuuziwa viji-trekta mungu nisaidie!!
Sasa wakati tunaelekea 2015 Movie yetu ipo kwenye finishing, Stering anamaliza movie kwa mbwembwe za hali ya juu eti BIG RESULT NOW aka BRN, its implementation will focus on six prior areas
1)Energy and natural gas
2)Agriculture
3)Water
4)Tducation
5)Transport
6)Mobility of resources
 
Kakosa cha kuhutubia Mkuu, si ajabu wamo ndani ya kikao kizito kuzungumzia muswada wa katiba ya CCM huku wengi wa MACCM wakimshawishi ausaini muswada huo bila kutafakari athari kubwa zitakazotokea siku za usoni kama katiba ya CCM itakataliwa na Watanzania walio wengi.

kuna uzi ulipita hapa jana kueleza kuwa jk leo atalihutubia taifa kwa mwenye kujua kinachoendelea atujuze
 
Kwa hiyo yeye kama rais wa nchi na mwenyekiti wa chama kilichopo madarakani hawezi kuwaambia wananchi msimamo wake na kujibu kero zilizojitokeza?

Kama ni hivyo, kuna haja gani ya kuwa na raisi anayefuta upepo?
sasa mkuu mbona tume ikiizungumzia katiba mpya akina simiyu povu linawatoka.leo tunataka dhaifu aseme wanatoa povu.
 
jk hawezi kuongelea swala la rasimu siyo jukumu lake bali ni la tume swala la mswada ni swala la bungeni nalo siyo lake yeye amesaini mswada tangu jana nyie mnapiga porojo.

mara nyingi kimada anaweza juwa siri kuliko mke. Hebu endelea kutujuza ilikuwaje wakati akisani
 
hivi unafikiri JK kuongea kwake ni tabu? subiri tu uone atakavyoporomoka na hoja za msingi

Ni kweli mtu ambaye hana la kuongea and unorganised always hakosi cha kuongea, chochote kinachokuja kichwani hulisema almradi kuporomoka. Lakini mtu makini anayejua anatakiwa alihutubie taifa la watu makini hukaa chini na kujiandaa na ikibidi kuandaa hotuba yake mwenyewe kama alivyokuwa anafanya mwl. Nyerere.

Nchi hii inapitia kwenye mapito mazito kwa kukosa viongozi wenye weledi kwenye chama tawala. Viongozi hawana vission wala mission ya kulisaidia Taifa bali ni wataalam wa kupiga deals.
 
Nenda mkamuage dada mliyemuuwa anaagwa sasa hivi kkkt wazo mamtu mnaroho mbaya kama nini kazi kuuwa wenzenu tu ngoja muwamalize sijui mtamuongoza nani.

kichaa kinaanzaga taratibu lakn mwisho wako lazima uokote makopo
 
Ya Marekani hatuyataki. Atueleze atashughulikiaje tatizo la umeme, kodi line za simu na huo mswada yeye anauonaje? Ajue anaongoza watu sio ngombe.
 
Kuna tetesi kuwa aliugua ghafla ule ugonjwa wake wakati anajiandaa kuhutubia. Source: mfanyakazi wa ikulu kitengo cha mawasiliano. Nasikia kunaweza kuwa na taarifa mbaya! Tujiandae kisaiklojia.

Ugonjwa upi mkuu? Ule wa kuanguka?.....
 
nakumbukia hotuba za enzi ya mzee mkapa yaani hadi unakuwa na hamu ya kumsikiliza
 
nakumbukia hotuba za enzi ya mzee mkapa yaani hadi unakuwa na hamu ya kumsikiliza

Huyu hamna kitu,Mdahalo mbio zinamuokoa,Hotuba nazo anaokolewa na Mbio...! Rais tunaye
 
Back
Top Bottom