Hotuba ya Dr. Slaa kwa Watanzania toka Hoteli ya Serena - Tarehe 1 Septemba, 2015

Wewe mwenye akili umehangaika nini kumquote mjinga?
Hiyo hotuba unadhani uliangalia/kusikiliza wewe na mkeo tu chumbani kwenu?
Nenda basi ukanywe chai na huyo Slaa, pia umpe salamu kuwa hajabadili chochote zaidi katutia hasira ya kupigania mabadiliko.

Hao walitegemea tutayumbishwa na kauli za Dr lakini ndio kwanza wamempiga teke chura!Tarehe 24 nalala kituoni niwe wa kwanza kupiga kura!
 
Slaa Hajanishawishi Chochote Katika Akili Yangu Zaidi Ameniongezea Molali Ya Kuendelea Na Mapambano Huku Nikijua Ccm Wako Kazini Aluta Continua
 
Nilishawaambia kuwa hii mission imefeli hata kabla hajabwabwaja pumba zake iliishajulikana kuwa Dr. Slaa tayari amerudi kwa magamba. Kwa mara ya pili hila za CCM zinafeli vibaya baaday aile ya Lipumba kushindwa vibaya. Kwa taarifa tu mimi niko mbeya wananchi wameapa kura ni UKAWA tu na wana hasira kweli baad ya kubaini njama za magamba.

Sure! … hizo documents kibao za ushahidi wa ufisadi alizojaza dr. kwenye mkoba wake cc watz haztusaidii km miaka yooote kashndwa kuzfanyia kazi, Tuachie Lowasa wetu, kaeni na mgombea wenu, oct c mbali.
 
Ndugu yangu umesema unauhakika kuwa wife wake kamshawishi! LIZABON alisema wiki ya kwanza ya sepember UKAWA utapata dhoruba kali huoni kuwa hii kitu ilikuwa imepangwa.Yeye alijuaje kama si haohao waliomharibu dokta?Bora nisipige kura tu.
 
Baada ya tamko la Dkt. Jana pale serena nimekuwa nikifuatilia majibu ya baadhi ya wapambe na wakereketwa wa Umoja huo na kujiuliza majibu mengi pasi na majibu ila machache yanayonisumbua ni

1. Mbona wanakuwa wepesi kusahau moja ya nguzo yao ya kutetea wananchi hasa kwenye masuala ya ubadhilifu wa mali za umma (ufisadi) kama ajenda kuu iliyowajenga.
2. Kwann wanakuwa wepesi kutoa majibu mepesi kwenye masuala mazito yaliyoongelewa na Dkt. Slaa, inawezekana vipi baada ya kutafakari na kujibu hoja eti we unauliza HELA ZA KUFANYIA MKUTANO SERENA KAPATA WAPI? Seriously?
3.kwanini mnataka Dola by any meanz hata kwa kukumbatia wale waliotajwa kwenye List of shame(mafisadi).
4.kwann inakuwa ngumu hata kulitaja neno fisadi wakati wa kampeni zenu, agenda iliyokuwa fimbo kwenye chaguzi zilizopita
5. Kwann mlitulaghai kwa kuwadanganya wananchi ETI Dkt. Slaa yupo mapumziko na soon atarudi wakati kuna issue behind that....(mnataka tuwafikirie na kuwaweka katika kundi gani).


Slaa hastahili hata kujibiwa, huyu ni wa kupuuzwa tu
 
eti anakula mihogo mzee unafikiri sisi ni watanzania wa mwaka 47 !!?
Slaa amekuwa magumashi kweli kweli !
 
Dr hawezi kubadilisha msimamo wangu nashukuru na watu wangu wa karibu wamempuuza kwa hiyo mwendo ule ule
 
Hii kweli kama Samsoni kwa Delila alivyoingizwa mkenge na mke wake kwa kweli lazima mwanaume uwe strong katika familia ndo utajulikana kuwa wewe ni kichwa cha nyumba sio kuyumbishwa yumbishwa.
 
Wakuu kama mtu alishawahi kupoteza kibarua chake either kwa nia nzuri au mbaya atakuwa na jibu.Ni watu wachache sana wanaopoteza kazi zao then wakabaki kutoa sifa nzuri kwa mabos wao wa zamani.Mara nyingi watu husema yale mabaya tu bila kusahau sana yale machache aliyosimamia akiwa bado ni mfanyakazi kwenye hiyo taasisi.Hivyo basi tuendelee na safari ya mabadiliko
 
kama anaushahidi apeleke mahakamani sisi tumeshaamua hata ukawa waweke jiwe na ccm waweke makufuri sisi tutapigia kura jiwe maana tumechoka na ccm.
 
nimeamini papuchino inanguvu

Hasa ikiongezewa yale maufundi ya gulioni KT.
Waweza kuambiwa nitukanie babaako nawe bilakujali ukatukana,acha kabisa! Hasa ukizingatia mambo hayo umeyaanza ukubwani.
Watawala waligundua udhaifu huo ndio maana hapa JF kulikuwa na Uzi unasema kuna kiongozi mmoja anafanya mawasiliano na Jose, nadhani alikuwa anamshawishi atumie ushawishi huo
 
Back
Top Bottom