Hoteli wanayopika ugali asubuhi

Kuna entobheke inawekwa kwenye (ntahe) thermos ya kikurya alafu kuna ule uji wa mkwelima na pembeni ufuta ulokaangwa ukachanganywa na ulezi wa kukaanga (vinaongeza nguvu za kiume ma mkwe be blessed kwa makusudi uliyonilisha hivyo)
 
Mwenyewe napenda sana ugali asubuhi
 
Yeeeeeuuuuuwwwwiiiiii...... Mkuu itabidi likizo ya mwaka huu niende home special kwa ajili ya hivyo vitu... Kwanza Kichuri, pili ubhusara, tatu ekhimoro, nne na mwisho huo uji unaotengenezwa kwa mafuta ya maziwa a.k.a NTOBHEKHE
Huo uji bana acha tu ile ladha yaani sijui ubunifu ule waliutoa wapi bibi zetu ila niliuza maandalizi ya ule uji si mchezo
 
Eeh tata hadi udenda umenitoka
 
Kwa maana moja au nyingine ni kwamba wewe umetembelea hotel zooooote za dar na ukabaini ya kuwa hiyo hotel pekee ndiyo inayopika ugali asubuhi!!
 
Huo ni ubunifu mkuuu naona wenye hoteli wameona wafanye hivo ili kujitofautisha na hoteli nyingine
 
Mazoe tu! Mm ugali hata saa 11 alfajiri nagonga vzuri tu! Tena ukipata ule wa muhogo na samaki ya kukaanga acha kabisaa!

Kanda ya ziwa kawaida sana mkuu hizo mambo!
 
Kwa maana moja au nyingine ni kwamba wewe umetembelea hotel zooooote za dar na ukabaini ya kuwa hiyo hotel pekee ndiyo inayopika ugali asubuhi!!
Hapana ,sema imezoeleka ugali kutokuwa kifungua kinywa, kwangu niliona ni habari na kuona niwashirikishe humu wadau nanyi mtoe maoni yenu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…