Kwa kweli mi nipo Morogoro, na kwa bahati (mbaya sijui) huwa hiyo barabara napita almost kila siku, hivyo imekuwa rahisi kukusanya vipandevipande vya taarifa kutoka kwa watu. Awali eneo hilo lilikuwa mali ya LITI na lilipakana na eneo la Magereza. Inasemekana hata hivyo ilikuja kuibuka mgogoro baina ya taasisi hizo mbili juu ya umiliki wa eneo hilo (miaka ya 90). Sintofahamu hiyo ilipelekea manispaa kuamua kulichukua eneo hilo na kuligawa viwanja miaka hiyo hiyo na waliobahatika walilipia hadi sh 500,000 kwa kiwanja kimoja (miaka ya 90). Wakati zoezi hilo likikaribia kumalizika, aliyekuwa Principle wa LITI alipeleka malalamiko Wizarani, na ikaamuliwa kuwa eneo hilo libakie kuwa la Serikali. Waliokuwa wamelipia viwanja walitakwa radhi na Manispaa na baada ya kufuatilia kwa miaka kadhaa (mostly waliopata viwanja walikuwa 'wakubwa' hivyo hakukuwa na kuandamana au nini sijui) walifanikiwa kupewa viwanja vingine maeneo ya Kilimanjaro (ni eneo hapa Moro).
Eneo libakia kuwa chini ya umiliki wa serikali, sehemu moja ikiangaliwa na LITI na nyingine ikiangaliwa na Magereza (ingawa halikuendelezwa). Binafsi SIJUI ni nini kilifanyika, lakini mwaka juzi eneo lile lilianza kuendelezwa kwa kujengwa, na hapo ndipo duru mbalimbali zikaripoti kuwa panajengwa Hotel ya kitalii, inayomilikiwa na Lowassa. Kuwa alifanyaje hadi akalipata, haieleweki vizuri, kila mtu anaeleza kivyake, lakini watu wote niliosikia wakielezea wanasema linamilikiwa na Lowassa, na kuan wakati amekuwa akionekana katika eneo hilo (binafsi sijawahi kumuona). Kinachowahuzunisha watu hapa ni pale wananchi wa kata lilipo walipoomba eneo hili wajenge shule ya kata wakakataliwa na kwenda kupewa eneo maeneo ya nanenane, kilomita kadhaa, mbali na kata hiyo, hivyo inawalazimu wanafunzi kutumia usafiri hasa wa dala dala kufika shule, wakati eneo lililopo katani mwao amepewa 'mwekezaji'.
Sambamba na hilo, lipo eneo jingine kilomita kadhaa nje ya mji wa Morogoro, kuelekea Kilosa, ambalo kwa miaka ya karibuni limezungushiwa fence ya seng'enge na linasemekana ni la Lowassa tena. Ni eneo kubwa ambalo kwa mwendo wa kawaida utaendesha gari takribani dakika ishirini, kutokea mwanzo hadi mwisho ukipita barabara iliyopakana na eneo hilo kwa upande mmoja. Kwa hiyo hapa tunaongelea ekari elfu kadhaa, au kilomita kadhaa za mraba. Inasemekana kuwa mmiliki wa eneo hili anataka kulifanya zoo ya kisasa (kama za sauz). Hii inawezekana kwa sababu eneo hili limepakana na Mikumi National park, na kwa bahati (mbaya pengine), linabeba mto mkubwa usiokatika maji hata kiangazi, ambao wanyama wa mikumi hufika kunywa maji hasa majira ya kiangazi.