Hospitali zimezidiwa wagonjwa wa COVID-19, kuanza kutibiwa nyumbani

Mbolabilika

JF-Expert Member
Jul 30, 2019
2,126
2,860
Serikali ya Kenya inatengeneza muongozo wa uangalizi salama wa wagonjwa wa virusi vya corona wakiwa nyumbani.

Kulingana na waziri wa afya Mutahi Kagwe serikali inachukua hatua hiyo ili kupunguza msongamano katika hospitali za umma ili kuzuia kujaa kupitia kiasi

”Hospitali za Mbagathi na Kenyatta zinakaribia kujaa. Wagonjwa wengi waliothibitishwa ni wagonjwa wa pumu na wanaweza kutibiwa kutoka nyumbani”, alisema waziri huyo

Kagwe alitoa tangazo hilo huku wagonjwa wengine 124 wakithibitishwa kuwa na virusi hivyo hatua inayofanya idadi ya wagonjwa walioambukizwa virusi hivyo nchini Kenya kufikia 2,340

Some of the new beds at the women's ward at the Coast Provincial General Hospital

Maktba
Wakati huo huo Serikali imetishia kutoa picha za wagonjwa wa Covid -19 waliotoroka vituo vya karantini katika vyombo vya habari.

Waziri Kagwe amesema kwamba hatua hiyo itachukuwa wajibu muhimu ili kuwasaidia raia kuwatambua wale walio hatari kwao.

Kagwe amesema kwamba wale wanaotafutwa wamebadilisha mbinu na wameamua kuzima simu zao na kuendelea kutangamana na raia na hivyo basi kuhatarisha maisha ya wengine.

‘Unapozima simu yako, na kutoka Kawangware na kuelekea Thika na kurudi huku marafiki zako wakitupigia simu’, hiyo ina maana gani, alisema Kagwe.
mbagathi
Aliongezea, “Tunapofikia wakati ambapo tuna thibitisho kwamba unatoroka, hakuna chochote kinachoweza kuizuia wizara kuchapisha picha zako magazetini.

Alisema kwamba picha zitaandamana na maelezo yanayosema kwamba mgonjwa huyu ametoroka katika kituo cha karantini na hivyo basi ni mtu hatari kwa umma.
Waziri huyo amesema kwamba wagonjwa sita waliotoroka karantini Turkana walitafutwa na kurudishwa katika kituo hicho.
 
Mikopo waliyochukua sasa inawapelekesha.
Wanaanza kuonja joto la jiwe ,Sasa watu baada ya ndugu yao kupata korona c wataamua wasimpeleke hospital wabaki nae tu home ,Ila hii mbinu ina faidia kwa Tanzania maana mda c mrefu watafika 10000 sababu wataambukizana kwa speed nyumbani
 
Wanaanza kuonja joto la jiwe ,Sasa watu baada ya ndugu yao kupata korona c wataamua wasimpeleke hospital wabaki nae tu home ,Ila hii mbinu ina faidia kwa Tanzania maana mda c mrefu watafika 10000 sababu wataambukizana kwa speed nyumbani

Wakenya nyie tunawaangalia tu nyie, you are ideally admitting failure in Mbu lokolokodauni, I hope by now your Kandahar and kalbalah are beyond normal fluidity.
 
Serikali ya Kenya imewachoka RAIA wake,sasa imeona wajifie nyumbani,hakuna nchi ya Afrika inayoweza kutibu wagonjwa zaidi ya elfu moja nyumbani,hakuna magari yakutosha,madaktari,miundo mbinu isio rafiki,madaktari wasiotosha.hii ni hatari kwa taifa la Kenya.MK254,humuoni hapa!hahaha.
 
Serikali ya Kenya inatengeneza muongozo wa uangalizi salama wa wagonjwa wa virusi vya corona wakiwa nyumbani.

Kulingana na waziri wa afya Mutahi Kagwe serikali inachukua hatua hiyo ili kupunguza msongamano katika hospitali za umma ili kuzuia kujaa kupitia kiasi

”Hospitali za Mbagathi na Kenyatta zinakaribia kujaa. Wagonjwa wengi waliothibitishwa ni wagonjwa wa pumu na wanaweza kutibiwa kutoka nyumbani”, alisema waziri huyo

Kagwe alitoa tangazo hilo huku wagonjwa wengine 124 wakithibitishwa kuwa na virusi hivyo hatua inayofanya idadi ya wagonjwa walioambukizwa virusi hivyo nchini Kenya kufikia 2,340

Some of the new beds at the women's ward at the Coast Provincial General Hospital's ward at the Coast Provincial General Hospital

Maktba
Wakati huo huo Serikali imetishia kutoa picha za wagonjwa wa Covid -19 waliotoroka vituo vya karantini katika vyombo vya habari.

Waziri Kagwe amesema kwamba hatua hiyo itachukuwa wajibu muhimu ili kuwasaidia raia kuwatambua wale walio hatari kwao.

Kagwe amesema kwamba wale wanaotafutwa wamebadilisha mbinu na wameamua kuzima simu zao na kuendelea kutangamana na raia na hivyo basi kuhatarisha maisha ya wengine.

‘Unapozima simu yako, na kutoka Kawangware na kuelekea Thika na kurudi huku marafiki zako wakitupigia simu’, hiyo ina maana gani, alisema Kagwe.
mbagathi
Aliongezea, “Tunapofikia wakati ambapo tuna thibitisho kwamba unatoroka, hakuna chochote kinachoweza kuizuia wizara kuchapisha picha zako magazetini.

Alisema kwamba picha zitaandamana na maelezo yanayosema kwamba mgonjwa huyu ametoroka katika kituo cha karantini na hivyo basi ni mtu hatari kwa umma.
Waziri huyo amesema kwamba wagonjwa sita waliotoroka karantini Turkana walitafutwa na kurudishwa katika kituo hicho.

Ajabu na kweli ya wachangiaji uchwara wa JF wa leo ni kuwa, palikuwa na uzi hapa May 25:

Mgonjwa wa Corona haambukizi baada ya siku 11 hata kama atakuwa 'positive'

Uzi huo ulishabikiwa sana na wale wale ambao leo wanayaponda matumizi hayo ya uelewa huo mpya kwenye kupambana na ugonjwa huu.

Huu ugonjwa ungali mpya mno. Uelewa mpya utaendelea kuja hadi tiba au chanjo vitakapo patikana.

Kila mapya mazuri yatakapokuja hata wakati wa mapambano yatatumika.

Alisema mzee baba, "hivi vitani ukiteka kifaru cha adui, si unakitumia na kuendelea kumpiga nacho huyo adui?" Mwisho wa kumnukuu.

Ama kweli ukiyastajaabu ya Mussa subiria ya wachangiaji hawa uchwara wa JF new generation. Nini wanataka nini hawataki anayejua kwa hakika ni shetani peke yake!

Slow slow kazi anayo!
 
Serikali ya Kenya imewachoka RAIA wake,sasa imeona wajifie nyumbani,hakuna nchi ya Afrika inayoweza kutibu wagonjwa zaidi ya elfu moja nyumbani,hakuna magari yakutosha,madaktari,miundo mbinu isio rafiki,madaktari wasiotosha.hii ni hatari kwa taifa la Kenya.MK254,humuoni hapa!hahaha.
Ndio ungelianza kujiuliza wewe kwanza, Tanzania wagonjwa nyumbani wako wangapi baada ya kuacha kupima?
 
Back
Top Bottom