Shapu
JF-Expert Member
- Jan 17, 2008
- 2,111
- 790
Nimesoma kipande hiki cha habari Raia mwema.. Naomba tukijadili.
Katika hatua nyingine, taarifa zinasema Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inazichunguza kamati kadhaa za Bunge, ikiwa ni pamoja na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, ambayo ilihusika kuibua sakata la Richmond na kuiumbua TAKUKURU yenyewe.
Kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Bumbuli (CCM), William Shelukindo na makamu wake, Dk. Harrison Mwakyembe, ilipendekeza kuchukuliwa hatua kwa Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Dk. Edward Hosea, na wasaidizi wake kutokana na kushindwa kubaini udhaifu mkubwa katika sakata la Richmond.
Kamati hiyo iliituhumu TAKUKURU kuisafisha kampuni ya Richmond iliyopaswa kuzalisha umeme wa dharura, na ikapendekeza hatua zichukuliwe dhidi ya watendaji waliohusika katika mchakato wa kutoa zabuni kwa kampuni hiyo.
Hatua ya sasa ya TAKUKURU kuchunguza kamati za Bunge inadaiwa ni ya kulenga kupunguza makali ya Bunge, kupitia kwa wabunge hao hususan kipindi hiki ambacho Bunge linaonekana kuwa moja ya taasisi zinazoungwa mkono na kubeba matumaini ya Watanzania wengi.
Kwa mujibu wa habari zilizotufikia, TAKUKURU wamejipanga kutumia fursa za kisheria walizonazo kufanikisha mpango huo ikiwa ni sehemu ya kujibu mapigo ya wabunge, na mbali na Kamati ya Shelukindo iliyoshupalia Richmond, nyingine ni za Hesabu za Serikali za Mitaa inayoongozwa na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, inayoongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
Taarifa zilizotufikia zinaeleza kuwa mambo mbalimbali yameanza kuchunguzwa katika kamati hizo ikiwa ni pamoja na safari za wajumbe wa kamati hizo kwenye maeneo mbalimbali ya nchi na hususan malipo ya posho, yanayodaiwa kuwa yanalipwa zaidi ya mara moja, kinyume cha taratibu.
Raia Mwema ilizungumza na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila kuhusu suala hilo ana akasema ya kuwa hajapewa taarifa zozote kuhusu kuwapo kwa uchunguzi huo, lakini akaongeza ya kuwa TAKUKURU wanayo mamlaka kisheria kuendesha uchunguzi bila kutoa taarifa rasmi.
Wakati wa uchunguzi wa mchakato ulioipa zabuni ya kufua umeme wa dharura Richmond, TAKUKURU, kupitia kwa Mkurugenzi wake, Dk. Hosea, ilitoa taarifa ya uchunguzi kuhusu kashfa ya kuwapo kwa rushwa na upendeleo katika utoaji zabuni kwa Richmond, ikieleza kuwa hakukuwa na rushwa wala upendeleo.
Hata hivyo, ripoti hiyo ilibainika kupingana na uchunguzi wa sakata hilo uliofanywa na Kamati ya Teule ya Bunge, iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, ambayo ilianisha kasoro kadhaa, zikiwamo za kuwapo mazingira ya rushwa.
Kutokana na tofauti hiyo, kamati hiyo ilipendekeza bungeni Dk. Hosea na watendaji wengine mbalimbali serikalini, ambao ilidai walihusika na upendeleo wa utoaji zabuni kwa Richmond wawajibishwe, na Bunge liliafiki mapendekezo hayo na kuyapitisha kama mojawapo ya maazimio yake kuhusu sakata hilo.
Kwa kuzingatia hali na hasa baada ya Serikali kutoa taarifa yake katika mkutano uliopita bungeni, taarifa ambayo ilikataliwa na Bunge, msimamo wa Bunge dhidi ya TAKUKURU na hususan mkurugenzi wa taasisi hiyo si mzuri na wabunge kupitia mijadala bungeni wamekuwa wakishinikiza wawajibishwe, ikiwa ni pamoja na kujiuzulu.
Katika taarifa yake kuhusu adhabu aliyopewa Dk. Hosea, Serikali kupitia kwa Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja ilisema mkurugenzi huo amepewa onyo kwa kutokuwa makini kuhusu Richmond, hatua ambayo inapingwa na wabunge.
=========================
Katika hatua nyingine, taarifa zinasema Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inazichunguza kamati kadhaa za Bunge, ikiwa ni pamoja na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, ambayo ilihusika kuibua sakata la Richmond na kuiumbua TAKUKURU yenyewe.
Kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Bumbuli (CCM), William Shelukindo na makamu wake, Dk. Harrison Mwakyembe, ilipendekeza kuchukuliwa hatua kwa Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Dk. Edward Hosea, na wasaidizi wake kutokana na kushindwa kubaini udhaifu mkubwa katika sakata la Richmond.
Kamati hiyo iliituhumu TAKUKURU kuisafisha kampuni ya Richmond iliyopaswa kuzalisha umeme wa dharura, na ikapendekeza hatua zichukuliwe dhidi ya watendaji waliohusika katika mchakato wa kutoa zabuni kwa kampuni hiyo.
Hatua ya sasa ya TAKUKURU kuchunguza kamati za Bunge inadaiwa ni ya kulenga kupunguza makali ya Bunge, kupitia kwa wabunge hao hususan kipindi hiki ambacho Bunge linaonekana kuwa moja ya taasisi zinazoungwa mkono na kubeba matumaini ya Watanzania wengi.
Kwa mujibu wa habari zilizotufikia, TAKUKURU wamejipanga kutumia fursa za kisheria walizonazo kufanikisha mpango huo ikiwa ni sehemu ya kujibu mapigo ya wabunge, na mbali na Kamati ya Shelukindo iliyoshupalia Richmond, nyingine ni za Hesabu za Serikali za Mitaa inayoongozwa na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, inayoongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
Taarifa zilizotufikia zinaeleza kuwa mambo mbalimbali yameanza kuchunguzwa katika kamati hizo ikiwa ni pamoja na safari za wajumbe wa kamati hizo kwenye maeneo mbalimbali ya nchi na hususan malipo ya posho, yanayodaiwa kuwa yanalipwa zaidi ya mara moja, kinyume cha taratibu.
Raia Mwema ilizungumza na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila kuhusu suala hilo ana akasema ya kuwa hajapewa taarifa zozote kuhusu kuwapo kwa uchunguzi huo, lakini akaongeza ya kuwa TAKUKURU wanayo mamlaka kisheria kuendesha uchunguzi bila kutoa taarifa rasmi.
Wakati wa uchunguzi wa mchakato ulioipa zabuni ya kufua umeme wa dharura Richmond, TAKUKURU, kupitia kwa Mkurugenzi wake, Dk. Hosea, ilitoa taarifa ya uchunguzi kuhusu kashfa ya kuwapo kwa rushwa na upendeleo katika utoaji zabuni kwa Richmond, ikieleza kuwa hakukuwa na rushwa wala upendeleo.
Hata hivyo, ripoti hiyo ilibainika kupingana na uchunguzi wa sakata hilo uliofanywa na Kamati ya Teule ya Bunge, iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, ambayo ilianisha kasoro kadhaa, zikiwamo za kuwapo mazingira ya rushwa.
Kutokana na tofauti hiyo, kamati hiyo ilipendekeza bungeni Dk. Hosea na watendaji wengine mbalimbali serikalini, ambao ilidai walihusika na upendeleo wa utoaji zabuni kwa Richmond wawajibishwe, na Bunge liliafiki mapendekezo hayo na kuyapitisha kama mojawapo ya maazimio yake kuhusu sakata hilo.
Kwa kuzingatia hali na hasa baada ya Serikali kutoa taarifa yake katika mkutano uliopita bungeni, taarifa ambayo ilikataliwa na Bunge, msimamo wa Bunge dhidi ya TAKUKURU na hususan mkurugenzi wa taasisi hiyo si mzuri na wabunge kupitia mijadala bungeni wamekuwa wakishinikiza wawajibishwe, ikiwa ni pamoja na kujiuzulu.
Katika taarifa yake kuhusu adhabu aliyopewa Dk. Hosea, Serikali kupitia kwa Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja ilisema mkurugenzi huo amepewa onyo kwa kutokuwa makini kuhusu Richmond, hatua ambayo inapingwa na wabunge.