Hongereni: Wanawake wema bado mpo kwenye dunia hii

Hongereni: Wanawake wema bado mpo kwenye dunia hii

Sokoro waito

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2014
Posts
2,201
Reaction score
2,602
Habari za siku nyingi wadau wa MMU. Nimerudi baada ya kupotea siku nyingi kutokana na majukumu ya utu uzima.

Ningependa kuwapongeza wanawake wote walioolewa wenye uvumilivu wa kushinda dhoruba mbalimbali zinazokabili ndoa zao. Mimi kama mme wa mtu nimejifunza na kukubali ya kuwa kuna wanawake wavumilivu, kuna wanawake sahihi wanaoweza kuishi na wewe katika shida na raha.

Kwa uzoefu wangu nimewahi kupitia changamoto kadha zikiwemo za magonjwa zilizopelekea kuyumba kiuchumi lakini bado mke wangu alizidi kunisapoti katika dhiki zote hizo. Ukweli ni kuwa hata dunia ichafukeje na kunuka kwa uovu mwingi bado wanawake wanaomcha Mungu wapo.

Kama hujaoa jibidishe kumpata mwanamke aliye sahihi kwa ajili ya maisha ya ndoa.

Hongereni wanawake wacha Mungu, Hongereni wanawake mnaojibidisha kuwatendea mema waume zenu pasipo kukata tamaa.
 
Mbona wapo wanawake wanaofaa na tunawaona na kuwajua. tatizo wanawake vivuruge wana kamvuto flani hivi unajikuta tu unatamani kuwa nae na upo tayari kupambana na hali yako.
yaani kama mwanamke anavofall kwa bad boy
hili nalo neno mkuu, je tuseme kwamba ni law of atrraction inapelekea kuwa hivyo ama ni kitu gani?
 
daaah mkuu hongera afadhari umenipa moyo wa kuoa, ila mimi nitaoa humuhumu jf
na naamini atakuwa mwema kama wako,
na lazma nilete mrejesho
hahahahah
na iwe hivyo, songa mbele ipo neema ya kumpata wala usikatishwe tamaa mkuu. mkeo mwema yupo mahali, mtafute kwa bidii na kwa kusali..
 
Back
Top Bottom