Hongereni Hospitali Rufaa ya Kanda ya Mbeya

Hongereni Hospitali Rufaa ya Kanda ya Mbeya

HAKI KWA WOTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2022
Posts
2,691
Reaction score
2,303
Habarini,
Hivi karibuni nilileta hoja ya hospitali nyingi za serikali kuwaandikia dawa wagonjwa na kuwataka walipie dozi nzima na wakishalipia ndani ya muda mfupi wanabadilisha dawa na kuwataka walipie tena dozi nzima kitu ambacho huwatia hasara kubwa wagonjwa na badae kuondoka na mafurushi ya dawa zilizobaki.

Tofauti na hospitali nyingine za serikali hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya wamekuwa na utaratibu mzuri ambapo mgonjwa hulipia dawa alizoandikiwa kwa kila siku na inapotokea kabadirishiwa dawa basi anakuwa hajapata hasara yoyote.

Huu ni mfumo mzuri unaopaswa kuigwa na kufuatwa na hospitali nyingine zote za serikali na binafsi.

Naomba kuwasilisha.
 
Habarini,
Hivi karibuni nilileta hoja ya hospitali nyingi za serikali kuwaandikia dawa wagonjwa na kuwataka walipie dozi nzima na wakishalipia ndani ya muda mfupi wanabadilisha dawa na kuwataka walipie tena dozi nzima kitu ambacho huwatia hasara kubwa wagonjwa na badae kuondoka na mafurushi ya dawa zilizobaki.

Tofauti na hospitali nyingine za serikali hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya wamekuwa na utaratibu mzuri ambapo mgonjwa hulipia dawa alizoandikiwa kwa kila siku na inapotokea kabadirishiwa dawa basi anakuwa hajapata hasara yoyote.

Huu ni mfumo mzuri unaopaswa kuigwa na kufuatwa na hospitali nyingine zote za serikali na binafsi.

Naomba kuwasilisha.
Hii ndiyo maana halisi ya huduma kwa wananchi.
Bahati mbaya wengine huduma muhimu kama hizi na ambazo ni life saving, wao ndiyo wanaona fursa ya kuingiza mapato...ushetani kabisa.
Kama kweli Mbeya wanafanya hivyo basi wanastahili pongezi sana kwa kutimiza wajibu wao kama watumishi wa umma.
 
Back
Top Bottom