Uchaguzi 2020 Hongera Tundu Lissu kwa kumpigia kampeni Magufuli leo

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Sep 4, 2019
1,395
3,901
Mimi nafuatilia kwa umakini sana hoja za wapinzani wetu ADC,NCCR MAGEUZI, CHADEMA, SAU, ACT WAZALENDO, CUF, kwa Leo nimemfuatilia kwa umakini sana Tundu lisu labda pengine angekuwa na jipya la kuifanyia nchi yetu lakini nimegundua kuwa ametembelea kwenye mafanikio makubwa ya Magufuli. Ahsante sana TAL, keep it up!

MOSI
TAL ametambua uwepo wa miradi mikubwa iliyofanywa na Serikali kama ununuzi wa ndege, ujenzi wa bwawa kubwa la umeme, na ujenzi wa miundombinu mikubwa kama reli hongera sana TAL kwa kumuongezea credit Magufuli.

Pamoja na kuyaongelea katika mitazamo hasi lakini tunashukuru kwa kutambua kuwa miradi hiyo IPO na imejengwa kwenye Kampeni sisi tutajikita kwenye hoja za kuelezea zaidi umuhimu wa miradi hii tutatumia nyimbo na ngonjera kufikisha ujumbe kwa Watanzania.

Tunaenda kusheherekea mafanikio haya makubwa ya serikali ya awamu ya Tano tunaenda kufanya sherehe ya miezi miwili tutaimba tutacheza na mnamo tarehe 28/10/2020 tutamtuza Magufuli tuzo ya umahiri wa mafanikio aliyoyafanya kwa miaka 5 kwa kumpa ushindi wa zaidi ya 90%

TAL ameongeleo kero za wakulima na wafanyakazi, nampongeza sana mgombea urais wa Chadema kwa kutambua matatizo haya lakini yaweza kuwa labda alikuwa Ubeligiji hajajua kuwa kero anazozisemea Magufuli aliziongelea 2015 kuwa na yeye zinamkera na amezishughulikia kweli kweli kisawa sawa amezikemea kisawa sawa amezidhibiti vilivyo amefukuza watu wengi waliowachokonoa wakulima na wafugaji amefuta tozo zaidi ya 84, yaani Magufuli ametenda uliyoyasema tutamtuza kwa ushindi wa zaidi ya 90% tarehe 28/10/2020.

Kitu pekee ambacho sijapenda kutoka kwako ni kupunguza kejeli leo, maana bila kejeli wewe si maarufu tena; bila kashifa wewe si maarufu tena kwa wafuasi wako wasio na busara ambao sisi hao wafuasi wako tunawatafuta sana ukipunguza kashfa hawakusilizi na ukiongeza kashifa wanakupuuza, kazi unayo.

Mheshimiwa Magufuli hajaharibu uhusiano wowote na nchi yoyote Duniani bali anaiheshimisha Tanzania tofautisha Kiburi na msimamo Magufuli ameonyesha msimamo wala si kiburi ameonyesha msimo kuzuia uporwaji wa Tanzanite yetu yaani Tanzanite ya Tanzania iuzwe zaidi kenya na India hafu na wewe ukenue meno ushangilie kuwa tuna uhusiano mzuri wanakuona huna akilli.

Tofautisha Beberu na mwekezaji yaani mwekezaji akiwa mnyonyaji tunamuita beberu na beberu akiwa na win-win situation tunamuita mwekezaji, mbona simple tu mtu au binadamu akiwa hospitali anaitwa mgonjwa akiiba anaitwa mwizi.

Mimi najua hata beberu ni kupe mwenye njaa mnyonya damu balaa huyu huwezi kumshangilia.

Labda mmesahau kuwa nyie hao hao mliojiita wapinzani mlilalamika sana juu ya safari za Rais, mlituupuuza sana juu ya Rasilimali za nchi yetu, mlitupuuza sn juu ya uhaba wa ndege tumefanya zaidi ya matarajio yenu mbona mwataka kuwa nguzo ya chumvi

Kuhusu majanga labda wewe hujui vizuri kwa sababu ulikuwa ubeligiji ni hivi Tanzania tumepambana na janga la Corona ambalo ni janga baya zaidi kuikumba Dunia kwa ufanisi makubwa sana hatukuguswa hata na rungu wala kiboko tumevuka salama kabisa huu ushindi wa Corona kwa kumtanguliza Mungu mbele unaharamisha hoja yako tumeona kwa macho huruma ya Magufuli ameandikwa na vitabu mbalimbali vya Dunia na ameingizwa kwenye jarida la watu wenye upeo mkubwa zaidi wa akili Dunia unaambiwa akili na IQ ya Magufuli iko level moja na akina Albeit Einstein baba wa Quantum Physics and relativity.

TAL Magufuli anakuzidi akili Mara nyingi sana ukipata 5% ya kura utakuwa umepigana sana jiandae kisaikolojia usije ukaumia mara ya pili maumivu ya kisaikolojia ni makali sana na yanatesa kuliko kawaida.
 
Leo mzee wa kutoa boko kaongea kama mtu mwenye kutaka urais. Hakujawa na mihemko na jazba.

Ni jambo jema anashaurika anabadilika ingawa kachelewa kiasi chake the damage has been done.
Wafuasi wake wanapenda atukane asipotukana hawapendi akiongea hoja za maana ansmpigia Kampeni Magufuli, kwanza Lisu kwa Chato na watu wanaozunguka pori la Burigi yaani Geita, Kagera hatapata kura ameponda uanzishwaji wa hilo pori bila kujua kuwa hiyo hifadhi ina manufaa makubwa kwa nchi.
 
Hata mimi nimesikiliza ile hotuba yote sikuona substance yoyote; ni ya kijiweni zaidi. Yaani ameshindwa kuonyesha tofauti ya miradi mipya na miradi iliyokuwepo, eti anasema kuwa ununuzi wa ndege siyo jambo jipya wakati ni wazi kuwa Tanzania hakukuwa na ndege kabisa kabla ya mwaka 2016 ingawa Nyerere aliacha ndege 14 wakati wake. Anaonyesha kuchukia matumizi ya neno mabeberu, wakati ni neno la siku nyingi sana lilioanza tangu mwaka 1967. Kuna sehemu ameonyesha kusifia hata utawala wa Nyerere wakati aliwahi kusema kuwa Nyerere alikuwa ni mwongo na dikteta.

Mambo mengine kuhusu maisha ya watu huko vijijini aliyoongea ni kufikirika zaidi ya ukweli. Kuna mambo aliyoongea ambayo siyo ya kweli, na sidhani kama kweli kuna watu wa vijijini watamwelewa.
 
Nigrastratatract,

Wanaodai Jiwe kaiheshimisha Tanzania, kaiheshimisha kwa nchi gani, Burundi? Hebu tuache ushamba na kuishi enzi za ujinga wa wakati wa chama kimoja. This country is a now a big joke in the eye of the international community. Hakuna mwekezaji serious anakuja hapa kuwekeza kutokana na nchi yetu kuwekwa miongoni mwa nchi zenye political instability kama mojawapo ya vigezo muhimu vya kiuchumi viitwavyo PEST.

Kuhusu kejeli kwenye siasa za ushindani, nadhani sumu ya hofu ya Jiwe imewaingia wengi mpaka mmeamini kwamba ukimkejeli Rais kama mgombea wa chama cha siasa umeitukana nchi na si mzalendo. What a load of rubbish!!

Kuongea kwa kejeli dhidi ya mpinzani wako ni moja ya communication strategies inayotumiwa ku lighten up the audience. Inasaidia ku keep interest of the listeners. Hata CCM wanaotumia Sana. Hata Jiwe juzi alipochukua fomu aliongea kwa kejeli dhidi ya wapinzani alioposema amejenga barabara na wanaompinga wanapitia.. amejenga hospital na walevi wanatibiwa.

Tutafute kitu kingine cha kumkosoa TL. Huyu tu ndiyo kiboko ya Jiwe na CCM kwenye uchaguzi huu, wajipange tu kisawa sawa.
 
Wafuasi wake wanapenda atukane asipotukana hawapendi akiongea hoja za maana ansmpigia Kampeni Magufuli, kwanza Lisu kwa Chato na watu wanaozunguka pori la Burigi yaani Geita, Kagera hatapata kura ameponda uanzishwaji wa hilo pori bila kujua kuwa hiyo Hifadhi ina manufaa makubwa kwa nchi
Lakin yote hamna uwezo wa kuyatangaza matokeo halali.
 
Hata mimi nimesikiliza ile hotuba yote sikuona substance yoyote; ni ya kijiweni zaidi. Yaani ameshindwa kuonyesha tofauti ya miradi mipya na miradi iliyokuwepo, eti anasema kuwa ununuzi wa ndege siyo jambo jipya wakati ni wazi kuwa Tanzania hakukuwa na ndege kabisa kabla ya mwaka 2016 ingawa Nyerere aliacha ndege 14 wakati wake. Anaonyesha kuchukia matumizi ya neno mabeberu, wakati ni neno la siku nyingi sana lilioanza tangu mwaka 1967. Kuna sehemu ameonyesha kusifia hata utawala wa Nyerere wakati aliwahi kusema kuwa Nyerere alikuwa ni mwongo na dikteta.

Mambo mengine kuhusu maisha ya watu huko vijijini aliyoongea ni kufikirika zaidi ya ukweli. Kuna mambo aliyoongea ambayo siyo ya kweli, na sidhani kama kweli kuna watu wa vijijini watamwelewa.

Huyu mgombea ameshachuja sana tatizo lake amekaa sn Ubeligiji amezungukwa na watu ambao hawamwambii ukweli wanampotosha ndiyo maana akina Zito wamegundua kuwa kumtukana JPM ni kuwatukana Watanzania wamejikita kwenye hoja hawashambulii MTU, TAL Lazima ajue kuwa Magufuli amejitoa kwa ajili ya nchi hii Leo asingewalipa wale boda boda angebakia mwenyewe barabarani yaaani ameaibika Dodoma balaa, amekuwa na moto wa Mabua sana yaani kwa kweli amechuja ile mbaya hii ni kwa sababu analazimisha umaarufu inawezekanaje?

Yaani Leo isingekuwa boda boda haki ya Mungu angebaki pekee yakeee atazomewa huyu MTU Watanzania tunamhitaji sana Magufuli
 
Hata mimi nimesikiliza ile hotuba yote sikuona substance yoyote; ni ya kijiweni zaidi. Yaani ameshindwa kuonyesha tofauti ya miradi mipya na miradi iliyokuwepo, eti anasema kuwa ununuzi wa ndege siyo jambo jipya wakati ni wazi kuwa Tanzania hakukuwa na ndege kabisa kabla ya mwaka 2016 ingawa Nyerere aliacha ndege 14 wakati wake. Anaonyesha kuchukia matumizi ya neno mabeberu, wakati ni neno la siku nyingi sana lilioanza tangu mwaka 1967. Kuna sehemu ameonyesha kusifia hata utawala wa Nyerere wakati aliwahi kusema kuwa Nyerere alikuwa ni mwongo na dikteta.

Mambo mengine kuhusu maisha ya watu huko vijijini aliyoongea ni kufikirika zaidi ya ukweli. Kuna mambo aliyoongea ambayo siyo ya kweli, na sidhani kama kweli kuna watu wa vijijini watamwelewa.

Lissu ana hoja nzito ni vizuri tujipange.. Deni la Tril 40 ni kubwa sana.. Bora JK aliondoka amekopa Tril 8 tuu.. Ila linalipika kwa kutoana damu ofcoz..

Mkapa alipandisha GDP per capita kutoka dola 150 mpaka 500.. JK yeye akaipandisha mpaka 1000.. Huyu yeye kwa miaka mitano kapandisha mpaka dola 1080.. Pamoja ni mikopo yote aliyokopa..

Kama chama tujipange kusema kweli.. Huu sio wakati wa kusifia pekee..
 
Wanaodai Jiwe kaiheshimisha Tanzania, kaiheshimisha kwa nchi gani, Burundi? Hebu tuache ushamba na kuishi enzi za ujinga wa wakati wa chama kimoja. This country is a now a big joke in the eye of the international community. Hakuna mwekezaji serious anakuja hapa kuwekeza kutokana na nchi yetu kuwekwa miongoni mwa nchi zenye political instability kama mojawapo ya vigezo muhimu vya kiuchumi viitwavyo PEST.

Kuhusu kejeli kwenye siasa za ushindani, nadhani sumu ya hofu ya Jiwe imewaingia wengi mpaka mmeamini kwamba ukimkejeli Rais kama mgombea wa chama cha siasa umeitukana nchi na si mzalendo. What a load of rubbish!!

Kuongea kwa kejeli dhidi ya mpinzani wako ni moja ya communication strategies inayotumiwa ku lighten up the audience. Inasaidia ku keep interest of the listeners. Hata CCM wanaotumia Sana. Hata Jiwe juzi alipochukua fomu aliongea kwa kejeli dhidi ya wapinzani alioposema amejenga barabara na wanaompinga wanapitia.. amejenga hospital na walevi wanatibiwa...

Tutafute kitu kingine cha kumkosoa TL. Huyu tu ndiyo kiboko ya Jiwe na CCM kwenye uchaguzi huu, wajipange tu kisawa sawa.

Hata mm nilijuwa kuwa TAL angetoa ushindani kwa Magufuli amepwaya sn tatizo ni moja tu anamtukana Magufuli amejaa jazba anatakiwa awe mwanaharakati lakini si Mgombea Urais, ACT wazalendo ndio watatoa Upinzani mkali wamejipanga sana nimeamini kuwa Zito Kabwe ndiye mwanasiasa anayejenga hoja zikaeleweka, namhofia zaidi Membe kuliko huyu lopolopo yaani kama ni Vitani ameshindwaa vibaya madhaifu yake yote yanajulikana hakika ndani ya siku 60 either atukane sana atende jinai au ajichanganye kumpigia Kampeni Magufuli tuliwaonya Kuwa Magufuli ni level zingine mkapuyaaanga sasa tutawapa adhabu Kali ya kuwaadhibu kwenye sanduku la kura nawahakikishieni mkipata 5% ya kura zote team Lisu shangilieni sana inaonesha kwamba mgombea wenu anatakiwaa apimwee akili
 
Hata mm nilijuwa kuwa TAL angetoa ushindani kwa Magufuli amepwaya sn tatizo ni moja tu anamtukana Magufuli amejaa jazba anatakiwa awe mwanaharakati lakini si Mgombea Urais, ACT wazalendo ndio watatoa Upinzani mkali wamejipanga sana nimeamini kuwa Zito Kabwe ndiye mwanasiasa anayejenga hoja zikaeleweka, namhofia zaidi Membe kuliko huyu lopolopo yaani kama ni Vitani ameshindwaa vibaya madhaifu yake yote yanajulikana hakika ndani ya siku 60 either atukane sana atende jinai au ajichanganye kumpigia Kampeni Magufuli tuliwaonya Kuwa Magufuli ni level zingine mkapuyaaanga sasa tutawapa adhabu Kali ya kuwaadhibu kwenye sanduku la kura nawahakikishieni mkipata 5% ya kura zote team Lisu shangilieni sana inaonesha kwamba mgombea wenu anatakiwaa apimwee akili

Tuwe wakweli wanaCCM wenzangu. TAL ndio tishio na ndio maana humu tumemkomalia. Tuwe wakweli tu. Tusipende kujitekenya wenyewe. Tuwe wakweli kama wanaume wa chama dume kweli.
 
Lissu ana hoja nzito ni vizuri tujipange.. Deni la Tril 40 ni kubwa sana.. Bora JK aliondoka akaacha deni la Tril 8.. Ila linalipika kwa kutoana damu ofcoz..

Mkapa alipandisha GDP per capita kutoka dola 150 mpaka 500.. JK yeye akaipandisha mpaka 1000.. Huyu yeye kwa miaka mitano kapandisha mpaka dola 1080.. Pamoja ni mikopo yote aliyokopa..

Kama chama tujipange kusema kweli.. Huu sio wakati wa kusifia pekee..
Hii ni matokeo ya kuongea maneno ya kufikirika na kupikwa tu. Madeni ya Tanzania kwa miaka 10 iliyopita ni kama ifuatavyo hapa kwenye image hii; je na wewe unaamini kuwa kuanzia mwaka 2015 madeni ya Tanzania yamepanda sana kufikia hiyo namba hiyo ya uwongo? Ameitoa wapi?

1596931783253.png
 
Lissu ana hoja nzito ni vizuri tujipange.. Deni la Tril 40 ni kubwa sana.. Bora JK aliondoka akaacha deni la Tril 8.. Ila linalipika kwa kutoana damu ofcoz..

Mkapa alipandisha GDP per capita kutoka dola 150 mpaka 500.. JK yeye akaipandisha mpaka 1000.. Huyu yeye kwa miaka mitano kapandisha mpaka dola 1080.. Pamoja ni mikopo yote aliyokopa..

Kama chama tujipange kusema kweli.. Huu sio wakati wa kusifia pekee..
Hoja yenyewe kaambiwa na mnyika yaani Leo jamaa ndo kavuruga nahisi alikuwa na sonona baada ya kukosa wa kumpokea akawa anapungia majengo tu kwa kweli amepwaya ngoja akina Lipumba waje na nondo uone sasa nini maana ya professional za watu yaliyotokea Dodoma kwa lopolopo ni funzo kubwa kwa wasaliti wa nchi wasipochanganyikiwa watalaaniwa na Watanzania wote, wewe lopolopo ulithubutu vipi kuwaambia Mabeberu watuwekee vikwazo umejikalisha wamekubagua weeeh ukaonaa bora home tunakuambia usinyee kabi, Deni la Taifa kukua ujue nchi yetu inatajirika
 
Lissu ana hoja nzito ni vizuri tujipange.. Deni la Tril 40 ni kubwa sana.. Bora JK aliondoka amekopa Tril 8 tuu.. Ila linalipika kwa kutoana damu ofcoz..

Mkapa alipandisha GDP per capita kutoka dola 150 mpaka 500.. JK yeye akaipandisha mpaka 1000.. Huyu yeye kwa miaka mitano kapandisha mpaka dola 1080.. Pamoja ni mikopo yote aliyokopa..

Kama chama tujipange kusema kweli.. Huu sio wakati wa kusifia pekee..
Opportunity cost unaielewa?? U can not eat a cake and still continue to have
 
Back
Top Bottom