Hongera Taifa Stars na poleni kwa uchovu

kiLimIlire

JF-Expert Member
Apr 8, 2012
311
639
Sikubaliani na wote wanaobeza kile kilichofanywa na Taifa Starz katika mechi ya leo dhidi ya Senegal katika mashindano ya AFCON. Nasema hivyo si kwa kuwa sijui soka bali kwa kuwa kati ya milioni zaidi ya 50 tuliopo nchini hapa hao ndio wameweza kuwepo uwanjani kutuwakilisha, bila shaka wao ndio bora kuliko sie wengine, vinginevyo nasi tungekuwa kati yao.

Sasa basi hatupaswi kuwakatisha tamaa, kila mmoja wapo alionekana kujituma vilivyo, jasho limewatoka haswa, kama mfumo haukuwa mzuri ni kwa kuwa walivurungwa na wapinzani wao Senegal ambao kwa takwimu za ubora wa soka barani Africa wanashika namba moja, sisi tukiwa wa 36.

Kubwa kabisa ni maumbo ya wachezaji, tofauti kati yao na sisi ni kubwa kubwa mno, kwa waliowahi kucheza soka wanafahamu kabisa ilivyoshida sana kukabiliana na mtu anayekuzidi mwili, wakati ukijaribu kuupata mpira yeye huuweka mbali na wewe akiwa kakukinga na mwili wake, ukikaza sana utaishia kumkwatua na kusababisha faulo kama ambavyo mmeshuhudia katika mechi hii, na kuambulia kadi za njano kadhaa na nyingine kuachwa kwa huruma ya mwamuzi.

Hivyo basi, kama ni lawama tuzibebe watanzania wote kabisa kwa kupungukiwa mikakati ya kuwapata wachezaji bora zaidi ya hawa tulionao. Na tatizo kuu kabisa ni kushindwa kupata wachezaji wenye maumbo makubwa miongoni mwetu. Najiuliza, hivi ni kweli kwamba hatuna vinasaba vya watu warefu wa kulisaidia taifa? Hatuna watu wanaoliona hilo!! Kuna wakati ili kujiunga na majeshi yetu kimo kilizingatiwa sana, sera hiyo inaweza kutumika sasa katika timu za watoto, academy mbalimbali na hatimae tukaepuka unyonge wa kuonekana watoto mbele ya timu za Africa Magharibi. Katika mechi hii hata Bocco alionekana mdogo kiumbo.
Poleni wachezaji wa leo kwa shughuli ya leo, fanyeni lililo ndani ya uwezo wenu msijefia uwanjani kwa mipango yetu dhaifu..

Amunike asilaumiwe na mambo ya vyama vya siasa yasiingizwe kwenye mjadala huu, sio kila mtanzania ni mwanasiasa ila Taifa stars ni ya kila mtanzania.
 
Sasa kama hutaki tumlaumu amunike tumlaumu nani? tangu lini samata akawa namba 9 tangu lini boko akawa winga? yule kessy nae ni beki?
 
Sawa kada mtiifu naona ulikua usha andaa na waraka kabsa
nigerian_panda-20190623-0001.jpeg
 
Sasa kama hutaki tumlaumu amunike tumlaumu nani? tangu lini samata akawa namba 9 tangu lini boko akawa winga? yule kessy nae ni beki?
Sasa wewe unataka kutuaminisha kuwa kuna Taifa Stars nyingine iloachwa na Amunike!! Kama hao wengine hawakuwa na nidhamu, tayari walikosa vigezo, sioni kama kuna aliyeachwa ambaye angebadilo haya matokeo. Goli la pili ilikuwa kiki moja matata, ni goli la kisoka kabisa! Huo ndo uwezo wetu. Nitafurahi kabisa ukiwapa lawama Uganda Cranes kwa kutupa fursa ya kushiriki haya mashindano, kama una matumaini yoyote katika mashindano haya kwa Taifa Stars futa kabisa, ila sio sababu ya kulaumu kocha na wachezaji wakati wewe ni "keyboard worrior".
 
Wamejitaidi sana pongezi kwao, ila kocha nae atazamwe upya.
Mkuu asante kwa kuwa na mtazamo chanya kwanza! Ila huyu kocha anayelaumiwa kwa udhaifu si ndo katupeleka huko ambako hatujawahi kwenda kwa zaidi ya miongo mitatu!! Yawezekana analo jicho la kisoka zaidi kuliko sisi. Yawezekana akiangaza huku na kule haoni wa kumletea sifa zaidi ya hao alionao sasa, angekuwa huru kuchukua kwao na kuwaunga kwetu pengine angeeleweka anachokimaanisha. Mchunguze akiwa uwanjani, hulengwa na machozi timu inapofanya fyongo... Sidhani kama yeye ni shida.
 
Siasa za nchi zishatuvuruga sana, nimetoa tahadhari mapema hakuna kuingiza siasa hapa. Unavuruga mjadala Mkuu. Kama unashindwa kumudu sharti jepesi hivyo, vipi ukipewa namba Taifa Stars ukabane na Sadio Mane! Si atakujamb*sha wewe...
Waulize walioigeuza kuwa timu ya kutekeleza Ilani ya chama chao.
 
Acha uongo wewe Samuel etoo ana mwili mdogo lakini ni mchezaji bora duniani
Nazungumzia timu, timu ni zaidi ya mtu mmoja!Huyo e'too si alikuwa na kina Song na majabari mengineyo! Na ni nani hasa pale Star unamfananisha na E'too... Kwa hizi akili acha tufungwe tu!
 
Sikubaliani na wote wanaobeza kile kilichofanywa na Taifa Starz katika mechi ya leo dhidi ya Senegal katika mashindano ya AFCON. Nasema hivyo si kwa kuwa sijui soka bali kwa kuwa kati ya milioni zaidi ya 50 tuliopo nchini hapa hao ndio wameweza kuwepo uwanjani kutuwakilisha, bila shaka wao ndio bora kuliko sie wengine, vinginevyo nasi tungekuwa kati yao.

Sasa basi hatupaswi kuwakatisha tamaa, kila mmoja wapo alionekana kujituma vilivyo, jasho limewatoka haswa, kama mfumo haukuwa mzuri ni kwa kuwa walivurungwa na wapinzani wao Senegal ambao kwa takwimu za ubora wa soka barani Africa wanashika namba moja, sisi tukiwa wa 36.

Kubwa kabisa ni maumbo ya wachezaji, tofauti kati yao na sisi ni kubwa kubwa mno, kwa waliowahi kucheza soka wanafahamu kabisa ilivyoshida sana kukabiliana na mtu anayekuzidi mwili, wakati ukijaribu kuupata mpira yeye huuweka mbali na wewe akiwa kakukinga na mwili wake, ukikaza sana utaishia kumkwatua na kusababisha faulo kama ambavyo mmeshuhudia katika mechi hii, na kuambulia kadi za njano kadhaa na nyingine kuachwa kwa huruma ya mwamuzi.

Hivyo basi, kama ni lawama tuzibebe watanzania wote kabisa kwa kupungukiwa mikakati ya kuwapata wachezaji bora zaidi ya hawa tulionao. Na tatizo kuu kabisa ni kushindwa kupata wachezaji wenye maumbo makubwa miongoni mwetu. Najiuliza, hivi ni kweli kwamba hatuna vinasaba vya watu warefu wa kulisaidia taifa? Hatuna watu wanaoliona hilo!! Kuna wakati ili kujiunga na majeshi yetu kimo kilizingatiwa sana, sera hiyo inaweza kutumika sasa katika timu za watoto, academy mbalimbali na hatimae tukaepuka unyonge wa kuonekana watoto mbele ya timu za Africa Magharibi. Katika mechi hii hata Bocco alionekana mdogo kiumbo.
Poleni wachezaji wa leo kwa shughuli ya leo, fanyeni lililo ndani ya uwezo wenu msijefia uwanjani kwa mipango yetu dhaifu..

Amunike asilaumiwe na mambo ya vyama vya siasa yasiingizwe kwenye mjadala huu, sio kila mtanzania ni mwanasiasa ila Taifa stars ni ya kila mtanzania.


Ahsante kwa uchambuzi. Tatizo kila kitu Tanzania tumekiwekeza kwenye siasa. Na bado.
 
Ahsante kwa uchambuzi. Tatizo kila kitu Tanzania tumekiwekeza kwenye siasa. Na bado.
Karibu Mkuu. Na siasa haziwezi kutufikisha kwenye mafanikia halisi, wale vijana wa Stars wamepambana tuwape pole! Yale matokeo sio yao ni ya kwetu na yanatokana na mipango isiyofaa
 
Waulize hao walioamua kuipora Taifa Stars na kuifanya ya maccm, mbona hata hayakuwepo awamu ya nne!? 😳

Mkuu unataka kusema tumefikia hapa kila kitu lazima kihusishwe na ushindani wa kisiasa nchini!!
 
Sasa wewe unataka kutuaminisha kuwa kuna Taifa Stars nyingine iloachwa na Amunike!! Kama hao wengine hawakuwa na nidhamu, tayari walikosa vigezo, sioni kama kuna aliyeachwa ambaye angebadilo haya matokeo. Goli la pili ilikuwa kiki moja matata, ni goli la kisoka kabisa! Huo ndo uwezo wetu. Nitafurahi kabisa ukiwapa lawama Uganda Cranes kwa kutupa fursa ya kushiriki haya mashindano, kama una matumaini yoyote katika mashindano haya kwa Taifa Stars futa kabisa, ila sio sababu ya kulaumu kocha na wachezaji wakati wewe ni "keyboard worrior".
tatizo sio kufungwa tatizo mihezaji kashindwa kuifundisha hata kutoa pasi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom