Hongera Rais Samia kwa 'Kuchomoa' leo kwenda kwenye Tamasha la Kiislamu wakati leo ni Pasaka Kuu kwa Wakristo wote

Na walikutega kwa Makusudi kwa kukufanya Wewe ndiyo Mgeni rasmi katika Tukio hilo lililofanyika katika Sikukuu ya Pasaka yenye Heshima Kubwa kwa Wakristo (GENTAMYCINE nikiwemo) ili waanze Kututambia kuwa sasa hivi ni zamu yao na watafanya watakavyo kwakuwa tu Wewe ni Mwenzao.

GENTAMYCINE nilipiga sana Kelele hapa hapa JamiiForums kuwa usiende na kwamba hata timing ya Tukio (hasa kwa tarehe) husika ambayo kwa Wakristo wote duniani ni Siku ya Pasaka ambayo inaheshimika na ina nguvu Kwetu Kiimani.

Shukran Kwako Mheshimiwa Rais Samia kwa Kutoenda huko Uwanjani na badala yake ukatuma tu Mtu akuwalishe ambaye ni Rais wa Zanzibar Isles Dk Hussein Ali Mwinyi.

Kiitifaki na hata Kikatiba (bila kusahau Uzito wake Kimapokeo) kuna tofauti Kubwa sana kati ya Wewe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan Kulihudhuria hilo Shindano na Rais wa Visiwa vya Zanzibar (iliyomo ndani ya Tanzania) Dk. Hussein Ali Mwinyi ambaye amehudhuria kwa Kukuwakilisha.

Umeukwepa vyema mno huu Mtego na kama Washauri wako nao waliliona limekaa vibaya kama na Mimi nilivyoliona na Kukushauri Uchomoe / Usiende basi nawapongeza mno kwani lingekuharibia hasa upande wa Wakristo ambao ndiyo wana Ushawishi mkubwa.

Na kama upo hapa JamiiForums na unadhani haya Maoni yetu au hizi Mada zetu huwa hazisomwi unakosea sana kwani 99% ya Mada za hapa huwa zina impact kubwa mno ya Kimabadiliko baada ya Ujumbe kufika / kuwafikia Walengwa.

Kama kawaida najua hapa sitoeleweka mapema na wenye Uhaba wa Akili Vichwani mwao, ila kwa wale Werevu wachache watakaonielewa Kiundani zaidi mbarikiwe nyote.
Rais Mwinyi yeye yuko wazi kuwa ni waisilamu na yuko kuukuza uisilamu.
 
Back
Top Bottom