Hongera mheshimiwa Zitto kuisemea Tabora

Hongera mheshimiwa Zitto kuisemea Tabora

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,707
Reaction score
1,729
Leo katika kipindi cha maswali na majibu kwa upande wa wizara ya ujenzi alimuuliza waziri swali na nyongeza kuhusu kusimama kwa makandarasi wanaojenga barabara za kuunganisha Tabora na mikoa mingine kwa kiwango cha lami.

Nilimuona akiwa na uchungu mno lakini jibu lililotoka kwa waziri husika kama kawaida ya mkoa wa Tabora majibu ya matatizo yake huwa ni siasa zaidi na nadhani hata mbunge wake haoni sababu ya kuutetea.
 
Nadhani Tabora ipo katika top 3 ya mikoa masikini nchini kama sikosei.
 
Nadhani Tabora ipo katika top 3 ya mikoa masikini nchini kama sikosei.
Ndibalema,kwa nini mkoa kama Tabora usiwe masikini?

Unadhani kuchagua wabunge kama Rage ambao kwao kutetea CCM wanadhani ndicho kilichowapeleka DODOMA kutakuwa na tija kweli? Ni wakati wa wana Tabora kufunguka macho na kujua bila kuiacha CCM umasikini utawaganda kama kupe.

Hongera Zito kwa kuonyesha kuwa wabunge wa CHADEMA huwa ni wa kitaifa pia.
 
Leo katika kipindi cha maswali na majibu kwa upande wa wizara ya ujenzi alimuuliza waziri swali na nyongeza kuhusu kusimama kwa makandarasi wanaojenga barabara za kuunganisha Tabora na mikoa mingine kwa kiwango cha lami.

Nilimuona akiwa na uchungu mno lakini jibu lililotoka kwa waziri husika kama kawaida ya mkoa wa Tabora majibu ya matatizo yake huwa ni siasa zaidi na nadhani hata mbunge wake haoni sababu ya kuutetea.
kama kawaida ya wabunge wa Tabora - ni utiii katika chama hata kuhoji vitu vya maslahi wa wananchi wao wanashindwa - Zitto tusaidie sisi wanyamwezi tuna utii wa uwoga.
 
Tabora haina tofauti na Mkoa wa Tanga, inahitaji ikombolewe, kazi yao kuchagua wabunge wa ccm, halafu wanadharauliwa na ccm, maendeleo ziro@gmail.com
 
kama kawaida ya wabunge wa Tabora - ni utiii katika chama hata kuhoji vitu vya maslahi wa wananchi wao wanashindwa - Zitto tusaidie sisi wanyamwezi tuna utii wa uwoga.

zitto jembe,, tena makao makuu wangempa kazi ya kudili na mikoa ya pwani tuu!
 
Wabunge wa Tabora na dhana ya utii bila shuruti. Naunga hoja mkono asilimia 100.
 
Watu hupata viongozi wanaowastahili, wanatabora wanavuna walichopanda.
 
Ndibalema,kwa nini mkoa kama Tabora usiwe masikini?

Unadhani kuchagua wabunge kama Rage ambao kwao kutetea CCM wanadhani ndicho kilichowapeleka DODOMA kutakuwa na tija kweli? Ni wakati wa wana Tabora kufunguka macho na kujua bila kuiacha CCM umasikini utawaganda kama kupe.

Hongera Zito kwa kuonyesha kuwa wabunge wa CHADEMA huwa ni wa kitaifa pia.
Kwahiyo mkuu unamaanishi ni wana Tabora wenyewe ndio wanajitakia?
Unfikiri tatizo ni nini mpaka wanatabora wasiamke na kubadilika?
 
Ule usemi wa mh.Zitto kuwa yeye ni mbunge wa Kitaifa unaonekana kuwa unaukweli ndani yake. Hii ni kutokana na kutumia nguvu nyingi kuzungumzia na kutetea maslahi ya taifa na si maslahi ya jimbo lake. Mh. Mnyika J.J hutumia nguvu nyingi kutetea maslahi ya jimbo lake sawa na nguvu ileile anayotumia kutetea maslahi ya kitaifa. Jimbo la kigoma kaskazini kuna changamoto nyingi zinazohitaji utatuzi wa haraka. Mazao ya chikichi,kahawa na ndizi hayajapata
ufumbuzi na uratibu mzuri wa masoko hivyo yameshindwa kuwakomboa wana Kigoma kiuchumi. Tatizo sugu la maji linahitaji ufumbuzi pia. Tunakushauri mh. Zitto uige mfano wa mh. Mnyika J.J
 
Ukifuatilia vizuri namna tulivo wa Tz,Historia yetu na Nature ya mipango mikakati ya nchi hii ni bora kuwa kama Mh.Zitto-Mimi nadhani anajua na anaamini"UKIMUUA SIMBA MWITUNI BASI MWITU WOTE UTAKUWA CHINI YAKO" Ndugu yupo vizuri katka kukabiliana na MASIMBA
 
Ule usemi wa mh.Zitto kuwa yeye ni mbunge wa Kitaifa unaonekana kuwa unaukweli ndani yake. Hii ni kutokana na kutumia nguvu nyingi kuzungumzia na kutetea maslahi ya taifa na si maslahi ya jimbo lake. Mh. Mnyika J.J hutumia nguvu nyingi kutetea maslahi ya jimbo lake sawa na nguvu ileile anayotumia kutetea maslahi ya kitaifa. Jimbo la kigoma kaskazini kuna changamoto nyingi zinazohitaji utatuzi wa haraka. Mazao ya chikichi,kahawa na ndizi hayajapata
ufumbuzi na uratibu mzuri wa masoko hivyo yameshindwa kuwakomboa wana Kigoma kiuchumi. Tatizo sugu la maji linahitaji ufumbuzi pia. Tunakushauri mh. Zitto uige mfano wa mh. Mnyika J.J

Hivi Mnyika huwa anapigania haki za wana Ubungo au anapigania kuonekana kwenye runinga kuwa ni muongeaji?
 
Ukifuatilia vizuri namna tulivo wa Tz,Historia yetu na Nature ya mipango mikakati ya nchi hii ni bora kuwa kama Mh.Zitto-Mimi nadhani anajua na anaamini"UKIMUUA SIMBA MWITUNI BASI MWITU WOTE UTAKUWA CHINI YAKO" Ndugu yupo vizuri katka kukabiliana na MASIMBA

Ukimuona mtu anamponda ZITTO ujue huyo ni pro-SLAA na MBOWE so anajaribu kumdhoofisha mheshimiwa jambo ambalo ni vigumu sana, ZITTO mtu wa watu bwana siyo hao hao wengine.
 
I don't think so. "Ukiona adui yako anakusifia jua kuwa kuna kitu au kazi imekushinda" by Nchibi bungeni.

Ukimuona mtu anamponda ZITTO ujue huyo ni pro-SLAA na MBOWE so anajaribu kumdhoofisha mheshimiwa jambo ambalo ni vigumu sana, ZITTO mtu wa watu bwana siyo hao hao wengine.
 
Nitatangaza hivi karibuni kwenda kukomboa jimbo moja wapo kutoka mkoa wa Tabora kupitia Chadema (2015).

Tabora haina wa kuitetea, Hongera Mh Zitto kwa kuwasaidia akina Rage na wenzake.
 
Ukimuona mtu anamponda ZITTO ujue huyo ni pro-SLAA na MBOWE so anajaribu kumdhoofisha mheshimiwa jambo ambalo ni vigumu sana, ZITTO mtu wa watu bwana siyo hao hao wengine.

Hizi ndio post unazozipenda sana Mbowe na Slaa wanakujaje hapa wewe pro JK muhongwa suti,mmh pro Kinana Jangiri wa ndovu mbona hivyo
 
KMkuu kama unavyojua Tabora kwa sasa hatuna wabunge nakumbuka bunge la tisa tulikuwa na selelii ila magamba walimfitini, Ila Zitto kwa sasa ni mlezi wa kanda ya magharibi actually ZZK is no just MP but rather a parliamentarian....., kuna vijana tunawapanga kukomboa mji..........pale mjini kwa sasa mbunge ni rage aka mzee wa bastola kiunoni,mirungi tuu kwa ujumla hamna kitu sikonge ndio bure...........yaani tunahitaji ukombozi kamili
 
Nitatangaza hivi karibuni kwenda kukomboa jimbo moja wapo kutoka mkoa wa Tabora kupitia Chadema (2015).

Tabora haina wa kuitetea, Hongera Mh Zitto kwa kuwasaidia akina Rage na wenzake.

Nadhani bila ushabiki, tunahitaji kuwa na mabadiliko ya sheria ya uchaguzi ili mtu awe mgombea lazima awe mkazi wa eneo husika katika kipindi cha muda flani hata miaka 3 kabla ya uchaguzi na tuweke sifa zinazomfanya mtu atambulike kuwa ni mkazi wa eneo hilo na utaache huu utaratibu wa eti kisa mtu alizaliwa Usongelani, Mabama, Malongwe, Ng,ambo, Usoke, n.k alafu akapotea miaka karibu 30 alafu anakuja kugombea ubunge. Ukiangalia wabunge walio wengi wa tz hutokea Dar kwenda Dom na wala sio kwenye majimbo yao
 
Back
Top Bottom