Hongera madaktari wetu tanzania kazi yenu na wito wa babu loliondo

DSN

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
2,837
1,674
Naomba kuwapa pongezi na pole madaktari wa Tanzania haswa [Specialist]

Tukianzia Dar es salaam, Muhimbili, Arusha, Kilimanjaro mpaka .....Daktari [Specialist wa wilaya kama wapo].Manake ukiangalia idadi ya wagonjwa waendao kwa Babu Loliondo. Jamani Madaktari wa Kitanzania wana Kazi na si utani wanastahiki Heshima aliyonayo Babu kwa sasa kwenye jamii.

Pata Picha ya wagonjwa hao walio kwa babu, na hao ni wale waliojikimu kufika huko,Je wale waliokua wakihudumiwa awali na wanaoendelea kuhudumiwa,du ni kazi nzito ukizingatia wabongo wanasema Udaktari ni wito[Tafsiri hiyo inayokaribina na Ukweli kwa mfano wa Babu] nao wanastahiki Heshima na kujaliwa na jamii nzima.

Kwa kiwango kikubwa idadi ya watanzania wengi tunamatatizo ya kiafya, ebu turushieni majina ya mabingwa wanao okoa maisha ya Watanzania kama babu anavyojaribu kuokoa maisha hayo.nasi wanajamii tuwape support japo kwa pongezi na kutambua uwezo wao kuanzia operation wanazofanya kuokoa maisha ya watanzania wanaopata ajari kila siku ya mungu,wanawake wanaojifungua labour,wagojwa wa kisukari,watoto,wagonjwa wa moyo,TB,nk.

Tuatajie daktari gani yuko Hospitali ya wilaya gani,Hospiatali mkoa gani mpaka Hospitali za rufaa.

Waambieni tunatambua chango wao,japo hatuna cha kuwapa ndio maana babu kwa kujua ni kazi ya wito akacharge shilingi mia tano tu kwa ambayo shilingia mia ndio mshahara wa babu,mia mbili zinaenda kwenye kanisa na shilingi mia mbili zingine zinaenda kwa wasaidizi wa babu.

Iko siku tutawapa maisha mazuri kwa kulinda afya zetu,
 
Huyo babu wa Loliondo - anastahili kupewa Phd ya heshima kwa utumishi uliotukuka katika kurekebisha afya za binadamu. Chuo gani kitawahi?
 
Back
Top Bottom