Hongera Lowassa, Hongera UKAWA

Hongera Lowassa, Hongera UKAWA

Hongera Lowassa, Hongera UKAWA. Pole sana CCM.
Nimesoma post nyingi sana za kukatisha tamaa kwenye jukwaa hili na kwingineko. Wengi wenu mnafikiri safari ya ukombozi ni sawa na kutembea kwa mguu toka Karimjee kwenda Ikulu. Wengine wananichekesha kuanza kudai ati ?sitapiga kura tena.? We mwehu au umetumwa!!! Sasa usipopiga kura ndio utakuwa unawakomoa usiowapenda? Wendawazimu wakubwa ni wale waoipongeza CCM kwa kushinda uchaguzi. Yaani, unaweza kumpongeza Magufuli kwa jambo moja tu, ?kufanikiwa kukanyaga Ikulu akiitwa rais. Huwezi kumpongeza kwa jambo lolote lingine. Mwenye kustahili pongezi katika uchaguzi huu ni Lowassa na UKAWA.

Wapo wana CCM wanaomcheka Lowassa kwa kuhama CCM na kugombea kupitia CHADEMA na mwisho kutangazwa amekuwa wa pili. Tume ya uchaguzi imempa Lowassa kura milioni sita. Wewe unayemkebehi Lowassa umewahi kushiriki uchaguzi wowote na kupata japo kura elfu mbili tu? Acha ujinga. Lowassa ameonesha kuwa anakubalika kuliko mtu mwingine yoyote Tanzania, na kauli yake inaogopewa sana, na ndio maana jeshi la polisi limeandikisha polisi wengi kuliko idadi. Wanaogopa. Neno moja tu la Lowassa linaweza kusababisha hata huyo mteule wa tume asiweze kuapishwa. Neno moja alilosema Lowassa, ?msifanye fujo na kuwapa sababu.? Ndio maana nasema hongera Lowassa.

UKAWA je, kwanini hongera? Kudadadeki! Hapo ndipo nasema HONGERA tena kwa herufi kubwa zaidi. Pamoja na waasisi kukimbia, UKAWA kamwe haijageuka kuwa ukiwa kama kiongozi mkuu wa CCM alivyosema katika moja ya mikutano. Kama unayesoma ujumbe huu ni mkazi wa Dar es salaam, basi kuna uwezekano kwa asilimia kubwa diwani wako ni UKAWA. Manispaa yako itaongozwa na UKAWA na hata Jiji la Dar es salaam huenda likabadilishwa jina na kuwa UKAWA CITY. Hakuna mwenye uwezo wa kuzuia jambo hilo. Pombe ataongoza toka Magogoni na kando yake tu, pale Karimjee; BENDERA za vyama vinavyounda UKAWA zitakuwa zinapepea, kando ya ile ya taifa au ya jiji. Hapo atakuwepo ?rais? wa Dar akimaliza kero za wananchi. Sasa unategemea wanaukawa waingiwe ukiwa kwa ushindi mkubwa kama huu? Nendeni Dodoma mkaipige hiyo minyimbo yenu ya TOT; kwani hapo Dar nani kaisoma namba? Na hata huko Dodoma, baadhi yao wamepisha siti ili UKAWA waweze kukaa; yaani kama vile mtoto wa shule anavyompisha siti mkubwa wake kwenye daladala. UKAWA anakaa na CCM anashika bomba, kisha atashuka tu kituo kinachofuata.

Ndugu zangu msiweke tena post za kusema pole au kukata tamaa. Wapeni pole hao waliopoteza dira. Unajua mabadiliko sio kuvuka kijito. Ni kuvuka mito, mabonde na bahari. Hapa safari ilipofika sio padogo na tafu ya Ngoyayi haikuwa haba. Wekeni sasa post za mikakati ya sasa na malengo ya kusonga mbele. Na hata kwenye uzi huu ningependa usiweke maneno mengi zaidi ya kusema HONGERA LOWASSA, HONGERA UKAWA.

Kwanza nikupe HONGERA wewe kwa kuto kukata tamaa! Unajua kwa nini, nimekufananisha na shujaa anaeshambuliwa kwa msimamo wake na sio kwa kosa. Pili, pia nipende kuwatia moyo waTZ wanaotaka kukata tamaa kuwa sasa kujiandaa kufanya kampeni za mikakati, kuanzia ngazi ya familia ya baba na mama, watoto n.k. Viongozi wa vyama vyetu wasijiingize katika mabishano yatakayoletwa na kina Nape, January, JMusukuma, Bulembo just to mention but a few.

Waweke pamba maskioni na kusonga mbele na zile operation zetu za mwanzo na kuziimarisha. Waliochaguliwa katika ngazi za udiwani, ubunge, na hata serikali za mitaa wakazane wawezavyo kupata wanachama wapya as many as possible, lakini huko huko wawafundishe namna ya kudumish uanachama. Kwa viongozi wa Taifa wa Vyama vyote vya Ukawa, tuendelee kudai katiba ya wananchi, tume huru ya uchaguzi. Hizo sehemu mbili za viongozi wa taifa zikifanikiwa, then tuna uhakika wa kushinda uchaguzi wowote. Hata huu tumeshinda lkn hakuna haki. Shangaa eti huwez kuhoji matokeo mahakamani, ukahoji wapi? Kenya au Uganda. Imagine ni sisi tu haturuhusiwi kuhoji matokeo ya urais mahakamani, what a shame ktk dunia ya sasa!

Umemsikia Raila akimpongeza Magufuli, huku akimshauri Lowassa aende mahakamani akifikiri kama walivyo na system nzuri ya kimahakama ni sawa na hii ya kwetu. Maskini hana habari kuwa sisi bado tupo Misri, Canaan bado kabisa. KICHEKESHO sidhani hata katika nchi duni kama Somalia kipo: Huwezi kuhoji matokeo mahakamani! Pigwa, umia utajiju. Kama huna ubavu wa kujibu mapigo kama Tarime, basi unaugulia maumivu taaratibu. La mwisho cheki ile sheria ya mita 200 ilivitafsiriwa na wanasheria wetu WASOMI kwa maslahi ya KIJANI! Wengine wakadiriki kusema kuwa ukishapiga kura sio kurudi nyumbani tu! Bali ukalale kabisa!!!! Unaona? Halafu na Malofa katika ubora wao, wanaishabikia hiyo sheria.

Najua na mimi sitasazwa katika hili, but nina hamu sana kuona jinsi watakavyodhibiti mfumko wa bei za bidhaa ili kumpa huyu LOFA unafuu wa maisha, coz najua Magufuli atarimotiwa na wenye chama kama wasemavyo, CCM ina wenyewe! Bei za bidhaa mbali mbali kupanda bila kuwa na mamlaka ya kudhibiti bei kwa maslahi ya huyu LOFA, au basi kuwabana waajiri wa kada zote kuongeza mishahara kuendana na hali halisi ya nchi.Hao wenyewe wanaendelea kuchuma kuhamishia utajiri nje ya TZ na mengine mengi. In fact, tumechagua misumari ya moto!

Natamani sana kuona watoto wa Magufuli and company waonekane wakisoma katika shule zetu za kawaida za msingi na kata. Hapo ntajua kweli ana uchungu na maisha ya mTanzania LOFA. Alieleza kwa hisia sana alipokuwa ktk kampeni zake, ngoja tuone. KILA LA HERI WANA MABADILIKO, KILA LA HERI UKAWA, HONGERA LOWASSA, TUNAKUPENDA TU, kama ulivyo!!!
 
Hongera Lowassa, Hongera UKAWA. Pole sana CCM.
Nimesoma post nyingi sana za kukatisha tamaa kwenye jukwaa hili na kwingineko. Wengi wenu mnafikiri safari ya ukombozi ni sawa na kutembea kwa mguu toka Karimjee kwenda Ikulu. Wengine wananichekesha kuanza kudai ati ?sitapiga kura tena.? We mwehu au umetumwa!!! Sasa usipopiga kura ndio utakuwa unawakomoa usiowapenda? Wendawazimu wakubwa ni wale waoipongeza CCM kwa kushinda uchaguzi. Yaani, unaweza kumpongeza Magufuli kwa jambo moja tu, ?kufanikiwa kukanyaga Ikulu akiitwa rais. Huwezi kumpongeza kwa jambo lolote lingine. Mwenye kustahili pongezi katika uchaguzi huu ni Lowassa na UKAWA.

Wapo wana CCM wanaomcheka Lowassa kwa kuhama CCM na kugombea kupitia CHADEMA na mwisho kutangazwa amekuwa wa pili. Tume ya uchaguzi imempa Lowassa kura milioni sita. Wewe unayemkebehi Lowassa umewahi kushiriki uchaguzi wowote na kupata japo kura elfu mbili tu? Acha ujinga. Lowassa ameonesha kuwa anakubalika kuliko mtu mwingine yoyote Tanzania, na kauli yake inaogopewa sana, na ndio maana jeshi la polisi limeandikisha polisi wengi kuliko idadi. Wanaogopa. Neno moja tu la Lowassa linaweza kusababisha hata huyo mteule wa tume asiweze kuapishwa. Neno moja alilosema Lowassa, ?msifanye fujo na kuwapa sababu.? Ndio maana nasema hongera Lowassa.

UKAWA je, kwanini hongera? Kudadadeki! Hapo ndipo nasema HONGERA tena kwa herufi kubwa zaidi. Pamoja na waasisi kukimbia, UKAWA kamwe haijageuka kuwa ukiwa kama kiongozi mkuu wa CCM alivyosema katika moja ya mikutano. Kama unayesoma ujumbe huu ni mkazi wa Dar es salaam, basi kuna uwezekano kwa asilimia kubwa diwani wako ni UKAWA. Manispaa yako itaongozwa na UKAWA na hata Jiji la Dar es salaam huenda likabadilishwa jina na kuwa UKAWA CITY. Hakuna mwenye uwezo wa kuzuia jambo hilo. Pombe ataongoza toka Magogoni na kando yake tu, pale Karimjee; BENDERA za vyama vinavyounda UKAWA zitakuwa zinapepea, kando ya ile ya taifa au ya jiji. Hapo atakuwepo ?rais? wa Dar akimaliza kero za wananchi. Sasa unategemea wanaukawa waingiwe ukiwa kwa ushindi mkubwa kama huu? Nendeni Dodoma mkaipige hiyo minyimbo yenu ya TOT; kwani hapo Dar nani kaisoma namba? Na hata huko Dodoma, baadhi yao wamepisha siti ili UKAWA waweze kukaa; yaani kama vile mtoto wa shule anavyompisha siti mkubwa wake kwenye daladala. UKAWA anakaa na CCM anashika bomba, kisha atashuka tu kituo kinachofuata.

Ndugu zangu msiweke tena post za kusema pole au kukata tamaa. Wapeni pole hao waliopoteza dira. Unajua mabadiliko sio kuvuka kijito. Ni kuvuka mito, mabonde na bahari. Hapa safari ilipofika sio padogo na tafu ya Ngoyayi haikuwa haba. Wekeni sasa post za mikakati ya sasa na malengo ya kusonga mbele. Na hata kwenye uzi huu ningependa usiweke maneno mengi zaidi ya kusema HONGERA LOWASSA, HONGERA UKAWA.

Hongera UKAWA na EDWARD LOWASSA..
Tuanze na mchakato wa Sheria ya kuibadilisha Tume ya Uchaguzi na staffs wake.
Khs nani atawafanyia usaili hao Makamishna pamoja na watakao kuwa ktk kila wilaya.
Ili tuweze kutangaziwa Matokeo halisi.

Mwaka huu wananchi wamepiga kura, Mawakala wamehesabu vzr na matokeo kubandikwa kila kituo pasipo lalamiko, shida kubwa ni khs utangazaji wa hayo matokeo ktk offices husika.
Mpk Police forces wawepo...!!!
Haikuingilia akilini.
 
Hongera Lowassa, Hongera UKAWA. Pole sana CCM.
Nimesoma post nyingi sana za kukatisha tamaa kwenye jukwaa hili na kwingineko. Wengi wenu mnafikiri safari ya ukombozi ni sawa na kutembea kwa mguu toka Karimjee kwenda Ikulu. Wengine wananichekesha kuanza kudai ati ?sitapiga kura tena.? We mwehu au umetumwa!!! Sasa usipopiga kura ndio utakuwa unawakomoa usiowapenda? Wendawazimu wakubwa ni wale waoipongeza CCM kwa kushinda uchaguzi. Yaani, unaweza kumpongeza Magufuli kwa jambo moja tu, ?kufanikiwa kukanyaga Ikulu akiitwa rais. Huwezi kumpongeza kwa jambo lolote lingine. Mwenye kustahili pongezi katika uchaguzi huu ni Lowassa na UKAWA.

Wapo wana CCM wanaomcheka Lowassa kwa kuhama CCM na kugombea kupitia CHADEMA na mwisho kutangazwa amekuwa wa pili. Tume ya uchaguzi imempa Lowassa kura milioni sita. Wewe unayemkebehi Lowassa umewahi kushiriki uchaguzi wowote na kupata japo kura elfu mbili tu? Acha ujinga. Lowassa ameonesha kuwa anakubalika kuliko mtu mwingine yoyote Tanzania, na kauli yake inaogopewa sana, na ndio maana jeshi la polisi limeandikisha polisi wengi kuliko idadi. Wanaogopa. Neno moja tu la Lowassa linaweza kusababisha hata huyo mteule wa tume asiweze kuapishwa. Neno moja alilosema Lowassa, ?msifanye fujo na kuwapa sababu.? Ndio maana nasema hongera Lowassa.

UKAWA je, kwanini hongera? Kudadadeki! Hapo ndipo nasema HONGERA tena kwa herufi kubwa zaidi.
Pamoja na waasisi kukimbia,
UKAWA kamwe haijageuka kuwa ukiwa kama kiongozi mkuu wa CCM alivyosema katika moja ya mikutano. Kama unayesoma ujumbe huu ni mkazi wa Dar es salaam, basi kuna uwezekano kwa asilimia kubwa diwani wako ni UKAWA. Manispaa yako itaongozwa na UKAWA na hata Jiji la Dar es salaam huenda likabadilishwa jina na kuwa UKAWA CITY. Hakuna mwenye uwezo wa kuzuia jambo hilo. Pombe ataongoza toka Magogoni na kando yake tu, pale Karimjee; BENDERA za vyama vinavyounda UKAWA zitakuwa zinapepea, kando ya ile ya taifa au ya jiji. Hapo atakuwepo ?rais? wa Dar akimaliza kero za wananchi. Sasa unategemea wanaukawa waingiwe ukiwa kwa ushindi mkubwa kama huu? Nendeni Dodoma mkaipige hiyo minyimbo yenu ya TOT; kwani hapo Dar nani kaisoma namba? Na hata huko Dodoma, baadhi yao wamepisha siti ili UKAWA waweze kukaa; yaani kama vile mtoto wa shule anavyompisha siti mkubwa wake kwenye daladala. UKAWA anakaa na CCM anashika bomba, kisha atashuka tu kituo kinachofuata.

Ndugu zangu msiweke tena post za kusema pole au kukata tamaa. Wapeni pole hao waliopoteza dira. Unajua mabadiliko sio kuvuka kijito. Ni kuvuka mito, mabonde na bahari. Hapa safari ilipofika sio padogo na tafu ya Ngoyayi haikuwa haba. Wekeni sasa post za mikakati ya sasa na malengo ya kusonga mbele. Na hata kwenye uzi huu ningependa usiweke maneno mengi zaidi ya kusema HONGERA LOWASSA, HONGERA UKAWA.


Nakubalina na wewe kwa 99% ila padogo ninapotaofautiana na wewe hiyo 1% ni pale unapodai kuwa "waasisi wamelikimbia". Hakuna muasisi hata mmoja aliyekimbia wote unaowataja walikuja tena nyakati za chagzi kama hizi. Sibezi michango yao ila huo ndio ukweli wenyewe.

Ni kweli kwamba ENL ametoa mchangoa mkubwa hususan katika kuwatoa watanzania wwengi woga walionao kuwa hakuna maisha ukitoka CCM. Ametoka CCM na maisha yameendelea.Kingine ambacho Lowassa, Sumyae na Kingune wamewafunza watanzania kwa ujumla wao ni kuwa wakati wowote ukiwa madarakani fikiri , tende na fanya maamuzi kwa maslahi ya taifa na sio chama. Kwa sababu wakati wote walipokuwa madarakani walikuwa wakifanya maamuzi kwa maslahi ya chama fulani ndio maana safari yao ya mabadiliko haikuweza kufanikiwa kwa 100%.

Ni imani yangu kutokea sasa waliobaki huko madarakani watajihoji mara mabili kila mara watakapokuwa walitaka kusigina haki za wananchi kwa faida ya chama chao. Mzee wetu wa Katiba mpya, akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali miaka ya 1970s ndio alikuwa kinara wa kupitisha hizi katiba mbovu zinzobana haki za wananchi tena kwa hati za dharura ili kuwanyiwa fursa wawakilishi wa wanachi kuchangia maoni ya wananchi. Hivi sasa kadri anavyojaribu kurekebisha mapungufu hayo anashindwa hadi kufikia kuchezea makofi toka kwa watoto wadogo.
 
No one can change my mind lowasa ni rais wangu kamwe sitotamka pombe ni rais wangu linafiki sana
 
Crucifix, umenena! Naamini kilichofanywa na ZEC Zanzibar ndicho hicho kilichofanywa na NEC, japo wao wametumia njia nyingine. Lakini hata kama tukikubali matokeo kadri yalivyotolewa na NEC, bado kura milioni 6 si haba. Hakuna mgombea yeyote katika historia ya ucnaguzi wa vyma vingi aliyeweza kupata kura nyingi kama alizopata Lowassa. Ameleta msisimko mkubwa na viti vya ubunge na udiwani vimeongezeka ambavyo haijawahi kutokea. HONGERA LOWASSA, HONGERA UKAWA.
 
Sasa tudai katiba mpya kwanza.. Kushindana na chama dola kwa katiba hii ni vichomi tu, tena katiba ya wananchi kupitia warioba na sio ile ya chenge na sita
 
Hongera UKAWA, Hongera Lowasa, Hongereni viongozi wote wa UKAWA. Msikate tamaa endeleeni kuwatetea watanzania. Viongozi wa UKAWA ndio Marais wetu, shida zetu tutawaeleza nyinyi, mtatutetea. Waliohama ccm msikate tamaa, mmeonyesha njia kwamba tanzania si ccm tu hata chadema inawezekana. Endeleeni kuwatetea wananchi ipo siku itaeleweka tu.
 
Hongereni wote mliowapigia kura wapinzani kwani mmeonyesha kutokukubalia na dhuluma za CCM
 
Hongera Lowassa, Hongera UKAWA. Pole sana CCM.
Nimesoma post nyingi sana za kukatisha tamaa kwenye jukwaa hili na kwingineko. Wengi wenu mnafikiri safari ya ukombozi ni sawa na kutembea kwa mguu toka Karimjee kwenda Ikulu. Wengine wananichekesha kuanza kudai ati ?sitapiga kura tena.? We mwehu au umetumwa!!! Sasa usipopiga kura ndio utakuwa unawakomoa usiowapenda? Wendawazimu wakubwa ni wale waoipongeza CCM kwa kushinda uchaguzi. Yaani, unaweza kumpongeza Magufuli kwa jambo moja tu, ?kufanikiwa kukanyaga Ikulu akiitwa rais. Huwezi kumpongeza kwa jambo lolote lingine. Mwenye kustahili pongezi katika uchaguzi huu ni Lowassa na UKAWA.

Wapo wana CCM wanaomcheka Lowassa kwa kuhama CCM na kugombea kupitia CHADEMA na mwisho kutangazwa amekuwa wa pili. Tume ya uchaguzi imempa Lowassa kura milioni sita. Wewe unayemkebehi Lowassa umewahi kushiriki uchaguzi wowote na kupata japo kura elfu mbili tu? Acha ujinga. Lowassa ameonesha kuwa anakubalika kuliko mtu mwingine yoyote Tanzania, na kauli yake inaogopewa sana, na ndio maana jeshi la polisi limeandikisha polisi wengi kuliko idadi. Wanaogopa. Neno moja tu la Lowassa linaweza kusababisha hata huyo mteule wa tume asiweze kuapishwa. Neno moja alilosema Lowassa, ?msifanye fujo na kuwapa sababu.? Ndio maana nasema hongera Lowassa.

UKAWA je, kwanini hongera? Kudadadeki! Hapo ndipo nasema HONGERA tena kwa herufi kubwa zaidi. Pamoja na waasisi kukimbia, UKAWA kamwe haijageuka kuwa ukiwa kama kiongozi mkuu wa CCM alivyosema katika moja ya mikutano. Kama unayesoma ujumbe huu ni mkazi wa Dar es salaam, basi kuna uwezekano kwa asilimia kubwa diwani wako ni UKAWA. Manispaa yako itaongozwa na UKAWA na hata Jiji la Dar es salaam huenda likabadilishwa jina na kuwa UKAWA CITY. Hakuna mwenye uwezo wa kuzuia jambo hilo. Pombe ataongoza toka Magogoni na kando yake tu, pale Karimjee; BENDERA za vyama vinavyounda UKAWA zitakuwa zinapepea, kando ya ile ya taifa au ya jiji. Hapo atakuwepo ?rais? wa Dar akimaliza kero za wananchi. Sasa unategemea wanaukawa waingiwe ukiwa kwa ushindi mkubwa kama huu? Nendeni Dodoma mkaipige hiyo minyimbo yenu ya TOT; kwani hapo Dar nani kaisoma namba? Na hata huko Dodoma, baadhi yao wamepisha siti ili UKAWA waweze kukaa; yaani kama vile mtoto wa shule anavyompisha siti mkubwa wake kwenye daladala. UKAWA anakaa na CCM anashika bomba, kisha atashuka tu kituo kinachofuata.

Ndugu zangu msiweke tena post za kusema pole au kukata tamaa. Wapeni pole hao waliopoteza dira. Unajua mabadiliko sio kuvuka kijito. Ni kuvuka mito, mabonde na bahari. Hapa safari ilipofika sio padogo na tafu ya Ngoyayi haikuwa haba. Wekeni sasa post za mikakati ya sasa na malengo ya kusonga mbele. Na hata kwenye uzi huu ningependa usiweke maneno mengi zaidi ya kusema HONGERA LOWASSA, HONGERA UKAWA.

Hongera ametikisa mpk wastaafu wasanii vyombo vya habari kutumika bado ushindi ukawa wa kawaida
 
Tuendeleze moto wa mabadiliko maeneo mengine tuna kila sababu ya kujipongeza tumeongeza idadi ya wabunge na ruzuku kutokana na kura za Rais.
 
Mkapa, kikwete na makamba ni mahaini wamepindua nchi kwa kujitangazia utawala wa mabavu. Wanastahili kuondolewa kwa namna yoyote.

Inatakiwa waoneshwe na nguvu ya umma kuwa ni wahaini na vibaka wa demokrasia na muhali wa taifa letu MAMA TANGANYIKA
 
Demokrasia ni hatu moja kwenda hatua nyingine ya pili....baada ya kikwete kushinda kwa kishindo mwaka 2005 (>80%0, mwaka 2010 kura zikashuka mpaka 62%, mwaka huu zimekomea 58.47% hii ni baada ya kufanya kila aina ya mbinu, gharama ya kura za JPM naamini ni kubwa mno .

Jingine kwa hizo kura za EL kitaipunguzia ccm ruzuku kwa sehemu kubwa mno maana ruzuku inatokana na idadi za kura za mgombea wa Rais. Na kwa kuwa ccm kina viongozi wengi na ruzuku ni ndogo basi lazima watatafuta mahali pa kuweza kuziba hili pengo...hivyo lazima ufisadi mwingine utengenezwe kama pesa za stanbic zilivyotumiwa kwenye kampeni za mwaka huu. Kila kata nchini ilipatiwa sh 6,470,000.

CCM walikuwa wamejipanga kuhakikisha wafuatao hawarudi Bungeni Tundu Lissu, Mbowe, Msigwa na Kafulila. Hivyo hawa kila hayo majimbo yalitengewa fungu maalum sh milioni 100 kwa kila jimbo katika kufanikisha hilo. Kafulila ndo amezurumiwa katika hao
 
Demokrasia ni hatu moja kwenda hatua nyingine ya pili....baada ya kikwete kushinda kwa kishindo mwaka 2005 (>80%0, mwaka 2010 kura zikashuka mpaka 62%, mwaka huu zimekomea 58.47% hii ni baada ya kufanya kila aina ya mbinu, gharama ya kura za JPM naamini ni kubwa mno .

Jingine kwa hizo kura za EL kitaipunguzia ccm ruzuku kwa sehemu kubwa mno maana ruzuku inatokana na idadi za kura za mgombea wa Rais. Na kwa kuwa ccm kina viongozi wengi na ruzuku ni ndogo basi lazima watatafuta mahali pa kuweza kuziba hili pengo...hivyo lazima ufisadi mwingine utengenezwe kama pesa za stanbic zilivyotumiwa kwenye kampeni za mwaka huu. Kila kata nchini ilipatiwa sh 6,470,000.

CCM walikuwa wamejipanga kuhakikisha wafuatao hawarudi Bungeni Tundu Lissu, Mbowe, Msigwa na Kafulila. Hivyo hawa kila hayo majimbo yalitengewa fungu maalum sh milioni 100 kwa kila jimbo katika kufanikisha hilo. Kafulila ndo amezurumiwa katika hao


Kafulila na wabunge wengine waliodhurumiwa wakienda mahakamani watashinda tu. Kikubwa wahakikishe wanatunza vielelezo na ikibidi waviweke nje ya nchi kwa sababu ccm ni mafia. Angali jana kuvamia kituo cha sheria na haki za binadamu kwamba hawatakiwi kufahamu ukweli wa kinachoendelea.

Hata hivyo hawatawali safari hii kwa sababu magufuli hana supporters ila ana haters wasiopungua 62% ya watanzania. Ccm itakuwa na kipindi kugumu kuliko vyote alvyowahi kuwa navyo.
 
Mh Raisi wangu Lowasa Alisema... Tusifanye Fujo Na Tuendelee Kuwa Na Amani Kwa Maana Hata Acha Haki Ya Wanaukawa Na watz Kwa Ujumla Ipotee

Naamin Wanaukawa Wote Tunayaishi Haya Maneno
 
Back
Top Bottom