PostGE2025 Hongera kwa JWTZ kwa kutuliza nchi. Lakini Nina ushauri huu

PostGE2025 Hongera kwa JWTZ kwa kutuliza nchi. Lakini Nina ushauri huu

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Kizibo

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2018
Posts
4,535
Reaction score
10,240
Moja kwa moja kwenye mada.

Najua viongozi wa jwtz wako humu.
Jwtz wenyewe (askari wenyewe) wako humu.

Nawapongeza sana kwa kutuliza hali ya nchi. Ni wazi, bila jwtz kuwa deployed mitaani kwa wingi, polisi peke yao wasingeweza kutuliza hali ikawa vile ilivyokuwa jana D9.

Pamoja na hayo...

Hivyo hivyo mlivyotuliza hali mitaani, nashauri pia yafuatayo.

1 Washaurini viongozi wa nchi hasa raisi kutenda haki. Atumie mamlaka na sio vitisho. Yeye ndiyo sababu ya kufika huku. Viongozi ndio wanaotishia amani ya nchi na sio raia. Sisi Gen Z ni reactors, ila viongozi hasa Raisi ndo actor. Aina ya utawala wake unatia hasira sana. Mshaurini ajirekebishe, kuanzia kauli zake, matendo yake. Wanahubiri amani bila kutenda haki, huo ni utahira. Mshauri raisi na wateule wake watende haki na amani itashamiri

2 Dhibitini na mkomeshe mtandao wa utekaji. Hilo swala linaichafua jeshi na kuonekana haliwalindi raia. Kama ni utekaji, basi uwe kwa watu ambao KABISA ni kwa wale watu wanaoonekana tishio kwa usalama wa nchi na sio kwa wafichua maovu na wasema kweli.

Nyie jwtz ndo mna dhamana ya usalama wa hii nchi, nyie ndo fainal say. Msitumike na kuwekwa chini ya wanasiasa bana. Hata kama raisi akitoa oda ya kijinga semeni hapana. Ni imani yangu kuwa sasa mmejifunza kuwa Tanzania kuingia kwenye machafuko kwa sababu ya upumbavu wa wanasiasa inawezekana.

Wasioitakia mema nchi sio raia, sio Gen Z wala sio wageni, NI hao wanasiasa wajinga wajinga walafi, WADHIBITINI HAO MUONE KUWA KUTAKUWA NA CHOKO CHOKO YOYOTE NCHINI. Lakini msipowadhibiti, haijalishi mtaweka ulinzi kiasi gani, haijallishi mtaua wangapi lakini ipo siku nchi itawaka moto na Tanzania itatengeneza wakimbizi.

Nimepata hasira ngoja niishie hapa. AAH MAMBO MENGINE NI YA KIPUMBAVU
 
Moja kwa moja kwenye mada.

Najua viongozi wa jwtz wako humu.
Jwtz wenyewe (askari wenyewe) wako humu.

Nawapongeza sana kwa kutuliza hali ya nchi. Ni wazi, bila jwtz kuwa deployed mitaani kwa wingi, polisi peke yao wasingeweza kutuliza hali ikawa vile ilivyokuwa jana D9.

Pamoja na hayo...

Hivyo hivyo mlivyotuliza hali mitaani, nashauri pia yafuatayo.

1 Washaurini viongozi wa nchi hasa raisi kutenda haki. Atumie mamlaka na sio vitisho. Yeye ndiyo sababu ya kufika huku. Viongozi ndio wanaotishia amani ya nchi na sio raia. Sisi Gen Z ni reactors, ila viongozi hasa Raisi ndo actor. Aina ya utawala wake unatia hasira sana. Mshaurini ajirekebishe, kuanzia kauli zake, matendo yake. Wanahubiri amani bila kutenda haki, huo ni utahira. Mshauri raisi na wateule wake watende haki na amani itashamiri

2 Dhibitini na mkomeshe mtandao wa utekaji. Hilo swala linaichafua jeshi na kuonekana haliwalindi raia. Kama ni utekaji, basi uwe kwa watu ambao KABISA ni kwa wale watu wanaoonekana tishio kwa usalama wa nchi na sio kwa wafichua maovu na wasema kweli.

Nyie jwtz ndo mna dhamana ya usalama wa hii nchi, nyie ndo fainal say. Msitumike na kuwekwa chini ya wanasiasa bana. Hata kama raisi akitoa oda ya kijinga semeni hapana. Ni imani yangu kuwa sasa mmejifunza kuwa Tanzania kuingia kwenye machafuko kwa sababu ya upumbavu wa wanasiasa inawezekana.

Wasioitakia mema nchi sio raia, sio Gen Z wala sio wageni, NI hao wanasiasa wajinga wajinga walafi, WADHIBITINI HAO MUONE KUWA KUTAKUWA NA CHOKO CHOKO YOYOTE NCHINI. Lakini msipowadhibiti, haijalishi mtaweka ulinzi kiasi gani, haijallishi mtaua wangapi lakini ipo siku nchi itawaka moto na Tanzania itatengeneza wakimbizi.

Nimepata hasira ngoja niishie hapa. AAH MAMBO MENGINE NI YA KIPUMBAVU
Hao Red cross wapo kwa ajili ya kumlinda Samia tu na sio wananchi,,,rejea yaliyotokea siku 5 baada ya uchaguzi
 
Utekaji wowote haufai iwe kwa anayehatarisha usalama au kitu gani haufai.ipo jesh full arm wanamshnda hadi wamteke.ipo mahakama kwnn asishtkiwe.HATUTAKI UTEKAJI.UTEKAJI=UHARAMIA WA KIDOLA ILIOSHNDWA.
 
Utekaji wowote haufai iwe kwa anayehatarisha usalama au kitu gani haufai.ipo jesh full arm wanamshnda hadi wamteke.ipo mahakama kwnn asishtkiwe.HATUTAKI UTEKAJI.UTEKAJI=UHARAMIA WA KIDOLA ILIOSHNDWA.

Nakubaliana na wewe mkuu. Polisi kazi yake iwe kukamata watuhumiwa, kisha mahakama kwa uhuru wake iamue
 
Unatoa ushauri kwa jeshi la wapumbavu(JWTZ) ukiamini eti watakuskiliza kama raia mwema?

Hao wajinga sio kuwa wanatii na kutekeleza amri ya huyu raisi haramu pekee tu, bali wanatii na kufuata mpaka amri za mapolisi kama Mfwele na Murilo.

Hao wanaamini watu muhimu wa kulinda nchi hii ni viongozi wa serikali tu basi, wanainchi hawana umuhimu wowote kwao na ndio maana hata kipindi wanakufa walikuwa wanawaangalia tu.
 
Mkuu umelewa? 🍺

Yani unakaa unapoteza muda wako kuwapongeza hao vibaraka?

1. Ipo hivi, mkuu wa JWtz anateuliwa na raisi na anaweza kufukuzwa dakika moja. Huyu hawezi kunyanyua mdomo kusema kitu.

2. Jwtz wanapitia mafunzo makali ya propaganda kuwaaminisha wao wapo karibu zaidi na serikali si wananchi.

3. Vijana wa wajeshi yetu huwa wanatishiwa wataachishwa kazi na maisha yao yatakuwa magumu zaidi. Refer video ya Mwafwele na nyingine nyingi.

4. Kuanzia sasa Tz itazidi kutawalia kiditketa na watu wengi zaidi watapotezwa.

5. Njia pekee yakuepuka hili ni KUPIGANA bila kuchoka.

6. They can win a battle but not a war, hawa lazima watatema bungo in a long run.

7. Tunafahamu serikali na vibaraka wao ni choka mbaya financially.
 
Siku chache zijazo, hili jeshi kitadharaurika mno kama ilivyo kwa police.
 
Ma wale wananchi wanaosema hawana rais kwa sababu hakukuwa na uchaguzi nani wa kusikiliza madai yao?
 
Nyie siyo watu wa kwenda nao kiungwana nyie ni watu wa kwenda nao kimenomeno, Samia alichokosea ni pale alipoingia madarakani na kujifanya anataka kuwa mwema kwa nyumbu akawaruhusu hadi mfanye maandamano na mikutano ya hadhara ambayo ilikua imezuiwa na Magufuli.

Matokeo yake hizo haki zilizoruhusiwa zimetumiwa kama petrol ya kuwashia moto wa chuki na kauli za kinyumbu kama za Tundu Lisu pale aliposema "Tutafanya uasi, nchi haitakalika, tutavufuga uchaguzi mkuu".

Nyie dawa yenu ni kwenda kimenomeno ukiwa mstaarabu utafanyiwa ustaarabu mkileta unyumbu wa kujaribu mapinduzi, kuchoma nchi na kuharibu mali za watu na za Umma dawa ni kuwachapa risasi hadi akili iwakae sawa.
 
Back
Top Bottom