asakuta same
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 14,829
- 5,039
Mkuu wanasiasa wote ni watu wa kuchukuliwa kwa tahadhari na kama ingewezekana wawe wanaongea chini ya viapo!!!!!!!!
...nami nimeshangaa leo kaibuka na maneno mazuri sijui kazaliwa upya!!! nimependa zaidi pale aliposema kwamba ili tupate Katiba inayostahili kitu MARIDHIANO haikiepukiki, na ili tufikie hayo maridhiano wajumbe hawana budi kuacha misimamo yao pembeni na wote kuwa na kauli moja yenye nia ya kujenga. Hivyo kusikilizana, kukubali kukosolewa ndani ya Bunge ndiyo njia pekee itakayotufikisha pale watanzania wanapopataka.
Bado naamini kuwa ili kupata Katiba bora itakayoweza kutuunganisha ni lazima iwe ya maridhiano, si kwa wingi au uchache wa waungaji mkono. Bado pia naamini kuwa si mfumo wa Serikali mbili au tatu utakaotatua kinachoitwa kero za muungano na hasa kama tutauchukua bila maridhiano ya pande zote. Bahati mbaya sana maridhiano haya yanaongozwa na wanasiasa, kwani matakwa ya kisiasa (political will) ndiyo kuu katika suala hili.Serekali 3 zinawatesa sana wabunge wengine wanasema hayo ni mawazo ya Waryoba wengine pamoja na Waryoba wanasema kuwa hayo ni maoni ya wananchi.Ndani ya bunge hilohilo wapo wabunge waliolishana yamini kuwa wahakikishe rasimu ya katiba haipenyi ikiwa na maoni ya serekali 3.Wapo wanaopambana kuhakikisha rasimu ya katiba inapenya bungeni ikiwa na maoni ya serekali3 kwa vile wanaamini kuwa hayo ndiyo maoni ya wananchi.Katika hili wabunge walikuwa hawana sababu ya kurushiana maneno machafu kuimbiana tarabu kuongea maneno ya mipashomipasho kama watoto kitu ambacho kimewafanya wabunge wawe kituko mbele ya jamii.Kitu walichopaswa kukifanya kwa vile kuna wanaoamini kuwa serekali 3 ni mawazo ya Waryoba,Waryoba na baadhi ya wabunge wanasema kuwa hayo maoni ya serekali 3 yametoka kwa wananchi kwa vile rasimu inatakiwa irudi kwa wananchi ikapigiwe kura kuliko kuendelea kurumbana wanatakiwa waiache rasimu ya katiba ikiwa na maoni ya serekali3 ili mwananchi ambaye inaonekana kupakaziwa maoni ambayo hakuyatoa akayakatae hayo maoni kwa njia ya kura.
...ni kweli katika hili swala la unafiki kutawala linaweza kupewa nafasi; lakini tukumbuke kwamba katika kundi la wapenda serikali 2 walioko humo si kwamba wote wameridhia au wanaunga mkono kwa matakwa yao; wako hivyo kwasababu ya mfumo tu, usije kushangaa na wengine wakajitokeza na kuanza kutoa kauli za style ya Job Ndugai, kwa mtu mwenye kufikiria Haki kuliko Dhuruma lazima aungane na wapenda Haki wenzake.Mie namuona ni mnafiki tu anatafuta gia ya kuwarudisha UKAWA bungeni. Nasema hivyo kwa sababu misimamo mikali anayoisema kuwa wajumbe wa CCM wanayo wameipata katika vikao vyao ambavyo nae Ndugai ni mjumbe, kwa nini hajawashauri huko huko? Pili mbona sijamsikia akiongea humo bungeni kuwashauri wenzie kulegeza misimamo yao?
Nina hakia tume ingetoa mapendekezo yanayolingana na chama tawala, sasa hivi wangekuwa wanalaumiwa na kudharauliwa na wapinzani...Tume ilifanya kazi yake vizuri , kwa weledi na juhudi kubwa. Tatizo ni ukigeugeu na unafiki wa viongozi wetu kuendekeza maslahi binafsi na ya vikundi vyao ndiyo walioharibu mchakato kwa ujumla.
hao tbc hawana maana yoyote kwa mustakabali wa nchi yetu.
Bado naamini kuwa ili kupata Katiba bora itakayoweza kutuunganisha ni lazima iwe ya maridhiano, si kwa wingi au uchache wa waungaji mkono. Bado pia naamini kuwa si mfumo wa Serikali mbili au tatu utakaotatua kinachoitwa kero za muungano na hasa kama tutauchukua bila maridhiano ya pande zote. Bahati mbaya sana maridhiano haya yanaongozwa na wanasiasa, kwani matakwa ya kisiasa (political will) ndiyo kuu katika suala hili.
Kuyapata maridhiano ni la kutokane na kuaminiana kwa Wajumbe na mchakato ulio sahihi unaokubalika na pande zote. Nikiangalia jinsi mambo yanavyokwenda, hivi vyote havipo. Sijaona Wajumbe wakijadili hoja bali misimamo. Mchakato wenyewe unaonekana kupingwa na pande zote ikiwemo hasa ule wa msingi wa tunda wanalojadili huko Dodoma! Kama hawaamini mchakato wa tume ya Katiba (na Wajumbe wake kwa pamoja na binafsi) na tunda lake sijui watafikiaje maridhiano na hasa sijui wanachokifanya Dodoma. Tunaona mashindano ya kupata mshindi na mshindwa ndani na nje ya bunge. Hii ni bahati mbaya kweli kweli!
Misimamo ya makundi na hasa ya kivyama imevuruga sana mchakato huu. Imefanya Wajumbe na watu nje ya bunge kuhairisha kufikiri na kusimamia misimamo hii. Imani zimekuwa kwenye misimamo hii. Mjumbe anasimama na kuanza kwa kutamka yeye ni 'muumini wa dini' gani - mbili au tatu! Ukisikiliza hoja anazotoa unabaki kinywa wazi kama anaelewa maana ya mfumo anaouchagua.
Sijasikia mjumbe ambaye ameongelea kwa kina ni masuala gani ya muungano, ama ndani ya Serikali tatu au mbili yatauimarisha muungano wetu. Muungano umefikisha miaka 50 badala ya kuuimarisha kwa kuongoza mambo tunayoshughulikia na kusimamia kwa pamoja eti tunayapunguza na kujitapa kuwa tunaimarisha muungano!
Mungu atubariki, tupite salama.
Sitta ameingia kikichwa kichwa kwenye mtego aliowekewa kummaliza kisiasa.
Mpango wake wa urais umeyeyuka kama nailoni kwenye moto.
...nami nimeshangaa leo kaibuka na maneno mazuri sijui kazaliwa upya!!! nimependa zaidi pale aliposema kwamba ili tupate Katiba inayostahili kitu MARIDHIANO haikiepukiki, na ili tufikie hayo maridhiano wajumbe hawana budi kuacha misimamo yao pembeni na wote kuwa na kauli moja yenye nia ya kujenga. Hivyo kusikilizana, kukubali kukosolewa ndani ya Bunge ndiyo njia pekee itakayotufikisha pale watanzania wanapopataka.
Yaani mkuu hapa duniani usipokuwa makini na ukashindwa kutumia akili vizuri utaumbuka mchana na historia itakukana.
Sitta alijenga heshima kupitia Uspika wa Bunge , na sasa Uenyekiti wa Bunge umemmaliza.Hana cha kujivunia tena.