Hongera Dr. Diodorus Kamala

Hongera Dr. Diodorus Kamala

Egwugu

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2011
Posts
17,558
Reaction score
8,551
Wasalaam Watanzania nyote.
Leo nina jambo moja la kumhusu huyu Mh.Mbunge wa jimbo la Misenyi Nampongeza sana huyu mzee.

Kwanza niseme wazi, (mie sina chama) ila ninao utashi tu wa kumuangalia mtu mmoja mmoja kwa kadili ya matendo yake na hasa katika nafasi yake. Binafsi naamini kabisa approach yangu hii inanisaidia sana, nakuwa huru mda wote kupongeza na kusifia yeyote yule ama kukosoa na kamwe sibanwi na mipaka ya vyama "vyao".

Tokea uchaguzi umalizike na huyu mzee kuibuka kidedea, kuusema ukweli pasipo kuuma maneno na wala kumuonea mwingine, huyu mh. kweli ni kati ya wabunge wachache sana kutoka CCM na hata upinzani wanaoifanya kazi yao. Na hata staili yake anayoitumia ya kelele kidogo na matendo mengi a.k.a mzee wa kimya kimya iko safi sana.
Hadi kufikia leo, ni mbunge pekee kutoka mkoa wa Kagera aliyeweza kulizunguka jimbo lake kwa zaidi ya mara tatu.

Nimesoma na kuzidi kumfatilia baada ya kuvutiwa sana na anavyokuwa karibu na wanajimbo wake, huyu mzee anastahili pongezi hata kama hana anachowapa. Ninajiuliza kwa wapinzani, achana na mizigo ya CCM ambayo tumeshaizoea, ni kwanini wa upinzani walio wengi hawana spirit ya kutumikia vyeo vyao zaidi ya kuonekana wako busy na kuratibu maandamano kana kwamba waligraduate katika kuandaa maandamano

Kwa wapinzani na Lwakatare akiwemo, wanatakiwa kuelewa mahitaji ya jamii za watu wao na mahitaji yao, bora liende na mob politics havitawasaidia kamwe. Nendeni majimboni mkafanye kama Nassari a.k.a dogo janja, nendeni mkafanye kama Prof. Muhongo, fanyeni kama Dr. Diodorous Kamara. Mkitaka kuendelea kuwa wauza sura mijini mtambue 2020 siyo mbali na watanzania hawatasita kuchukua maamuzi "sahihi".

Atakaye mwona Mh. Mbunge huyu naomba ampe salaam zangu nyingi.
 
Acha kupotosha, Kamala na Kyerwa wapi na wapi? Huyu ni mbunge wa Nkenge. Hiyo kutembelea wapiga kura wake ni kwasababu ya tetemeko la ardhi vinginevyo hana tofauti na wabunge wengine walio wengi.

Lazima ajipendekeze sana maana hatosahau tulichomfanyia mwaka 2010 kwa kumpitisha Assumpta Mshama baada ya kutudharau kwa kutuambia tule kima (Tulye e'nkende).
 
kyerwa..! tatizo la njaa lilipotokea!

je ana mchango gani kwa jamii?
 
Acha kupotosha, Kamala na Kyerwa wapi na wapi? Huyu ni mbunge wa Misenyi. Hiyo kutembelea wapiga kura wake ni kwasababu ya tetemeko la ardhi vinginevyo hana tofauti na wabunge wengine walio wengi.

Lazima ajipendekeze sana maana hatosahau tulichomfanyia mwaka 2010 kwa kumpitisha Assumpta Mshama baada ya kutudharau kwa kutuambia tule kima (Tulye e'nkende).

Nimechanganya majimbo, nisamehe kwa hilo. Ila narudia kusema tena, kwanza jimbo lake siyo jimbo nakotokea mie na pili sijamsema kwasababu yoyote ile iwayo nje ya kazi yake.

Ukitaka kunielewa vizuri na kumwelewa kwa usahihi tafuta clip kupitia Jamco.blog ama Bukobawadau.blog ndo utaelewa mie siko katika kuongelea tetemeko ijapo najua hata sahivi yuko site ( jimboni) akiendelea na ziara zake na hata wewe ukifungua hizo blog utamwona

Achia hii ya mara baada ya tetemeko, ingia hizo blog anzia mwezi January mpaka juzi kabla ya tetemeko ukaone ni kwa kiasi gani huyu mh. yuko site mda wake mwingi. Hivi vitu si stori za mtaani, we tafuta hizo clip halafu baada ya hapo njoo hapa unipinge ninachokisema


Tujifunze kama na yeye alivyojifunza, ..tujifunze kusema na tujifunze pia, kuukubali ukweli. Kumsema mwenzio yasiyo kweli tukumbuke pia, ni kosa kubwa kwa Mungu, tukiwa na Mungu daima tutausema ukweli na kuukana ulongo
 
Wewe mzushi tu hujui hata jimbo la unayemzungumzia, umetumwa bila data sahihi
 
Wewe mzushi tu hujui hata jimbo la unayemzungumzia, umetumwa bila data sahihi
Uzushi wangu nini mkuu make kama ni ishu tu ya majina ya jimbo, basi mie hilo halikuwa kipaumbele changu. Ni sawa na kutokulitaja kabisa so long as naamini ukimtaja mhusika wenye kuelewa inatosha kabisa kuelewa

Kiufupi msingi wangu ni kumjadiri mhusika kwa mazuri aliyojitahidi kuyaonesha yawe madogo/makubwa
 
kyerwa..! tatizo la njaa lilipotokea!

je ana mchango gani kwa jamii?
Hata kwa Obama nako majanga utokea, janga halina uhusiano wa lilivyotokea na uongozi uliopo. Majanga mengine ni sehemu ya mipango ya mwenyezi Mungu na hasa ukidili na nature ya janga husika. Na ndo maana hata wazungu wenyewe wanakiri kushindwa kudetect lini nini kinatokea na wapi. Sasa fikiria linapokuja kwa nchi Kama zetu hizi za "sizonje" ni kitu gani kinatokea.

Kujua mchango wake kwa wanajimbo wake tafuta kwenye s.networks ukitaka utajua.
 
Nimechanganya majimbo, nisamehe kwa hilo. Ila narudia kusema tena, kwanza jimbo lake siyo jimbo nakotokea mie na pili sijamsema kwasababu yoyote ile iwayo nje ya kazi yake.

Ukitaka kunielewa vizuri na kumwelewa kwa usahihi tafuta clip kupitia Jamco.blog ama Bukobawadau.blog ndo utaelewa mie siko katika kuongelea tetemeko ijapo najua hata sahivi yuko site ( jimboni) akiendelea na ziara zake na hata wewe ukifungua hizo blog utamwona

Achia hii ya mara baada ya tetemeko, ingia hizo blog anzia mwezi January mpaka juzi kabla ya tetemeko ukaone ni kwa kiasi gani huyu mh. yuko site mda wake mwingi. Hivi vitu si stori za mtaani, we tafuta hizo clip halafu baada ya hapo njoo hapa unipinge ninachokisema


Tujifunze kama na yeye alivyojifunza, ..tujifunze kusema na tujifunze pia, kuukubali ukweli. Kumsema mwenzio yasiyo kweli tukumbuke pia, ni kosa kubwa kwa Mungu, tukiwa na Mungu daima tutausema ukweli na kuukana ulongo
Naona umekuja kumpamba tu hapa. Huyu jirani yangu Mugana pale. Sio kwamba anakubalika sana kama unavyotaka kuaminisha. Ni kawaida sana na anatumia nguvu kubwa sana maana anajua 2005-2010 jeuri aliyofanya mpaka tukamtosa. Upinzania wangejipanga vyema na kama Focus asingeongeka hakika huyu mheshimiwa angekuwa analia.
 
Naona umekuja kumpamba tu hapa. Huyu jirani yangu Mugana pale. Sio kwamba anakubalika sana kama unavyotaka kuaminisha. Ni kawaida sana na anatumia nguvu kubwa sana maana anajua 2005-2010 jeuri aliyofanya mpaka tukamtosa. Upinzania wangejipanga vyema na kama Focus asingeongeka hakika huyu mheshimiwa angekuwa analia.
Mkuu sijasema ili kumpamba na wala sijasema kwamba anakubalika/hakubaliki.
Ni kweli huenda hakubaliki na ni kweli watu wana watu wao na mapenzi yao. Mie nimeongelea kile anachoonekana anakifanya kwa kulinganisha na wengine mnaowaona walipita kwa kukubalika zaidi.

Na huu ndo wehu wetu sisi watanzania, fulani akihisi anapendwa basi mikono yote huweka mfukoni na matokeo yake tunakuja kujuta baadae, na tumeyaona haya kwa akina Mnyika, Lema, Mdee n.k ni mfano mzuri kwa yaliyowapata mwaka jana.

Ni mara 100 ukaingia hupendwi na hutegemewi kufanya na ukafanya makubwa kuliko kuingia unaaminiwa na ukapoteza kabisa uaminifu wako
kwa unaowaongoza

Mie na wewe naamini tunaelewana na unanielewa jinsi nisivyo na upande mkuu
 
Wasalaam Watanzania nyote.
Leo nina jambo moja la kumhusu huyu Mh.Mbunge wa jimbo la Misenyi Nampongeza sana huyu mzee.

Kwanza niseme wazi, (mie sina chama) ila ninao utashi tu wa kumuangalia mtu mmoja mmoja kwa kadili ya matendo yake na hasa katika nafasi yake. Binafsi naamini kabisa approach yangu hii inanisaidia sana, nakuwa huru mda wote kupongeza na kusifia yeyote yule ama kukosoa na kamwe sibanwi na mipaka ya vyama "vyao".

Tokea uchaguzi umalizike na huyu mzee kuibuka kidedea, kuusema ukweli pasipo kuuma maneno na wala kumuonea mwingine, huyu mh. kweli ni kati ya wabunge wachache sana kutoka CCM na hata upinzani wanaoifanya kazi yao. Na hata staili yake anayoitumia ya kelele kidogo na matendo mengi a.k.a mzee wa kimya kimya iko safi sana.
Hadi kufikia leo, ni mbunge pekee kutoka mkoa wa Kagera aliyeweza kulizunguka jimbo lake kwa zaidi ya mara tatu.

Nimesoma na kuzidi kumfatilia baada ya kuvutiwa sana na anavyokuwa karibu na wanajimbo wake, huyu mzee anastahili pongezi hata kama hana anachowapa. Ninajiuliza kwa wapinzani, achana na mizigo ya CCM ambayo tumeshaizoea, ni kwanini wa upinzani walio wengi hawana spirit ya kutumikia vyeo vyao zaidi ya kuonekana wako busy na kuratibu maandamano kana kwamba waligraduate katika kuandaa maandamano

Kwa wapinzani na Lwakatare akiwemo, wanatakiwa kuelewa mahitaji ya jamii za watu wao na mahitaji yao, bora liende na mob politics havitawasaidia kamwe. Nendeni majimboni mkafanye kama Nassari a.k.a dogo janja, nendeni mkafanye kama Prof. Muhongo, fanyeni kama Dr. Diodorous Kamara. Mkitaka kuendelea kuwa wauza sura mijini mtambue 2020 siyo mbali na watanzania hawatasita kuchukua maamuzi "sahihi".

Atakaye mwona Mh. Mbunge huyu naomba ampe salaam zangu nyingi.
 
Rweye
Wewe sio bure umetumwa. kutupeleka kwenye clips za blogs alizolipia yeye na wewe hili umtangaze sivyo.
Watu wamepata majanga ya tetemeko kila mtu mwenye wadhifa na asiyekuwa nao wote walikimbilia Bukoba (Wenyeji na wasio wenyeji) na leo ni mwezi tayari (siku zaidi ya 30) huyu mzee wako ndo anakuja!! alikuwa wapi? imagine tetemeko lilitokea (source) ni jimbo lake la Nkenge!!!

Wenzake, i.e. Prof. Ana Tibaijuka toka bungeni mpaka Bukoba na kurudi kutoa taarifa ya hali halisi bungeni, Charles Mwijange, Lwakatare, nk. achilia mbali wabunge na wageni wengine wasiokuwa wanasiasa, aibu na asubiri matokeo kwani malipo ni hapa hapa duniani.

Huyu mbunge wako amekuja kama msaani hasa Ze Comedi.

Usimpambe kwa lolote amechemsha. Mfilisi. Tulikuwepo site muda wote, ili uendelee na filimbi zako tuonyeshe kwenye hizo Clip zako za blogs ni kikao gani cha mikakati, kutoa au kupokea misaada pale kwa mkuu wa mkoa, Mh. Kijuu. Hakuna!!! Alikuwa wapi muda wote? Je, huyu ni sehemu ya jamii hii unayolenga kuindanganya?

Si mfano wa kuigwa. Ameiteteaje jamii inayotabika na kulala nje wakati wadau wametoa misaada isiyofika ilikolengwa kwa kisingizio cha tathimini?

Ukome kudanganya, kweli njaa mbaya. Yuda mko wengi!!!!
 
Kwa nn aliacha ubalozi !!!??
Sijuhi na the past is gone. Ni vizuri tukamhukumu kwa anachokifanya kwasababu wanadamu huanguka, kujifunza na kuinuka.

Na navyojua ubalozi si kazi ya milele, inaisha ijapo cheo utakufa nacho
 
Mh. Kamara uko wapi Mbunge wetu?

This was posted on 14 September 2016
"Wananchi wa jimbo la NKENGE hasa wa vijiji vya Kitobo na Bugandika na baadhi ya sehemu mbalimbali za wilaya ya Misenyi tumepatwa na madhara ya tetemeko la ardhi kwa baadhi ya majumba kuanguka, kubomoka na mengine yamejaa nyufa nyingi tu lakini hadi sasa hatujakuona mbunge wetu Mh Kamara.
Uko wapi Mbunge wetu?"

Alafu unasema huna chama ila bado unaonyesha ulivyo na chama kama sio hivyo haya maneno yana uhusiano gani na hoja hii
"Na huu ndo wehu wetu sisi watanzania, fulani akihisi anapendwa basi mikono yote huweka mfukoni na matokeo yake tunakuja kujuta baadae, na tumeyaona haya kwa akina Mnyika, Lema, Mdee n.k ni mfano mzuri kwa yaliyowapata mwaka jana".

 
Sijaona mahali unapomsifu kwa kutatua kero ama kufanya jambo linalochochea maendeleo. Unamsifia kwa kutembea jimboni?? Unataka nass tusifie hilo?? Nenda Hai ukaone mbunge wao anavyohamasisha kilimo,elimu,usafi,mazingira,afya nk.
Ivi nikweli Kagera ndomkoa masikini zaid Tz??naomba kujua
 
Kamala huyu huyu aliyepigwa chini na Asumpta Mshama? Sijashangaa hajaukwaa hata unaibu waziri.
 
Wasalaam Watanzania nyote.
Leo nina jambo moja la kumhusu huyu Mh.Mbunge wa jimbo la Misenyi Nampongeza sana huyu mzee.

Kwanza niseme wazi, (mie sina chama) ila ninao utashi tu wa kumuangalia mtu mmoja mmoja kwa kadili ya matendo yake na hasa katika nafasi yake. Binafsi naamini kabisa approach yangu hii inanisaidia sana, nakuwa huru mda wote kupongeza na kusifia yeyote yule ama kukosoa na kamwe sibanwi na mipaka ya vyama "vyao".

Tokea uchaguzi umalizike na huyu mzee kuibuka kidedea, kuusema ukweli pasipo kuuma maneno na wala kumuonea mwingine, huyu mh. kweli ni kati ya wabunge wachache sana kutoka CCM na hata upinzani wanaoifanya kazi yao. Na hata staili yake anayoitumia ya kelele kidogo na matendo mengi a.k.a mzee wa kimya kimya iko safi sana.
Hadi kufikia leo, ni mbunge pekee kutoka mkoa wa Kagera aliyeweza kulizunguka jimbo lake kwa zaidi ya mara tatu.

Nimesoma na kuzidi kumfatilia baada ya kuvutiwa sana na anavyokuwa karibu na wanajimbo wake, huyu mzee anastahili pongezi hata kama hana anachowapa. Ninajiuliza kwa wapinzani, achana na mizigo ya CCM ambayo tumeshaizoea, ni kwanini wa upinzani walio wengi hawana spirit ya kutumikia vyeo vyao zaidi ya kuonekana wako busy na kuratibu maandamano kana kwamba waligraduate katika kuandaa maandamano

Kwa wapinzani na Lwakatare akiwemo, wanatakiwa kuelewa mahitaji ya jamii za watu wao na mahitaji yao, bora liende na mob politics havitawasaidia kamwe. Nendeni majimboni mkafanye kama Nassari a.k.a dogo janja, nendeni mkafanye kama Prof. Muhongo, fanyeni kama Dr. Diodorous Kamara. Mkitaka kuendelea kuwa wauza sura mijini mtambue 2020 siyo mbali na watanzania hawatasita kuchukua maamuzi "sahihi".

Atakaye mwona Mh. Mbunge huyu naomba ampe salaam zangu nyingi.
....ila niongeze kidogo kwa kusema, mbunge wako, bado si mzee...ni makamo ya mtu mzima...!
 
Wasalaam Watanzania nyote.
Leo nina jambo moja la kumhusu huyu Mh.Mbunge wa jimbo la Misenyi Nampongeza sana huyu mzee.

Kwanza niseme wazi, (mie sina chama) ila ninao utashi tu wa kumuangalia mtu mmoja mmoja kwa kadili ya matendo yake na hasa katika nafasi yake. Binafsi naamini kabisa approach yangu hii inanisaidia sana, nakuwa huru mda wote kupongeza na kusifia yeyote yule ama kukosoa na kamwe sibanwi na mipaka ya vyama "vyao".

Tokea uchaguzi umalizike na huyu mzee kuibuka kidedea, kuusema ukweli pasipo kuuma maneno na wala kumuonea mwingine, huyu mh. kweli ni kati ya wabunge wachache sana kutoka CCM na hata upinzani wanaoifanya kazi yao. Na hata staili yake anayoitumia ya kelele kidogo na matendo mengi a.k.a mzee wa kimya kimya iko safi sana.
Hadi kufikia leo, ni mbunge pekee kutoka mkoa wa Kagera aliyeweza kulizunguka jimbo lake kwa zaidi ya mara tatu.

Nimesoma na kuzidi kumfatilia baada ya kuvutiwa sana na anavyokuwa karibu na wanajimbo wake, huyu mzee anastahili pongezi hata kama hana anachowapa. Ninajiuliza kwa wapinzani, achana na mizigo ya CCM ambayo tumeshaizoea, ni kwanini wa upinzani walio wengi hawana spirit ya kutumikia vyeo vyao zaidi ya kuonekana wako busy na kuratibu maandamano kana kwamba waligraduate katika kuandaa maandamano

Kwa wapinzani na Lwakatare akiwemo, wanatakiwa kuelewa mahitaji ya jamii za watu wao na mahitaji yao, bora liende na mob politics havitawasaidia kamwe. Nendeni majimboni mkafanye kama Nassari a.k.a dogo janja, nendeni mkafanye kama Prof. Muhongo, fanyeni kama Dr. Diodorous Kamara. Mkitaka kuendelea kuwa wauza sura mijini mtambue 2020 siyo mbali na watanzania hawatasita kuchukua maamuzi "sahihi".

Atakaye mwona Mh. Mbunge huyu naomba ampe salaam zangu nyingi.
Una matatizo gani kichwani? Hii ni mara ya kwanza jamaa yako kushika nafasi hiyo? Mwambie atulie tu! Maamuzi mabaya, uchaguzi mbaya wa nafasi ya kazi. Miscalculation!
 
Back
Top Bottom