BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Homa mitihani kuvuja
na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
SAKATA la kuvuja kwa mitihani ya kidato cha nne linazidi kuchukua sura mpya tangu Baraza la Taifa la Mitihani lilipotangaza kuahirisha mtihani wa somo la Hisabati.
Siku chache tu baada ya hatua hiyo ambayo imefuatiwa na shinikizo la kutaka baadhi ya watendaji na viongozi wa serikali kujiuzulu, hali inaonyesha kuzidi kuwa mbaya.
Katika hatua moja jana, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe, jana alikwepa kuzungumza na wanahabari waliokwenda ofisini kwake kupata kauli yake juu ya kuwapo kwa shinikizo hilo la kumtaka ajiuzulu kutokana na kuvuja huko kwa mitihani.
Taarifa za awali kwamba Maghembe angezungumza na waandishi wa habari zilibadilika baada ya kutolewa habari kwamba alikuwa ametingwa na shughuli nyingi za kiofisi.
Badala yake, maofisa wa wizara hizo waliwaeleza waandishi wa habari waliokuwa na shauku ya kumsikia Maghembe kwamba kazi hiyo ingefanywa na mtu mwingine wizarani hapo.
Uamuzi huo ulisababisha waandishi hao waanze kuzungushwa kutoka ofisi moja kwenda nyingine kusaka mtu sahihi wa kuzungumza.
Hata hivyo hakuna ofisa yeyote aliyekuwa tayari kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu sakata hilo ambalo limekuwa likichukua sura mpya kila kukicha.
Mmoja wa maofisa wa wizara hiyo, ambaye hata jina lake hakutaka kulitaja, alisema hawezi kuzungumza na waandishi wa habari kwani tangu amekuwa ndani ya wizara hiyo kwa zaidi ya miaka 20, hajawahi kuzungumza na vyombo vya habari.
Mimi nashangaa, tangu nimeanza kazi hapa ni miaka 20, sijawahi kuwaona waandishi wa habari ofisini kwangu, wala kuzungumza nao, leo nimeletewa nitawaambia nini jamani? alisema na kuongeza kuwa, kuna wasemaji wa masuala hayo na yeye, hausiki.
Ofisa mwingine wizarani hapo ambaye hakupenda kutaja jina lake, alijitetea kuwa suala la kuvuja mitihani linamhusu Katibu wa Baraza, Dk. Ndalichako na Waziri Maghembe, na akawataka waandishi kuwafuata wao.
Hili ni suala la kimaadili zaidi na linamhusu Maghembe yeye mwenyewe. Mfuateni yeye azungumze, alitolee ufafanuzi, sisi wengine hatuwezi kuingilia, alisema ofisa huyo.
Wakati waandishi wakiendelea kumsubiri Profesa Maghembe, Ofisa Habari wa wizara hiyo, Ntabi Bunyanzu, alitoa taarifa kwamba wizara ingetoa taarifa baada ya kikao cha Bodi ya Baraza la Mitihani (NECTA) kilichokuwa kikifanyika jana hiyo hiyo.
Wakati maofisa wizarani wakitupiana mpira, mjini Dodoma jana kulikuwa na taarifa za kuvuja kwa kiwango kikubwa kwa mtihani wa somo la Jiografia unaofanyika leo.
Taarifa hizo za kuvuja kwa mtihani huo, ambao ulidaiwa kuzagaa mitaani zilisambaa kwa kasi kubwa katika maeneo mbalimbali ya mji huo.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima ambayo pia iliziona baadhi ya nakala za mtihani huo, umebaini kuwa mtihani huo ulikuwa ukiuzwa kwa bei ya kati ya sh 300,000 na sh 200,000.
Kwa mujibu wa uchunguzi huo, baadhi ya wauzaji wa nakala hizo walielezwa kuwa walifikia hatua ya kutaka kulipwa fedha kwa makubaliano kwamba, malipo yangefanyika baada ya watahiniwa kutoka nje ya vyumba vya mitihani leo hii na kujiridhisha kuwa mitihani iliyovuja ilikuwa ni ya kweli.
Habari za uhakika zinaonyesha kwamba, kwa kipindi kirefu jana, watahiniwa wengi waliokuwa wamepata nakala hizo za mtihani wa Jiografia walikuwa wamejifungia katika vyumba vya baadhi ya nyumba za kulala wageni, wakiwa na walimu waliowalipa fedha kwa ajili ya kuwafanyia mitihani hiyo leo.
Baadhi ya wanafunzi waliozungumza na Tanzania Daima, walikielezea kitendo cha watu waliowapa mitihani hiyo kukataa kupokea fedha mapema kuwa ni kielelezo kwamba mitihani iliyovuja ni ya kweli.
Tumepata kwa mtu tunayemuamini sana na kwa vile ametuambia tulipe baada ya kuufanya mtihani huo leo, tunashawishika kuamini kuwa mtihani huo ni halisi, alisema mmoja wa wanafunzi aliyekiri kuona nakala ya mtihani wa Jiografia.
Vyanzo vyetu vya habari vinasema kuwa mtihani huo umevuja kutoka kwenye moja ya vyuo vikubwa vya mjini hapa.
Kutokana na hali hiyo, baadhi ya wananchi waliotoa maoni yao, walitaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya watendaji wa Baraza la Mitihani nchini (NECTA), kwa kuhusika na uvujaji huo wa mitihani.
Wananchi hao walisema kuwa serikali inapaswa kuifuta mitihani yote, badala ya mmoja wa Hisabati, kwani kuna uwezekano mkubwa wa mitihani yote kuvuja.
Ofisa Elimu wa Mkoa wa Dodoma alipotakiwa kuzungumzia hali hiyo, hakuwapo ofisini kwake, lakini msaidizi wake aliyejitambulisha kwa jina moja la Msoma, alisema ofisi yake imepata taarifa hizo na ilikuwa imeshaanza kuzifuatilia kwa karibu na akaahidi kutoa taarifa zaidi leo.
na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
SAKATA la kuvuja kwa mitihani ya kidato cha nne linazidi kuchukua sura mpya tangu Baraza la Taifa la Mitihani lilipotangaza kuahirisha mtihani wa somo la Hisabati.
Siku chache tu baada ya hatua hiyo ambayo imefuatiwa na shinikizo la kutaka baadhi ya watendaji na viongozi wa serikali kujiuzulu, hali inaonyesha kuzidi kuwa mbaya.
Katika hatua moja jana, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe, jana alikwepa kuzungumza na wanahabari waliokwenda ofisini kwake kupata kauli yake juu ya kuwapo kwa shinikizo hilo la kumtaka ajiuzulu kutokana na kuvuja huko kwa mitihani.
Taarifa za awali kwamba Maghembe angezungumza na waandishi wa habari zilibadilika baada ya kutolewa habari kwamba alikuwa ametingwa na shughuli nyingi za kiofisi.
Badala yake, maofisa wa wizara hizo waliwaeleza waandishi wa habari waliokuwa na shauku ya kumsikia Maghembe kwamba kazi hiyo ingefanywa na mtu mwingine wizarani hapo.
Uamuzi huo ulisababisha waandishi hao waanze kuzungushwa kutoka ofisi moja kwenda nyingine kusaka mtu sahihi wa kuzungumza.
Hata hivyo hakuna ofisa yeyote aliyekuwa tayari kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu sakata hilo ambalo limekuwa likichukua sura mpya kila kukicha.
Mmoja wa maofisa wa wizara hiyo, ambaye hata jina lake hakutaka kulitaja, alisema hawezi kuzungumza na waandishi wa habari kwani tangu amekuwa ndani ya wizara hiyo kwa zaidi ya miaka 20, hajawahi kuzungumza na vyombo vya habari.
Mimi nashangaa, tangu nimeanza kazi hapa ni miaka 20, sijawahi kuwaona waandishi wa habari ofisini kwangu, wala kuzungumza nao, leo nimeletewa nitawaambia nini jamani? alisema na kuongeza kuwa, kuna wasemaji wa masuala hayo na yeye, hausiki.
Ofisa mwingine wizarani hapo ambaye hakupenda kutaja jina lake, alijitetea kuwa suala la kuvuja mitihani linamhusu Katibu wa Baraza, Dk. Ndalichako na Waziri Maghembe, na akawataka waandishi kuwafuata wao.
Hili ni suala la kimaadili zaidi na linamhusu Maghembe yeye mwenyewe. Mfuateni yeye azungumze, alitolee ufafanuzi, sisi wengine hatuwezi kuingilia, alisema ofisa huyo.
Wakati waandishi wakiendelea kumsubiri Profesa Maghembe, Ofisa Habari wa wizara hiyo, Ntabi Bunyanzu, alitoa taarifa kwamba wizara ingetoa taarifa baada ya kikao cha Bodi ya Baraza la Mitihani (NECTA) kilichokuwa kikifanyika jana hiyo hiyo.
Wakati maofisa wizarani wakitupiana mpira, mjini Dodoma jana kulikuwa na taarifa za kuvuja kwa kiwango kikubwa kwa mtihani wa somo la Jiografia unaofanyika leo.
Taarifa hizo za kuvuja kwa mtihani huo, ambao ulidaiwa kuzagaa mitaani zilisambaa kwa kasi kubwa katika maeneo mbalimbali ya mji huo.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima ambayo pia iliziona baadhi ya nakala za mtihani huo, umebaini kuwa mtihani huo ulikuwa ukiuzwa kwa bei ya kati ya sh 300,000 na sh 200,000.
Kwa mujibu wa uchunguzi huo, baadhi ya wauzaji wa nakala hizo walielezwa kuwa walifikia hatua ya kutaka kulipwa fedha kwa makubaliano kwamba, malipo yangefanyika baada ya watahiniwa kutoka nje ya vyumba vya mitihani leo hii na kujiridhisha kuwa mitihani iliyovuja ilikuwa ni ya kweli.
Habari za uhakika zinaonyesha kwamba, kwa kipindi kirefu jana, watahiniwa wengi waliokuwa wamepata nakala hizo za mtihani wa Jiografia walikuwa wamejifungia katika vyumba vya baadhi ya nyumba za kulala wageni, wakiwa na walimu waliowalipa fedha kwa ajili ya kuwafanyia mitihani hiyo leo.
Baadhi ya wanafunzi waliozungumza na Tanzania Daima, walikielezea kitendo cha watu waliowapa mitihani hiyo kukataa kupokea fedha mapema kuwa ni kielelezo kwamba mitihani iliyovuja ni ya kweli.
Tumepata kwa mtu tunayemuamini sana na kwa vile ametuambia tulipe baada ya kuufanya mtihani huo leo, tunashawishika kuamini kuwa mtihani huo ni halisi, alisema mmoja wa wanafunzi aliyekiri kuona nakala ya mtihani wa Jiografia.
Vyanzo vyetu vya habari vinasema kuwa mtihani huo umevuja kutoka kwenye moja ya vyuo vikubwa vya mjini hapa.
Kutokana na hali hiyo, baadhi ya wananchi waliotoa maoni yao, walitaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya watendaji wa Baraza la Mitihani nchini (NECTA), kwa kuhusika na uvujaji huo wa mitihani.
Wananchi hao walisema kuwa serikali inapaswa kuifuta mitihani yote, badala ya mmoja wa Hisabati, kwani kuna uwezekano mkubwa wa mitihani yote kuvuja.
Ofisa Elimu wa Mkoa wa Dodoma alipotakiwa kuzungumzia hali hiyo, hakuwapo ofisini kwake, lakini msaidizi wake aliyejitambulisha kwa jina moja la Msoma, alisema ofisi yake imepata taarifa hizo na ilikuwa imeshaanza kuzifuatilia kwa karibu na akaahidi kutoa taarifa zaidi leo.