Hoja ya Udikteta wa Magufuli: Tundu Lissu isn't Right. Haupingwi kwa kupaza sauti kupiga tu Kelele!

Hoja ya Udikteta wa Magufuli: Tundu Lissu isn't Right. Haupingwi kwa kupaza sauti kupiga tu Kelele!

Aliyewaita chadema nyumbu hakukosea sio kwa mapovu hayo nendeni mkafulie kwanza

Mayalla amechambua kwa undani kabisa kawaambia mapungufu yenu kuwa siku zote chadema ni ma laymen wa kurukaruka tu hamna hoja

Sasa hamna jipya ngoja JPM awanyooshe tu
 
Ndugu... hebu tupe mifano kidogo yenye ushahidi wa haki zilizominywa Mahakamani kwasababu ya maelekezo ya Kisiasa. Lakini pia majaji waliojizulu kutokana na kuingiliwa kwa Mahakama. Otherwise this is Speculations tu.

Unaongelewa wabunge wa upinzani kunyamazishwa bungeni na kutolewa nje. Hivi kwnn watu mnapenda kuwa waongo kiasi hichi? Wabunge wengi wa upinzani waliokwishatolewa nje ( Myika, Mdee na Bulaya) ni kwasbb tu ya utovu wa nidhamu na kuvunja kanuni za Bunge kwa makusudi kwsbb wanajua kuna nyumbu nje watawatetea.

Sent from my SM-A310F using JamiiForums mobile app
utakuwa umevaa mawani ya mbao na earphones za lami! tumemsikia mkuu akimuamuru spika awashughulikie wabunge wa upinzani bungeni na yeye mkuu atakuwa anawashughulikia wakiwa nje ya bunge! au hukuwepo?
 
Chadema kuna tatizo kubwa la matumizi ya busara katika kauli za baadhi ya viongozi wake. Unaweza kukosoa kwa lugha ya kistaarabu na kwa unyenyekevu ukafikisha ujumbe vizuri zaidi kuliko kutumia lugha kali, machukizo, matukano na lugha isiyo ya staha.

Nafikiria utakuwa unatania au huelewi maana ya busara na uropokaji, ili uwe na busara ni lazima uwe na intelligence + rational za kutosha, sasa imagine km Lissu hana busara hali ikoje kwa watz ukianza na uchwara kuja kwako?



Sent using Jamii Forums mobile app
kwanini chadema tuu ndio wawe wastaarabu na hao wengine wako free kuropoka, kuudhi, kutusi na kuweka ndani? be objective
 
Effective name ni lile alilopewa yeye yaani Paskali. La wazazi wake ama mababu zake halina nafasi. Kikwetu jina baya uua Paka, Paskali siyo Mayalla
Mayala kwa kisukuma maana yake njaa!

Kabla ya kutoa opinion ni bora ukawa unajiumiza kidogo kufanya utafiti na kujua nature ya suala ndugu Mayala,Ukiudisect ushauri wako, utaona kwamba ushauri wako ni one dimensional kwa issue complex ambazo kiuchache dimensions zake ni Legal-Social-Political!

Sasa, huwezi kuja na jibu jepesi kama hilo ulilolisema ndugu Mayala katika issue yenye dimensions nyingi!

Halafu unatumia Logical Fallacy ya Ad-hominem attack kwenye hoja yako ( yaani unashambulia personality ya mtu), kwa mfano maneno kama vile " anaropoka" hayaifanyi hoja yako iwe na nguvu!

Je wewe ndugu Mayala umeshafungua kesi mahali popote?, au unamsubiri Lissu afungue ili uje tena hapa uanzishe thread akishindwa mahakamani?.

Ndugu Mayala if you think you are right then lead the way!!
 
Kwa kawaida, mtu akipambana na mgomvi wake kwa zote halafu akashindwa, kinachobaki huwa ni MATUSI, KEJELI na MAMBO MENGINE ya kipuuzi yanayofanana na hayo.
Kasi ya JPM imewamaliza kabisa CDM, kilichobaki kwao ni hayo yanayoendelea sasa.
Kwa style hii, ni rahisi zaidi kuendesha gari lisilo na MATAIRI kuliko CDM kushika dola.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba nianze kwa kumpongeza Mhe. Tundu Lisu Kwa kutokuwa muoga kuizungumzia dhana ya udikiteta Tanzania bila uoga, japo the way anavyoielezea anazungumza kwa style ile ile ya uropokaji, the Magufuli style, hivyo kuonekana kama insane fulani
UNAMAANISHA NA MAGUFULI ANAPOTOA HOJA ANAONEKANA KANA LISSU ALIVYO INSANE?
 
Mayala kwa kisukuma maana yake njaa!

Kabla ya kutoa opinion ni bora ukawa unajiumiza kidogo kufanya utafiti na kujua nature ya suala ndugu Mayala,Ukiudisect ushauri wako, utaona kwamba ushauri wako ni one dimensional kwa issue complex ambazo kiuchache dimensions zake ni Legal-Social-Political!

Sasa, huwezi kuja na jibu jepesi kama hilo ulilolisema ndugu Mayala katika issue yenye dimensions nyingi!

Halafu unatumia Logical Fallacy ya Ad-hominem attack kwenye hoja yako ( yaani unashambulia personality ya mtu), kwa mfano maneno kama vile " anaropoka" hayaifanyi hoja yako iwe na nguvu!

Je wewe ndugu Mayala umeshafungua kesi mahali popote?, au unamsubiri Lissu afungue ili uje tena hapa uanzishe thread akishindwa mahakamani?.

Ndugu Mayala if you think you are right then lead the way!!
Nimeipenda sana hii. Thanks Gamba la Nyoka
 
Kwa sasa mahakama kuu ya Tanzania sio Taasisi huru,majaji wanaingiliwa kwenye shughuli zao mpaka wanaamua kujiuzuru,

Na kama mahakama inaingiliwa kwenye kutenda haki,haki zetu tuzitafutie wapi?je kuna haja ya kupeleka kesi mahakamani katika hali hii au tuangalie namna nyingine? Kama unazizuia mahakama zisitupe haki,na sisi kama nchi tunataka haki na tumekubaliana kikatiba tutaipata mahakamani,na wewe umezizuia mahakama zisitoe haki,nchi nzima ikiamua kutafuta mbadala wa mahakama nchi hii itakalika?

Wabunge bungeni mnawafukuza na kuwatisha,mnataka taifa lisemee wapi? Bunge ni mahala pa mijadala ya taifa,wakianza kujadili mnawafukuza na kuwatisha

Serikali nayo ikisikia watu wanatumia Uhuru wao kujadili,wanatuma polisi kuwakamata

Kuna kihadithi fulani kinasema kwamba hata umuwekeee vifaranga mia,ukimuachia tu,mwewe atapaa na kuondoka,Uhuru ni kitu cha asili cha binadamu,

Mkoloni na mabomu yote na mabunduki,hakufanikiwa kumnyamazisha Nyerere,kenyata,Mandela,Mugabe,

Leo karne ya 21 unawaza kuzuia watu wasiongee?

Wapinzani waliongea tena kwa ruksa na kukingiwa kifua na Nyerere baada ya tume ya Nyalali,

Leo wewe ni nani wa kumshinda Nyerere busara? Wewe unaweza kumshinda baba wa taifa kwa maono? Ccm walikataa vyama vingi,Nyerere akawaambia acheni ujinga,na wakati Mkapa anaomba urais,nyerere hakuzuia wapinzani wasipige kampeni,alisema muacheni Lyatonga mashabiki wake wamsukume gari lake,mrema yuko mwanza kwenye kampeni ,nyerere yuko mbeya,hakuamuru lyatonga akamatwe

Mtoto wa Nyerere alikuwa NCCR,Nyerere wala hakuumia kichwa... Leo hii unataka kufukia jalalani busara za Nyerere? Kwa ugwiji upi wa kisiasa ulio nao?

Mwinyi alitaka kuleta Tanganyika,Nyerere akamwambia ilani tuliyokupa haina hiyo hoja,umeitolea wapi? Leo ilani INA hoja ya mimba za wasichana,unaikataa,kwa hiyo kwenye kampeni mlikuwa mnawadanganya watu? Ccm itwambie kwamba ilani yao iko kichwani kwako au wana kitabu maalum cha ilani kinachoongoza mambo mbalimbali ikiwemo Uhuru wa mahakama
Dah, watu wana mambo moyoni jamani, eeeh! Wakipata nafasi ya kufunguka wanafanya kweli. Taifa lina haja ya kujitafakari. Asante chinembe
 
Katika jinsi ya kupinga udikiteta Tanzania, Tundu Lisu ametuasa tupaze sauti zetu kuupinga huu udikiteta kwa kupiga kelele ambako huku ni kuipinga kisiasa, wakati hoja halisi ya udikiteta, sio hoja ya kisiasa ni hoja ya kisheria. Hoja za kisiasa zishughulikiwe kisiasa, na hoja za kisheria, zishughulikiwe kisheria. Kushughulikia kisiasa kwa hoja za kisheria, ni kujifurahisha tuu, kamwe hakutaleta matokeo yoyote chanya.

Mkuu Paskali. Huna tofauti na hoja za majuzi kama si jana ya Dr.wetu alituacha na kuvuka mipaka. Nadhani unakukmbuka rekodi za Mch. R.I.P (Mtikila). Hukumu ya Mahakama ya Afrika mpaka leo iko hai lakini Serikali haijatimiza jukumu lake. Kwanini ?????????????????. Kwa hiyo tukubaliane kwenda mahakamani ni sawa ilikuweka kubukumbu sawa lakini matokeo kwenye utekelezaji wa hukumu ni 0.
 
Wanabodi,

Declaration of Interest, mimi Paskali, sio mwanachama, mshabiki au mfuasi wa chama chochote cha siasa, bali hoja zangu zote hutanguliza mbele maslahi ya taifa kwa kuzitoa truthfully, with objectivity, impartiality na balance. Kwa vile watu humu wana vyama vyao na viongozi wao ambao wengine wana waabudia, hivyo nakujua fika kinachomfika mtu atakayepandisha hoja, kuwapinga waabudiwa wao!.

Naomba nianze kwa kumpongeza Mhe. Tundu Lisu Kwa kutokuwa muoga kuizungumzia dhana ya udikiteta Tanzania bila uoga, japo the way anavyoielezea anazungumza kwa style ile ile ya uropokaji, the Magufuli style, hivyo kuonekana kama insane fulani, lakini ujumbe umefika.



Kwanza naomba kukiri kuwa mimi Paskali sio mwanasheria, Mhe. Tundu Lisu ni mwanasheria, hivyo mimi nazungumza kama a layman, na Tundu Lisu, japo kwanza mwanasheria kisha ndipo akawa mwanasiasa, mtu kuwa mwanasheria hakukufanyi always kuwa right, na mtu just a layman, anaweza kabisa kutofautiana na mwanasheria mbobezi na akawa right, mfano ni huu
Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele! | Page ...

Katika jinsi ya kupinga udikiteta Tanzania, Tundu Lisu ametuasa tupaze sauti zetu kuupinga huu udikiteta kwa kupiga kelele ambako huku ni kuipinga kisiasa, wakati hoja halisi ya udikiteta, sio hoja ya kisiasa ni hoja ya kisheria. Hoja za kisiasa zishughulikiwe kisiasa, na hoja za kisheria, zishughulikiwe kisheria. Kushughulikia kisiasa kwa hoja za kisheria, ni kujifurahisha tuu, kamwe hakutaleta matokeo yoyote chanya.

Naomba kutofautina na Mhe. Tundu Lisu katika hili la udikiteta, kwa hoja kuwa udikiteta haupingwi kwa Press Conference, kwa maandamano, kwa mikutano ya hadhara, kwa kupaza sauti na kupiga kelele.

Udikiteta unapingwa kwa njia moja tuu, Court Review kupitia Mamlaka ya Mahakama Kuu kutoa kitu kinachoitwa Prerogative orders ziko 6, ila maarufu zaidi ni 3. (
  • certiorari, an order by a higher court directing a lower court to send the record in a given case for review;
  • mandamus, an order issued by a higher court to compel or to direct a lower court or a government officer to perform mandatory duties correctly;
  • prohibition, directing a subordinate to stop doing something the law prohibits;
  • habeas corpus, demands that a prisoner be taken before the court to determine whether there is lawful authority to detain the person;
  • quo warranto, requiring a person to show by what authority they exercise a power.
  • procedendo, to send a case from an appellate court to a lower court with an order to proceed to judgment) mtanisamehe sizijui Kiswahili chake.
Hivyo Lisu kama mwanasheria mbobezi, Mwenyekiti wa TLS na Mwanasheria Mkuu wa Chadema alipaswa kwanza kutumia the legal local remedies available, kwanza kuuthibitisha huo udikiteta, zikishindikana ndipo sauti zipazwe ili kusaidiwa na jumuiya ya kimataifa.

Udikiteta wa Magufuli Ulianza Lini?.
Kuna wengi humu wanaousikia udikiteta wa Magufuli wakidhani umeanza leo, no!, kuna aina mbili za vyanzo vya udikiteta na aina mbili za udikiteta.
Vyanzo vya udikiteta ni
1. Hulka ya Udikiteta nimeizungumza hapa -
Yajue Makundi 10 Top Ten wa CCM, Ambamo Watatoa Top 5, Top 3 na ...

2. Mazingira ya Udikiteta nimeyazungumza hapa
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...

Aina za udikiteta
1. Udikikiteta Katili nimeuzungumza hapa-
Character Assassination ni Modus Oparandi ya Madikiteta Katili ...

2. Udikiteta Uzalendo nimeuzungumza hapa-
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...

Jee ni Kweli Tanzania Tuna Udikiteta?.
Hili ndilo swali kuu la msingi la kujiuliza, jee ni kweli Tanzania tuna udikiteta?.
Hili nimelizungumzia hapa
Udikiteta ni Dhana Tuu or ni Real?. "Lets Call A Spade A Spade ...
Udikiteta: Uongo Ukisemwa Sana na Kuachwa Bila Kukanushwa Hugeuka ...


Udikiteta wa Vyama: CCM ni chama cha Kidikiteta, Ila pia Chadema ni Chama cha Kidikiteta.
Udikiteta wa vyama ni jinsi vyama vinavyoendesha mambo yake, haswa wakati wa uchaguzi wa viongozi wake, vyama karibu vyote vinahubiri demokrasia, lakini vinaendeshwa kidikiteta.
Udikiteta wa CCM katika uchaguzi wa viongozi wake, nimeuzungumza hapa
Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC! | Page 9 ...

Kwenye hili la udikiteta, hata Chadema hawana demokrasia hiyo wanayoihubiri, tena kuna hatari, hata kama ni Chadema wengeshinda uchsaguzi wa 2015, wangeweza kuendesha nchi hii kwa udikiteta wa ajabu kuliko hata huu tunaoushuhudia sasa. Hili nililiona na nililizungumza hapa
CHADEMA Ikipewa Nchi, October 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala ...

Chadema na Matumizi ya Busara: Chama Cha Kiharakati, Hakiwezi Kupewa Nchi Kutawala!.
Chadema kuna tatizo kubwa la matumizi ya busara katika kauli za baadhi ya viongozi wake. Unaweza kukosoa kwa lugha ya kistaarabu na kwa unyenyekevu ukafikisha ujumbe vizuri zaidi kuliko kutumia lugha kali, machukizo, matukano na lugha isiyo ya staha. Wakati tukielekea uchaguzi wa 2015, tulishauri humu, ili Chadema kiweze kuaminiwa na kukabidhiwa nchi, ni lazima kionyeshe ukomavu, maturity, kufuatia kwa muda mrefu Chadema kujitanabaisha kama ni chama cha kiharakati, tulishauri Chadema kujibadili kutoka chama cha kiharakati, kuwa chama tawala chenye uwezo wa kuongoza nchi.
CHADEMA: Tujadili Utayari wa Kutawala Nchi 2015 | Page 7 ...
Kuelekea 2015: CHADEMA Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If ...

Hata walipounda UKUTA, akina sisi tuliwashauri humu
Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane ...

A Way Forward Kuelekea 2020, Kwa Kwa Udikiteta Huu Uliopo, na Siasa Hizi za Chadema, Do They Stand A Chance?.
Naomba kuwasilisha.
Hakuna kitu kigumu kukizungumza humu jf kama ukweli mchungu!, wengi wetu humu wataanza kuizungumzia 2020 on 2019, by that time it will be too little too late!, sisi waona mbali, tunaizungumzia 2020 sasa, ili kutoa muda wa gestation period ya kujipanga and to do something worthwhile before its too late.
CHADEMA Hamkujipanga, hamjajipanga, hamjipangi na hamtajipanga ...
Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible ...
CHADEMA Chama cha Ajabu Sana!.Kwenda Mahakamani Kwa Non Issue ...


Kwa siasa hizi Chadema inazokwenda nazo, kwenye mazingira ya udikiteta huu uliopo, kama hawatabadilika, I'm very sorry to say....
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020 ...

Je, Kasi ya Magufuli itaua Upinzani Uchwara na Kuimarisha Upinzani ...

In 2015 Election, Tanzania had A Choice To Choose From. Jee Kwa ...


Paskali
Rejea Kuhusu Udikiteta.
Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia ...

Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...

Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The ...

Je, Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya ...

Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote | Page ...

Nimetishwa, Kushitushwa na Kuogopeshwa na Kauli Hii ya Rais ..

Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ...

Rejea Kumhusu Tundu Lisu
Vurugu za Bungeni: Mhe.Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni ...
Mhe. Tundu Lissu, Please Acha Kumsulubu Spika Wetu!, Unammaliza ...
Usiyoyajua Kuhusu Nyerere: Shuleni Alikuwa Toto Tundu!, Almanusura ...
Kazi nzuri Tundu Lissu Antipas! | Page 10 | JamiiForums | The Home ...
Swali la Kizushi: Kwa Nini Job Ndugai Anamuogopa Tundu Antipasi ...
Opinion: Kung'atuka Kwa Zitto, CHADEMA, Msishangilie, Mkajisahau ...


Lissu yuko sahihi, watu kupiga kelele ni hatua ya kwanza kabisa. lazima kumobilise watu, hii ni vita ya watu wote. wachache hawawezi kushinda vita kubwa namna hii, ambayo ni multi-dimensional!!
 
Ndugu... hebu tupe mifano kidogo yenye ushahidi wa haki zilizominywa Mahakamani kwasababu ya maelekezo ya Kisiasa. Lakini pia majaji waliojizulu kutokana na kuingiliwa kwa Mahakama. Otherwise this is Speculations tu.

Unaongelewa wabunge wa upinzani kunyamazishwa bungeni na kutolewa nje. Hivi kwnn watu mnapenda kuwa waongo kiasi hichi? Wabunge wengi wa upinzani waliokwishatolewa nje ( Myika, Mdee na Bulaya) ni kwasbb tu ya utovu wa nidhamu na kuvunja kanuni za Bunge kwa makusudi kwsbb wanajua kuna nyumbu nje watawatetea.

Sent from my SM-A310F using JamiiForums mobile app
Siku Mnyika anatolewa kama kibaka kosa lilikuwa la nani?! Au mapenzi yanakusumbua

Cairo's
 
Aliyewaita chadema nyumbu hakukosea sio kwa mapovu hayo nendeni mkafulie kwanza

Mayalla amechambua kwa undani kabisa kawaambia mapungufu yenu kuwa siku zote chadema ni ma laymen wa kurukaruka tu hamna hoja

Sasa hamna jipya ngoja JPM awanyooshe tu
Akina Gaddafi, Sadaam, Bokassa, Amini etc waliishia kujinyoosha Wenyewe

Cairo's
 
Back
Top Bottom