Hoja ya kubadilisha Wimbo wa Taifa

getrusa

JF-Expert Member
Aug 16, 2013
2,150
1,812
Kwa wote wanao husika,

Wakuu amani iwe kwenu, kwa siku za karibuni kumekuwa na mijadala isiyo rasmi inayohusiana na wimbo wetu wa Taifa, ambapo pamoja na mambo mengine wimbo huu unatengeneza hoja mbali mbali ambazo nyingine zinaumiza hisia za Watanzania wanahisi kudhihakiwa kwa Utanzania na tunu yao ya Taifa.

Na Wengine unaumiza maisha yao na familia zao kama Watanzania wenzetu bila kujali itikadi zao za kisiasa. Mfano Nusrat na wenzie tukumbuke hawa ni ndugu zetu pia.

Msingi wa hoja yangu ni Uhalali wa kuufanya wimbo huu wa Taifa kwa maana ya hati miliki ya wimbo huu kwa Taifa letu, kwa sabbu kwa umaarufu wake umeshahaririwa na Mataifa mbalimbali.

Mtunzi wa wimbo huu sio Mtanzania, hivyo huenda hata hati miliki au umiliki wa Utunzi wa Wimbo huu sio wa Tanzania, (sio Wetu)..
wimbo huu unatumika Zambia, Afrika ya Kusini huenda Nchi nyingine pia, hivyo sidhani kama haki ya kubadirisha maneno ya wimbo huo inazuiwaa kisheria..

Angalizo:
Huenda kikaibuka kizazi kitakachodai haki miliki ya wimbo huu, kutoka katika Uzao wa marehemu Mtunzi na kupeleka jambo hili katika vyombo vinavyosimamia hati miliki na sisi kama Taifa tukajikuta tunapaswa kulipa gharama ambazo hazikuwa na ulazima.

Ushauri:
Kuna nyimbo zinazochochea Uzalendo na hari ya kuwa Mtanzania zikiimbwa hata ukiwa mbali ya Nje ya Tanzania unaungwanishwa kihisia na Nchi yako.

Nyimbo hizi zimetungwa na Watanzania wenyewe.
Mfano: " TANZANIA TANZANIA NAKUPENDA KWA MOYO WOTE "

AU "TAZAMA RAMANI UTAONA NCHI NZURI..."

Nyimbo hizi zimebeba ujumbe wa ndani sana wa Uzalendo wa Taifa letu..

Enyi wabunge watarajiwa na Watanzania kwa Ujumla nawasilisha kwa heshima jambo hili mbele yenu ili tusiendelee kuumizana bila sabbu za msingi..

Ahsanteni.
 
Hakika ni wimbo ulioshiba ujumbe na mashairi yanayostahiki kuimbwa ili kukuza uzalendo..
Nafikiri Tanzania nakupenda kwa moyo wote ndio ungekuwa wimbo wa Taifa letu.
 
Nafikiri Tanzania nakupenda kwa moyo wote ndio ungekuwa wimbo wa Taifa letu.

Hauna tofauti sana na wimbo wa kumpamba tu mpenzi wako. Ni wimbo mzuri, lakini hauweki msisitizo kwenye nguzo muhimu za taifa. Pia sio kawaida kwa wimbo wa taifa lolote kumalizika bila kutoa rai kwa Mungu kuliweka taifa kwenye mbawa zake!
 
Hauna tofauti sana na wimbo wa kumpamba tu mpenzi wako. Ni wimbo mzuri, lakini hauweki msisitizo kwenye nguzo muhimu za taifa. Pia sio kawaida kwa wimbo wa taifa lolote kumalizika bila kutoa rai kwa Mungu kuliweka taifa kwenye mbawa zake!
Unaweza kufanyiwa marekebisho na kuingiza ubeti juu ya Muumba.
 
Mtunzi wa huu wimbo Ni muafrica na Africa Ni moja. Huu wimbo ni wakihistoria ndio maana mataifa kadhaa wanautumia. Hizo hisia za kuupinga zitoke kabisa ndani yetu
 
Unaweza kufanyiwa marekebisho na kuingiza ubeti juu ya Muumba.

Kuongeza ubeti mmoja juu ya Muumba kwenye love song hakuifanyi love song kuwa national anthem.

Ukilinganisha maudhui ya huu wimbo na yale ya wimbo wa sasa wa taifa, utagundua kuwa kweli hii ni love song na mwingine ni national anthem!

Kuibadili hii love song kuwa national anthem, lazima hii love song ifanyiwe total overhaul.
 
Sote ni waafrika lakini Tunapokuwa ndani ya Afrika tuna Utaifa wetu, haiyumkiniki tunapoingia kwenye mashindani ya Kimataifa yahusuyo Nchi zilizo ndani ya wimbo wenu unaanza kwa kuwabariki washindani wenu kwanza kisha ndio ifuate Tanzani.

Hata basi ingekuwa vema beti la pili liwe la kwanza na kwanza liwe la pili.. yaani Mungu ibariki Tanzania kisha ndo ifuate Mungu ibariki Africa.
Mtunzi wa huu wimbo Ni muafrica na Africa Ni moja. Huu wimbo ni wakihistoria ndio maana mataifa kadhaa wanautumia. Hizo hisia za kuupinga zitoke kabisa ndani yetu
 
Ni jamaa kutoka Africa ya kusini miaka mingi sana iliyo pita


Sio, kweli, iweje wimbo wa taifa letu tutungiwe na mtu kutoka nje???.

Wimbo wa taifa ulitungwa na Sheikh Kaluta Amri Abeid kaluta, huyu alikuwa waziri wa sheria na baadaye akawa waziri wa utamaduni enzi za Mwalimu nyerere.

Uwanja wa Arusha (Amri Abeid memorial stadium) umepewa jina kwa heshima yake.

Tune ya huo wimbo ndio ilitoka South Africa; Tanzania, Zambia na South Africa zina tune moja za nyimbo zao za taifa.
 
Sio, kweli, iweje wimbo wa taifa letu tutungiwe na mtu kutoka nje???.

Wimbo wa taifa ulitungwa na Sheikh Kaluta Amri Abeid kaluta, huyu alikuwa waziri wa sheria na baadaye akawa waziri wa utamaduni enzi za Mwalimu nyerere.

Uwanja wa Arusha (Amri Abeid memorial stadium) umepewa jina kwa heshima yake.

Tune ya huo wimbo ndio ilitoka South Africa; Tanzania, Zambia na South Africa zina tune moja za nyimbo zao za taifa.
Yule sjui sontonga Enoch alifanya kazi gan
 
Kuongeza ubeti mmoja juu ya Muumba kwenye love song hakuifanyi love song kuwa national anthem.

Ukilinganisha maudhui ya huu wimbo na yale ya wimbo wa sasa wa taifa, utagundua kuwa kweli hii ni love song na mwingine ni national anthem!

Kuibadili hii love song kuwa national anthem, lazima hii love song ifanyiwe total overhaul.
Mapenzi juu ya nini?
 
Mkuu mokaze je, unafahamu Maneno yaliyo kwenye wimbo wa Taifa wa Zambia? Je unafahamu maneno yaliyo kwenye wimbo wa Taifa wa Afrika ya kusini? Kwa tune hiyo hiyo?

Unataka kunambia huyo mzee aliwatungia lia Zambia na akawatungia na Afrika ya kusini? Sabbu maneno ni yale yale ila yamebadirishwa majina tu ya Nchi na Lugha.
Au kwako wewe kutunga ni kutafsiri kutoka lugha fulani kwenda kiswahili.
Sio, kweli, iweje wimbo wa taifa letu tutungiwe na mtu kutoka nje???.

Wimbo wa taifa ulitungwa na Sheikh Kaluta Amri Abeid kaluta, huyu alikuwa waziri wa sheria na baadaye akawa waziri wa utamaduni enzi za Mwalimu nyerere.

Uwanja wa Arusha (Amri Abeid memorial stadium) umepewa jina kwa heshima yake.

Tune ya huo wimbo ndio ilitoka South Africa; Tanzania, Zambia na South Africa zina tune moja za nyimbo zao za taifa.
 
Back
Top Bottom