OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 457
- 773
67.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo-
Hii ni moja kati ya kitu cha kuangaliwa kwa ukaribu sana, ikumbuke kipindi tunatengeneza katiba hii kulikuwa na idadi ndogo ya wasomi, na hivyo katiba ikataka yeyote mwenye uwezo wa kusoma na kuandika kuwa mbunge ili kuwasemea wengi wasiojua kusoma.
Kama mtakumbuka maswala ya UPE nk ili kufanya watu wajue kusoma na kuandika.
Kwa ulimwengu wetu wa sasa ambao literacy rate imepanda kwa kiasi kikubwa ni upuuzi kukiendeleza kipande hiki cha sheria, na naweza kuto hoja zifuatazo.
Suala la kujua kusoma na kuandika lilikuwa kipindi kile ambacho waliokuwa wanajua kusoma na kuandika walikuwa wachache, kwa sasa tunao wengi hivyo ni vyema kubadili kipande hicho kama tulivyofanya marekebisho kwenye sheria nyingine.
Signed
OEDIPUS
- ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na kuandika katika Kiswahili au Kiingereza;
Hii ni moja kati ya kitu cha kuangaliwa kwa ukaribu sana, ikumbuke kipindi tunatengeneza katiba hii kulikuwa na idadi ndogo ya wasomi, na hivyo katiba ikataka yeyote mwenye uwezo wa kusoma na kuandika kuwa mbunge ili kuwasemea wengi wasiojua kusoma.
Kama mtakumbuka maswala ya UPE nk ili kufanya watu wajue kusoma na kuandika.
Kwa ulimwengu wetu wa sasa ambao literacy rate imepanda kwa kiasi kikubwa ni upuuzi kukiendeleza kipande hiki cha sheria, na naweza kuto hoja zifuatazo.
- Mbunge mbali na kuwawakilisha wananchi bungeni pia huhusika kwenye mchakato wa kupitisha miswada mbali mbali kuwa sheria. Hapo inahitaji walau utaalamu wa mambo hayo ambayo hayatokani na kujua kusoma na kuandika tu. Yaani unaweza kujua kusoma na kuandika lakini usiwe mzuri kwenye kujadili masuala ya kodi, uwekezaji, nk. Hapa kunaweza kupelekea sheria mbaya kuendelea kuwepo nchini
- Kwa sasa wao wahitimu wengi wa shahada mbalimbali ikiwemo sayansi ya siasa, ili kuepuka tatizo la ajira kwa vijana ni vyema kuwapa kipaumbele wenye elimu kwenye masuala ya kisisasa ili kutatua suala hilo lakinipia kuipa tija mijadala inayoweza kuwa inaendelea bungeni
Suala la kujua kusoma na kuandika lilikuwa kipindi kile ambacho waliokuwa wanajua kusoma na kuandika walikuwa wachache, kwa sasa tunao wengi hivyo ni vyema kubadili kipande hicho kama tulivyofanya marekebisho kwenye sheria nyingine.
Signed
OEDIPUS