Hoja juu ya hoja: Bunge kutoshirikiana na CAG si kuizika vita dhidi ya ufisadi iliyoasisiwa na inayosimamiwa na Rais Magufuli?

Kufuatia kuhojiwa kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Assad na Kamati ya Maadili ya Bunge kuhusu kauli yake kuhusu udhaifu wa Bunge,hatimaye leo Bunge limepitisha azimio la kutoshirikiana na CAG. Bunge limesikiliza,limejadili na kupigia kura azimio hilo lililopendekezwa na Kamati ya Maadili.

Kutoshirikiana na CAG ni kutofanya naye kazi kwa kipindi cha uhai wa azimio la leo. Kihistoria, Bunge limekuwa likiunda Kamati Teule za Bunge kufanya uchunguzi juu ya tuhuma za ufisadi Serikalini. Ilitokea hata kwenye masuala ya Escrow.

Inapoundwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza ufisadi, utaalamu na uthibitisho wa CAG hauepukiki. CAG Prof. Assad ni nguli katika masuala ya udhibiti na ukaguzi akisaidiana na wataalamu wabobezi waliosheheni kwenye ofisi yake. Anaachwaje pembeni katika utendaji wa Bunge linaloisimamia Serikali na kupitisha bajeti inayopaswa kulindwa dhidi ya ufisadi?

CAG huwasilisha Ripoti zake za ukaguzi kwa Rais. Baadaye,Ripoti hizo huwasilishwa na kujadiliwa Bungeni. Ndimo hasa unapoibuliwa na kuanikwa ufisadi ambao ni adui mkuu wa Rais Magufuli na Serikali yake. Ripoti za CAG huitaji ufafanuzi wake. Asiposhirikiana na Bunge si kukwamisha vita ya ufisadi na kukosa ufafanuzi wa kitaalamu.

CAG haepukiki katika shughuli za Bunge.Nitaelewa vinginevyo kama azimio la Bunge linalenga kutoshirikiana na Prof. Mussa Assad in his personal capacity na si ofisi ya CAG. Kama ni zuio la kutoshirikiana na Prof. Assad binafsi,Bunge litakuwa limewasilisha ombi kwa Rais Magufuli kuteua CAG mpya.
Ivi statement ni kutoshirikiana na ofisi nzima ya CAG au ni kutoshirikiana na CAG Prof Mussa Assad? If the second is true then hiyo position si ina kaimu CAG?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie mbona hamueleweki mnaongea nini? Mko upande gani ?
Wengi hawaangalii angle hii.Waliosoma administration and management wanaelewa kosa la Assad ila Wafia chama hawaelew lolote lile.

We think too small, like the frog at the bottom of the well. He thinks the sky is only as big as the top of the well. If he surfaced, he would have an entirely different view.
Petro E. Mselewa unapojadili hili jambo ondoa muhemuko wa kisiasa. Kwa watumishi wa umma, hasa viongozi wanaelewa maana ya viapo vya maadili na utiifu. Hicho alichokifanya Prof Assad siyo sahihi kabisa, tena ni kupungukiwa busara.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie mbona hamueleweki mnaongea nini? Mko upande gani ?

Sent using Jamii Forums mobile app
We unataka upande au unataka FACTS?

We think too small, like the frog at the bottom of the well. He thinks the sky is only as big as the top of the well. If he surfaced, he would have an entirely different view.
 
Siwa elewi hata kidogo kwamba Asad waitaka hata kwenye udhaifu aseme ni ujasiri. ?
Kusema kuna udhaifu kwenye bunge ni kosa kubwa kiasi hicho? Methinks it is just a smokescreen. Kosa la Prof. Assad ni ujasiri wake, kujiamini na integrity yake. Nothing more nothing less.

USOGA WI KUA KATI MWINA NSONGOO
 
Kufuatia kuhojiwa kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Assad na Kamati ya Maadili ya Bunge kuhusu kauli yake kuhusu udhaifu wa Bunge,hatimaye leo Bunge limepitisha azimio la kutoshirikiana na CAG. Bunge limesikiliza,limejadili na kupigia kura azimio hilo lililopendekezwa na Kamati ya Maadili.

Kutoshirikiana na CAG ni kutofanya naye kazi kwa kipindi cha uhai wa azimio la leo. Kihistoria, Bunge limekuwa likiunda Kamati Teule za Bunge kufanya uchunguzi juu ya tuhuma za ufisadi Serikalini. Ilitokea hata kwenye masuala ya Escrow.

Inapoundwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza ufisadi, utaalamu na uthibitisho wa CAG hauepukiki. CAG Prof. Assad ni nguli katika masuala ya udhibiti na ukaguzi akisaidiana na wataalamu wabobezi waliosheheni kwenye ofisi yake. Anaachwaje pembeni katika utendaji wa Bunge linaloisimamia Serikali na kupitisha bajeti inayopaswa kulindwa dhidi ya ufisadi?

CAG huwasilisha Ripoti zake za ukaguzi kwa Rais. Baadaye,Ripoti hizo huwasilishwa na kujadiliwa Bungeni. Ndimo hasa unapoibuliwa na kuanikwa ufisadi ambao ni adui mkuu wa Rais Magufuli na Serikali yake. Ripoti za CAG huitaji ufafanuzi wake. Asiposhirikiana na Bunge si kukwamisha vita ya ufisadi na kukosa ufafanuzi wa kitaalamu.

CAG haepukiki katika shughuli za Bunge.Nitaelewa vinginevyo kama azimio la Bunge linalenga kutoshirikiana na Prof. Mussa Assad in his personal capacity na si ofisi ya CAG. Kama ni zuio la kutoshirikiana na Prof. Assad binafsi,Bunge litakuwa limewasilisha ombi kwa Rais Magufuli kuteua CAG mpya.
Ndo kusema hakuna, na hakijawahi kuwa navita kama hiyo. Ni drama tu tuna chezewa.
Imefikiatu sasa imeonyeshwa live kuwa hakuna kitu kama hicho.
 
Sio mbaya madamu tumeshajua BUNGE NI DHAIFU.
Wewe kama msomi,kipimo chako kinasemaje?,halafu hiyo yote maana yake ni kuwa hatutajua tena mapato,matumizi na upotevu wa pesa zetu?Tunakubaliananayo?
 
Yaani kauli tu isiyobandua nyama inatugharimu?na tuliowapa kutusimamia wanatuona sisi vichaa?
Mbona hawaazimii mambo mazito ambayo serikali haiyatekelezi kama kutoa 100% ya fedha za maendeleo,badala yake zinapopotea ndiyo tunajifanya tumekasirikia kauli tu?
 
Masikin weeeeee, kwa hiyo mlitaka aseme bunge lina changamoto?
Wengi hawaangalii angle hii.Waliosoma administration and management wanaelewa kosa la Assad ila Wafia chama hawaelew lolote lile.

We think too small, like the frog at the bottom of the well. He thinks the sky is only as big as the top of the well. If he surfaced, he would have an entirely different view.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengi hawaangalii angle hii.Waliosoma administration and management wanaelewa kosa la Assad ila Wafia chama hawaelew lolote lile.

We think too small, like the frog at the bottom of the well. He thinks the sky is only as big as the top of the well. If he surfaced, he would have an entirely different view.
Wewe mfia CCM tu!!!
 
Wanaisikia sauti iliyotokana na mapungufu yao,lakini hawasimam8 na wananchi kuhoji ziliko 1.5 Trillion!,Hawawezi kuwa makini.
 
Bora tutamkumbuka PIERE kuliko viongozi wa huu muhimili katika miaka hii.
 
Kufuatia kuhojiwa kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Assad na Kamati ya Maadili ya Bunge kuhusu kauli yake kuhusu udhaifu wa Bunge,hatimaye leo Bunge limepitisha azimio la kutoshirikiana na CAG. Bunge limesikiliza,limejadili na kupigia kura azimio hilo lililopendekezwa na Kamati ya Maadili.

Kutoshirikiana na CAG ni kutofanya naye kazi kwa kipindi cha uhai wa azimio la leo. Kihistoria, Bunge limekuwa likiunda Kamati Teule za Bunge kufanya uchunguzi juu ya tuhuma za ufisadi Serikalini. Ilitokea hata kwenye masuala ya Escrow.

Inapoundwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza ufisadi, utaalamu na uthibitisho wa CAG hauepukiki. CAG Prof. Assad ni nguli katika masuala ya udhibiti na ukaguzi akisaidiana na wataalamu wabobezi waliosheheni kwenye ofisi yake. Anaachwaje pembeni katika utendaji wa Bunge linaloisimamia Serikali na kupitisha bajeti inayopaswa kulindwa dhidi ya ufisadi?

CAG huwasilisha Ripoti zake za ukaguzi kwa Rais. Baadaye,Ripoti hizo huwasilishwa na kujadiliwa Bungeni. Ndimo hasa unapoibuliwa na kuanikwa ufisadi ambao ni adui mkuu wa Rais Magufuli na Serikali yake. Ripoti za CAG huitaji ufafanuzi wake. Asiposhirikiana na Bunge si kukwamisha vita ya ufisadi na kukosa ufafanuzi wa kitaalamu.

CAG haepukiki katika shughuli za Bunge.Nitaelewa vinginevyo kama azimio la Bunge linalenga kutoshirikiana na Prof. Mussa Assad in his personal capacity na si ofisi ya CAG. Kama ni zuio la kutoshirikiana na Prof. Assad binafsi,Bunge litakuwa limewasilisha ombi kwa Rais Magufuli kuteua CAG mpya.
Nani kakuambia jiwe anapambana na ufisadi wakati ufisadi mkubwa wa kihistoria umefanywa chini ya usimamizi wake na ndio chanzo cha haya yote
 
Bunge lilipoteza maana na kazi zake toka awali nazani ukweli tutaujua behind the scene!! CAG-Msema ukweli ni mpenzi wa Mungu....
 
Back
Top Bottom