Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,348
- 26,144
Katika mchango wake wa leo katika Bunge Maalum la Katiba,Mjumbe Mwigulu Nchemba ameonyesha hofu yake ya kuendelea na majadiliano kwa siku themanini na nne (84) na mwishowe kushindwa kupata theluthi mbili za Tanzania Bara na theluthi mbili za Tanzania Visiwani ili kupitisha Rasimu tayari kwa kupigiwa kura ya maoni na watanzania. Mwigulu Nchemba amemtaka Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba afanye hesabu na kujiridhisha juu ya kupatikana kwa takwa hilo la Kikatiba.
Hii ni hofu kuu.Ni hofu isiyo na chembe ya shaka kuwa wapo Wajumbe wameshaona dalili za kulazimisha visivyolazimishwa. Hofu inayolenga kuponya fedha za walipakodi wa nchi hii ambazo zaweza kutafunwa kwa siku 84 bila ya kupelekewa Rasimu ya Katiba kuipigia kura. Ni hofu ya wengi. Wachambuzi wa kisiasa wanaiona kauli ya Mwigulu Nchemba kama kuanza kushtuka kwa CCM na kutaka kurejea 'kwenye njia sahihi' ya kupata Katiba mpya.
Kama Mwigulu Nchemba,kama Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara na Naibu Waziri wa Fedha ameshindwa hadi leo kujua kama wana theluthi mbili za pande mbili za Muungano,itoshe kuaminika kuwa CCM na wafuasi wao hawana uhakika wa kupitisha Rasimu iliyo Bunge Maalum la Katiba.Mwenyekiti Sitta anapaswa kuufanyia kazi ushauri wa Mwigulu Nchemba AS SOON AS POSSIBLE (ASAP). Binafsi naamini,takwa la theluthi mbili halitafikiwa kwa hali ilivyo sasa na hivyo Bunge Maalum la Katiba lapaswa kusitishwa hima.
Hii ni hofu kuu.Ni hofu isiyo na chembe ya shaka kuwa wapo Wajumbe wameshaona dalili za kulazimisha visivyolazimishwa. Hofu inayolenga kuponya fedha za walipakodi wa nchi hii ambazo zaweza kutafunwa kwa siku 84 bila ya kupelekewa Rasimu ya Katiba kuipigia kura. Ni hofu ya wengi. Wachambuzi wa kisiasa wanaiona kauli ya Mwigulu Nchemba kama kuanza kushtuka kwa CCM na kutaka kurejea 'kwenye njia sahihi' ya kupata Katiba mpya.
Kama Mwigulu Nchemba,kama Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara na Naibu Waziri wa Fedha ameshindwa hadi leo kujua kama wana theluthi mbili za pande mbili za Muungano,itoshe kuaminika kuwa CCM na wafuasi wao hawana uhakika wa kupitisha Rasimu iliyo Bunge Maalum la Katiba.Mwenyekiti Sitta anapaswa kuufanyia kazi ushauri wa Mwigulu Nchemba AS SOON AS POSSIBLE (ASAP). Binafsi naamini,takwa la theluthi mbili halitafikiwa kwa hali ilivyo sasa na hivyo Bunge Maalum la Katiba lapaswa kusitishwa hima.
Last edited by a moderator: