Hofu hii ni ya nini?

Hofu hii ni ya nini?

vukani

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2009
Posts
244
Reaction score
166
Wana JF,

Jana nilikuwa na Dine na rafiki yangu mmoja, binti wa Kijerumani katika mghahawa mmoja marufu ulioko maeneo ya Masaki..
Yeye, yuko hapa nchini kama Expert akiwa anafanya kazi katika sekta ya Utalii.

Wakati tukiendelea kula huku tukipiga soga, mara wakaingia Wachina kama kumi hivi wakataka waandaliwe meza ya pamoja, lakini baada ya kuingia hao Wachina, atmosphere ya pale ndani yote ilibadilika kwani karibu wateja wote waliokuwepo pale ndani ambao mostly walikuwa ni wazungu waligeuka kuwatazama.

Wachina wale walikuwa wakiongea kwa kikwao tena kwa sauti kiasi kwamba utulivu uliokuwepo pale mghahawani ulitoweka ghafla.

Yule rafiki yangu ambaye muda wote alikuwa amewatumbulia macho, alinigeukia na kuniuliza, "Ninashangazwa sana na serikali yenu kuwakumbatia Wachina kiasi hiki, mnadhani watasaidia kuinua uchumi wenu"

Kwa kifupi nilimjibu kuwa huu ni utandawazi na serikali yetu haina mkataba na taifa Fulani kuwa ndilo lenye mamlaka ya kuingia na kuishi au kufanya kazi hapa nchini, kwa hiyo yeyote yule mwenye kutaka kuja kuwekeza hapa nchini anaruhusiwa ili mradi asivunje sheria a afuate taratibu za kuingia hapa nchini basi.

"Nadhani huko sahihi", alisema binti wa Kijerumani, "Unajua sisi inapotokea tunataka ku renew working permit zetu, kunakuwa na usumbufu mkubwa sana, ukilinganisha na hawa Wachina, wao wapo kila mahali na wanafanya biashara ambazo zilipaswa kufanya na nyie lakini hawabughuziwi kama tunavyobughuziwa sisi wazungu, imefikia mahali sasa tunahisi kubaguliwa waziwazi tofauti na hawa Wachina"

"Wewe unadhani tatizo ni nini?" Nilimuuliza.

"Sikiliza, hawa wachina ni wajanja sana wameleta miradi ya ujenzi wa barabara kama danganya toto, na katika miradi hiyo wamejipenyeza kwa kisisngizio cha expert na baada ya mradi kuisha wanendelea kuishi hapa nchini kwa kisingizio kingine cha wawekezaji ambapo hufanya shughuli ambazo zilipaswa kufanywa na nyie wazawa, na wamejipenyeza katika maeneo ya uswahilini na kuishi na wenyeji kwa ushirikiano na wamejifunza Kiswahili kiasi kwamba wamegeuka sehemu ya jamii ya chini kabisa, lakini baadae hawa watu wata take over kila kitu na kuwaacha mkishangaa, sio watu hawa jiangalieni"

"Ok, kwa nini na nyie msifanye hivyo" nilimshauri,

Haiwezekani, unajua sisi tuna utamaduni tofauti na nyie, lakini Wachina huenda utamaduni wao hauna tofauti kubwa na wa kwenu na ndio maana wameweza ku corp na society yenu bila shaka" alinijibu……….

Nilishusha pumzi...........

Kwa kifupi mjadala ulikuwa ni mzito na mrefu kiasi kwamba ulichukua sehemu kubwa ya mazungumzo yetu…….any way labda nilichotaka kuwauliza wana JF,ni Je kuna haja ya watanzania kuhofia ujio wa hawa wachina, au wamekuja kusukuma mbele gurudumu la maendeleo?…………………

 
Si rahisi kufanya fina judgement
Sometimes yaweza kuwa tatizo kwa uwepo wao
tatizo hasa maana ya expert imepotoshwa na haifanyiwi kazi kwa maana yake halisi.
siyo wachina tu bali ni suala la ujio wa wageni tz japo vigezo vya being an expert wengi wao hawana.
 
just wait till we have our own china town led by some chinese mafia
 
angalia tena post zako............ zinaonekana kama copy and paste............. nina wasiwasi si zako vukani........... labda uthibitishe..................

hata kama ni mwanhabari.............. hebu jaribu kuzi-editkidogo zikae kwa standard ya JF sio kuzibwaga hapa kama ulivyozikopi huko.............. unasimulia utadhani ....................
 
Hao wachina na huyo mjerumani wako wote wamekuja kuchuma kwenye shamba la bibi, as simple as that.
 
mhhh huyo mjerumani anaijua historia ya ujerumani japo kidogo kama mm ninavyoifahamu??

Mfano mdogo tu imechukua miaka mingapi kuona mwanamichezo wa kiafrika akiwakilisha ujeruamani kimataifa.???

Kisaikolojia
huyo anayejiita au aliyepachikwa u-expert akiwa kwao ndo waleeee wanaowatemea wageni mate.

Otherwise
Scenario nyingine ya hayo mazungumzo ingeweza kuwa mzawa kuwaponda wachina na kuwafgilia wajerumani( wazungu).mhh itakuwa kichekesho

Vyovyote vile
Kama alivyosema abdul wote wanakuja kuganga njaa kwenye shamba la bibi.
 
Vyovyote vile
Kama alivyosema abdul wote wanakuja kuganga njaa kwenye shamba la bibi.

Naturally, ni hivo mkulu. Kuna wahindi wengi wanachuma bongo wanaenda kula Canada na UK. Sasa sioni cha ajabu kwamba tunashangaa Wachina wanapokuja na kufanya the same.
 
angalia tena post zako............ zinaonekana kama copy and paste............. nina wasiwasi si zako vukani........... labda uthibitishe..................

hata kama ni mwanhabari.............. hebu jaribu kuzi-editkidogo zikae kwa standard ya JF sio kuzibwaga hapa kama ulivyozikopi huko.............. unasimulia utadhani ....................

Kaaazi kweli kweli........labda wewe ndo uthibitishe kuwa nazikopi wapi na kuzipest hapa JF...

Naona hukutumia busara kunishambulia waziwazi.
Mimi sio mwanahabari ila napenda sana kuandika.
Lakini kama makala zangu zimeonekana kuwakera wana JF na wewe ukiwa ni mmoja wapo basi nitajitoa humu. maana naona nabaguliwa wazi wazi, tena kuna wakati hata maoni yangu huondolewa bila kuambiwa sababu.

Labda JF ina wenyewe...............
 
Binadamu yoyote hutulia kwao kama mambo yamemnyookea....hawa wageni wote hawan opportunities huko makwao..awe mjerumani au mchina....sidhani kama angekuwa na well paying job kwao nagekuja kuwa expert huko kwetu....mimi naamini ni madiplomats tu wapo huku kwetu kwa merit..others I doubt...

Sisi wenyewe tumekimbia ugumu vijijini kwetu sasa tunalalamika oooh Dar foleni.....hakuna opportunities kule...tumewakimbiza Wazaramo kwao sasa tuntaka kulaumu Wachina...
 
Back
Top Bottom