Hizi tuhuma kwa Samwel Sita ni za kweli?

kama angekua fisadi angelamba ile 10% waliyotaka kumpa kimya kimya enzi hizo kwa ajili ya moja ya miradi ya wizara yake,lakini mbona baada ya kushawishiwa hivyo tena akiwa huko huko ulaya,alichofanya ni kumpigia simu mwalimu nyerere na kumwambia hawa jamaa wanataka kunipa 10%,mwalimu akamwambia ichukue then uilete serikalini isaidie kununua vitabu vya shule,na sitta akatii agizo hilo la bosi wake,sasa huo ndio ufisadi?
 
Tadhali Kama unajua juu ya tuhuma hizi tufafanulie zaidi. Binafsi nashindwa kuamini kuwa Nyerere angeishia kumpa kazi nyingine katika serikali. Sitta ni mmoja wa watu waliofanya kazi kwa uadilifu sana.
 
Lakini asavali tunaiona barabara,kuna wengine walileta Richmond na mpaka sasa tatizo lipo palepale na hali inazidi kuwa mbaya kwani umeme uko juu zaidi kwa ajili ya kulipia matozo yanayoenda kwa haohao waliotuingiza zizi la simba
 
Aliyewapeleka Simba Brazil ni nani?...
Kwa fedha zipi?
 
kwani yeye anaonaje ni fisadi au sio fisadi, lakini ukizaliwa baba fisadi na wewe ni fisadi , Sitta ni mtoto wa CCM awezi sita kushiriki ufisadi
 

"Aliyekuwa spika wa bunge ambae alimaliza muda wake Bwana Samwel Sita na ambae anajinadi kupambana na ufisadi nae inasadikika ni mmoja wa mafisadi ambao walipopata nafasi hawakusita kukwapua mlungula katika kandarasi mbalimbali.

Alipokuwa waziri wa Mawasiliano na Ujenzi katika serikali ya awamu ya kwanza alihusika na ulaji rushwa katika kandarasi mbalimbali za ujenzi
Mojawapo ni ujenzi wa barabara ya Morogoro - Dodoma. Huyu bwana aliafukuzwa uwaziri na Mwalimu Nyerere baada ya kuchukua rushwa ya Ma-trector ambayo yalikuwa na harrow, planter na combined harvester kutoka kampuni ya ujenzi ya Brazil ambayo ilipewa kandarasi ya kujenga barabara hiyo. Tujuzeni wenye habari zaidi ktk hili.
huu ni udaku
 
unamhukumu mtoa mada kwa kosa gani?, ameleta mada ili mwenye data(+ve or -ve) azilete ili kuweka kumbukumbu sawa, wewe waleta habari ya kunyooosheana vidole?!, gt watia aibu but endelea na moyo wako wa kumtetea 6.

inaonekana wandishi hana data kamili..........mbona kikwete ni rai wako na ni fisadi aliyetajwa na ni mlindaji wa mafisadi lakini hamsemi tumfanye nini............sasa km mafisadi kibao wapo tu barabarani na watz tumekaa kimya hatufanyi kitu kuna haja gani ya kuendelea tu kuwataja?............
 
Wewe mafisadi unawajua, leo Sitta katoka wapi na hiyo barabara iliyojengwa na waBrazil toka 1982 ni kweli alikuwa CDA na akaenda uwekezaji kabla ya Naiko lakini si fisadi kama wakina Richmond
lete habari zenye uhakika tuchangia, Samweli keshasema hagombei
Nimekupata kaka
 
niny mnatumwa ili kuharibu thinking za watu ili kupotosha ufahamu na ukwel wa mambo ili wasafi walingane na wachafu(sitta=lowassa) ili kuwapotosha wananchi_utalaaniwa kwa zambi hiyo maisha yako na vizaz vyako
 
sasa kwani kula rushwa ni ufisadi, rushwa ni rushwa na ufisadi ni ufisadi.
 

"Aliyekuwa spika wa bunge ambae alimaliza muda wake Bwana Samwel Sita na ambae anajinadi kupambana na ufisadi nae inasadikika ni mmoja wa mafisadi ambao walipopata nafasi hawakusita kukwapua mlungula katika kandarasi mbalimbali.

Alipokuwa waziri wa Mawasiliano na Ujenzi katika serikali ya awamu ya kwanza alihusika na ulaji rushwa katika kandarasi mbalimbali za ujenzi
Mojawapo ni ujenzi wa barabara ya Morogoro - Dodoma. Huyu bwana aliafukuzwa uwaziri na Mwalimu Nyerere baada ya kuchukua rushwa ya Ma-trector ambayo yalikuwa na harrow, planter na combined harvester kutoka kampuni ya ujenzi ya Brazil ambayo ilipewa kandarasi ya kujenga barabara hiyo. Tujuzeni wenye habari zaidi ktk hili.

wewe ndo umeleta habari then unataka ujuzwe nini?? acha kutumika kwa bei poa, lete ushahidi hapa jamvini
 
Unamhukumu mtoa mada kwa kosa gani?, ameleta mada ili mwenye data(+ve or -ve) azilete ili kuweka kumbukumbu sawa, wewe waleta habari ya kunyooosheana vidole?!, GT watia aibu but endelea na moyo wako wa kumtetea 6.

sizani kama tutafika kama tukianza kukumbushana mambo ya 1982, zipo changamoto nyingi sana mbele yetu akili zetu tuzielekeze mbele na si nyuma.
 
Wewe mafisadi unawajua, leo Sitta katoka wapi na hiyo barabara iliyojengwa na waBrazil toka 1982 ni kweli alikuwa CDA na akaenda uwekezaji kabla ya Naiko lakini si fisadi kama wakina Richmond
lete habari zenye uhakika tuchangia, Samweli keshasema hagombei

Nilisoma sehemu.Samweli amenukuliwa akisema kuwa Urais unamfuata yeye lakini yeye hana habari nao.:lol:
 
1982 utalinganisha na ufisadi wa sasa kweli?



ufisadi ni ufisadi tu juzi, jana, leo na hata kesho, ukikutana naye muulize kwanini kulikuwa na maslahi gani kwenye muswada wa sheria ya famasi???? Mjibu yoyote atakayokupa tujuze, hapo tutajua kama ni fisadi au la, ila fisadi ni fisadi, juzi, jana, leo na hata keshooooooooooooooooooooooooo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom