Hizi tabia zikome huku MMU haraka

Hizi tabia zikome huku MMU haraka

kuna tabia humu zinakera sana, zikome haraka sana.

  1. tabia ya kila ukiletwa uzi na mwanaume kuhusu mke wake wanaume karibu wote wanamshauri mwenzao amwache mke wake, hiyo tabia mkome mkome, hamjui upande wa pili upoje wala kama yaliyosemwa ni ya kweli au mtu anatafuta sababu tu nyie mnapigilia msumari wa moto.

    Acheni hiyo tabia kabisa, humu tumo na fake id unaweza kuta unaropoka ropoka kumbe unavunja ndoa ya dada ako, shangazi yako na acheni kabisa hii tabia.

  2. tabia ya mtu anaamua tu kuja kudhalilisha wanawake humu nayo ikome haraka, palipo na mwanaume lazima kuna mwanamke.

    Sasa iweje kila siku wanaume muishi kwa kuwakashifu wanawake etii kisa tu mtu kakunyima papuchi basi unakuja kutukana wanawake woteee duniani.

    Hii tabia ikome haraka.
  3. tabia ya watoto wadogo kuingilia mada za watu wazima ikome, subirini ikifika wakati wako utachangia, acha kujikomaza, ka jogoo anayejifunza kuwika, anawika hata saa 7 mchana.

  4. mwisho: Tabia ya mtu kuja pm wakati hujui amekuja pm kufanya nini ikome, au mtu unakuja pm kuleta ubabe nayo ikome ubabe peleka ulingoni.

    Pm ni sehemu ya kuongea faragha na jambo la msingi, sio kuja kujikanyaga kanyaga na kumaliziana charge over.

    angalizo: Kama nimekukera kuwa mpole usije na matusi hapa.

    [/size][/color]


  1. meseji imefikia walengwa aisee
 
Hahaha thatha tutakuwa na adabuu. Na tabia ya kutafuta humu viburudisho nao wakomeee!
 
Ubabe wa kumnyima mwenzio papuchi hiyo tabia nayo ikome

Kwani ukiomba lazima upewe, ni karanga hizi??????

Noted, Apology Lady nanyi wanawake siku hizi hamjambo kwa kuwasema waume zenuu....!! Tujiangalie sote pls

Mimi sipendi tabia yenu yakupenda wanawake tuachike, muwe mnawashauri wenzenu vizuri.

Hahaha hiyo number 4. Sasa ya PM si unaniambia huko huko yanaisha? Kama mambo yenyewe ndiyo haya, siendi tena PM kwa mtu kuanzia sasa.

Hahahaha!!!!!!!!! sasa mtu anakuja pm kuleta ubabe huo si ukorofi??

[5*] na wanaume wanaowadanganya wanaume wenzao wasiwape wapenzi wao pesa mkome tena mkome kabisa... uchoyo wenu uishie huko huko.

Hii niliisahau, watakutoa macho wallah!!!! wanaume wakitziiiiiiiii.

pm ni sehemu ya kuongea faragha!!! mi hapo tu ndo umenikosha, ngoja nimalizie hapa nije....

Aiseee!!!

Kuna watu wameajiriwa ili kukera wengine.

Tena wanakera vizuri.

Hilo la watoto kuingilia mada za wakubwa nadhani mods waongeze jukwaa lao wakajiachie pia

Vitoto vinakera sana, vitafutiwe tu jukwaa.

Na. Nyie acheni kuleta thread za mambo yenu

Ndio kazi la hili jukwaa.

Watakuwa wamekoma!!!!

Wakome hasaaaa.

Mmmh !! hii nimeipenda..

[*]Tabia ya watoto wadogo kuingilia mada za watu wazima ikome, subirini ikifika wakati wako utachangia, acha kujikomaza, ka jogoo anayejifunza kuwika, anawika hata saa 7 mchana.


Hahahahaha!!!!!!!!!

Aisee
Leo umependeza eeh:A S 41:

Sanaeeee??????
 
Nataka siku moja nikuanzishie tifu mpaka tupigwe ban, maana sijapigwa ban muda mrefu sana.
,Khaa!!! Yaani ban utaman wewe ila unataka namim nipate heee!!!

Mim niache niendelee kuongeza siku za kuishi kupitia jf.
 
[5*] na wanaume wanaowadanganya wanaume wenzao wasiwape wapenzi wao pesa mkome tena mkome kabisa... uchoyo wenu uishie huko huko.

Hii tabia ya kuwafundisha wanawake wenzenu kuwachuna wanaume ikome mara moja
 
Back
Top Bottom