Sungurampole
JF-Expert Member
- Nov 17, 2007
- 984
- 205
Watanzania tufikeni mahali tuwe wa kweli na tumuogope Mungu kudanganya peupe. Binafsi yangu nimeona noti nyingi niliona noti ya brown ya shilingi 5, nimeona 100 ya Mmasai mpaka noti za sasa. Sijawahi kuona noti mbovu kama hizi. Ukisikiliza kila mmoja analalamikia ubora wa noti hizi. Hii si mbaya sana, mbaya zaidi ni majibu ya Benki Kuu. Wanasema tatizo ni jinsi tunavyozitunza kama vile hizi noti za kwanza kuwa nazo, haya ni maneno ya kihuni. Wanakuwa wakali kutetea uozo uliofanyika ambao huhitaji kuwa mtaalam kujua zimechakachuliwa. Sijawahi kuona noti inafumuka naiona sasa. Wakati zinatoka walituambia hizi zimetengenezwa kwa teknolojia ya kisasa zaidi na hazitaweza kugushiwa. Mara tukaanza kusikia watu wanalia kwani ghafla feki zilizagaa kila mahali. Wanageuka wanatuasa kusema ili usibambikiwe feki chunguza special features moja iangalie noti kwenye jua utaziona, au hata unuse. Hapa unachukia na kutaka kupasuka kwani unaambia ufanye kisichowezekana- yaani umelipwa millioni yako pale kariakoo utoke dukani ukae pale nchi uanzee kuangalia juani noti mojamoja ndiyo ukimaliza umpe bidhaa mteja huyu. Jamani hivi viongozi wetu hamlioni hili? Mmeshindwa kabisa kuona kuwa tumeibiwa katika tenda hii na hivyo tuachane nazo, tuzibadili noti hizi na safari tuwe makini? ningeongeza kusema tuwawajibishe waliohusika lakini wewe na mimi tunajua hiyo ni ndoto ya mchana. All in all these are the worst notes we have ever had in Tanzania.