Hizi ndoto zinanitesa sana jamani

Hizi ndoto zinanitesa sana jamani

Kuna mambo ambayo yanakutatiza lakini huna maarifa ya kutatua.

Roho wa ndoto anakuonyeaha kwamba jiandae sasa au lah unatumia sana mbeleni.

Ni tatizo lipi? Na ujiandae namna gani? hapo ndipo mtihani ulipo. mwabudu Mungu sana ili akufunulie zaidi uweze kujiandaa!!

Majority huwa ni mitihani ya kimaisha..
Yaweza kuwa maisha yako ya ndoa, kazi yako inakwenda kuisha, Biashara yako inakwenda kuporomoka nk
Dooh!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nina ndoto tatu ambazo hujirudiarudia.

1. Naota niko safari lakini hata kama ni safari fupi sifiki ninakoenda.

2. Kuna mlima mmoja mrefu huko kwetu basi huu mlima huwa naota nimeuona maeneo tofautitofauti tena mbali kabisa na mahala ulipo. Huu mlima hata sijawahi kuusogelea karibu lkn ndoto sasa.

3. Naota niko zangu toilet najisaidia haja kubwa lkn cha ajabu simalizi hata saa nzima namaliza huko.

Hizi ndoto zimeshajirudia zaidi ya mara kumi kila mmoja mpaka nimeshazoea tu kuziota.

Hata za kuwa shule naota sana. Nashindwa kuelewa ni kawaida ndoto hizohizo kujirudia mara kwa mara au kuna maana zake?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hapo sijui hali yako kiuchumi ila kiukweli kiimani hizi sio ndoto salama kabisaa katika maisha yako kiutafutaji yaani hapo malaika mlinzi anajaribu kuwakumbusha,unarudishwa nyuma kimaendeleo mwambie namtoa mada
 
Ndoto za mashuleni si nzuri,nyingi ni ishala ya kuanguka ,kuwa sehemu si sahihi katika maisha yako,mfumo wa maisha yako kutokwenda vizuri,mahali ulipo hausitahili kuwepo,umekwama mahari fulani katika maisha.
Mfano ulikuwa vizuri katika masomo na hatimaye mtihani wa mwisho unapata matokeo ya chini tofauti na matalajio yako.

Kufanya kazi ambayo hukuitarajia katika maisha yako,kuishi ndoto ambazo si zako,ulitaka uishi maisha fulani ila matokeo yako unaishi maisha ambayo hukuyapenda hata tangu hujafikiria kujitegemea kiuchumi.Mambo yako kutokwenda katika mtililiko unao faa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee hata mimi huwa naota hizi ndoto, ila mie ni tofauti na wewe kidogo,

Mie kidato cha 6 nilizingua, kipindi nipo kidato cha 5 mwishoni nilitia mimba mabinti fulani wawili(mmoja yupo kkoo, mwingine kinondoni) kipindi hicho nipo hostel kalita magomeni, natwanga shule Azania pale, mmoja mimba yake iliharibika km miezi miwili hivi, nikabaki na kasheshe huku, so 6 sikuisoma kwa raha wala amani kabisa mzee, sababu kidogo ile familia ilikuwa mtihani, mara binti wamfukuze, anipigie katimuliwa yupo mtaani hiyo saa 6/7 usiku,mara wanipigie simu za mikwara, mara nipigiwe simu wako njiani kwenda kwetu, uzuri bibie alikuwa hawapeleki mtaani kabisa, anazuga kapasahau! Iliwachukua kama miezi mi4/5 kupafahamu maskani, hapo nina km wiki 2 mbele nipoge pepa la mwisho, nakumbuka mpaka namaliza pepa, niliogopa hata kwenda home, ilibidi nijifungie kinondoni kwao rafiki yangu(wa damu) wiki kama 3 hivi mpaka mama aliponipigia simu kuwa nirejee tu nyumbani, kifupi sikusoma kwa amani km sio kusoma kabisa form 6, waliobahatika vibaya kupata majanga kama haya wanaelewa.(story ni ndefu kidogo) baada ya pepa km wiki 3 mbele ndio mwanangu akazaliwa.
Baada ya matokeo kuwa hovyo moyo ukafa ganzi kabisa na kitu shule nikaombwa nikasome hata diploma nikagoma kabisa nikaamua nifanye biashara zangu tu mtaani, baada ya mwaka kidogo nikatulia ile hamu ya school ikarudi tena nikaenda pale DIT kwa matokeo ya form 4, kupiga telecom nikasoma semister ya kwanza fresh! Ya pili nafsi ikaanza unyonge nikitizama wenzangu walipo na mie nilipo , nikajikuta semister ya pili ada yake nafanyia mambo mengine nikawa naenda kama ushahidi tu pale, nikapiga pepa nafsi ikagoma kabisa kurudi kusoma.

Na ubaya ama uzuri class nilikuwa vizuri, toka niko mdogo(primary) o level nilikuwa nikiishi najua mimi ni engineer wa baadae. Jamaa zangu wengi sasa ni ma engineer.

Hii kitu huwa naota saana, mara nyingi naota nipo zangu napiga pepa ya namba nacheza na zile namba km sina akili nzuri, au ndio hivyo nipo class, ama napiga pepa halafu vitu vinashuka tu easy, nacheki matokeo na vitu kama hivyo.
Ni ndoto ambazo naziota mnoo.
Sometimes natamani nirudi kusoma hata nikamilishe tu ndoto zangu, hata kama sintakifanyia kazi kile nitakachosomea, naimani nafsi itatulia, kama sio mwaka huu hata mwakani nikishafaniliwa kuoa inshaallah nitajaribu kusoma tena.

Sasa sijui kwa wewe ndoto hizo zinachagizwa na nini kwa kweli.
1. Naota ghafla naingia kwenye chumba cha mitihani ya mwisho alafu hakuna nilichosema

2. Siku nyingine naota nimechelewa kuingia chumba cha mtihani muda unaisha sijajaza answer sheet kabisa na nakuwa nahangaika kwelikweli

3. Mara naota kuna mtihani nafika shule nimechelewa nafika ubaoni kujua jina langu liko room gani inanichukua muda mrefu kugundua, ile nafika chumba cha mtihani zimebaki dk chache muda wa mtihani kuisha, najikuta naingiwa na stress kisha nashindwa kujibu swali hats moja kisha nashtuka ndotoni nikiwa tafrani

NOTE: Nimepita pita shule mpaka elimu ya chuo na huko kote nilikuwa napita bila shida yeyote, msaada wakuu maana nakosa amani kabisa na zimekuwa zikijirudia mara kwa mara.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hizo ndoto zimewahi kunitokea 2017 sana tu, nilikuwa sina time ya kurudi kusoma ila ndoto zilipoanza ah kusoma kulikuja automatically niliingia class baada ya hapo sijawahi ota tena hizo ndoto..
Kwa ushauri rudini mkasome mkamilishe ndoto zenu
 
2.Ndoto za elimu hasa shule za msingi
mambo ya kuzingatia ulikuwa na Nani? , mnafanya nini?, somo au mtihani gani ulikushinda?
Maana zake ni

.Jambo ulilolikusudia kufanya na kiwango cha maandalizi kifikra etc haviendani.

.kuna kitu umepungukiwa kwenye msingi WA kufikiri, misingi ya kufikiri imeharibika.

.kuna jambo linalokusumbua Sasa limekosa msingi mzuri wa kufikiri.

. Kupungukiwa maarifa, maono, ufahamu na fikra.






Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu umetafsiri vizuri.

Mungu akubariki.
 
~Mkuu usipuuzie ndoto yoyote unayoota! Iandike!
Ukitaka kuamini hili,angalia unapoamka,unakua na hali gani? Umekosa raha,huzuni,umefadhaika,umekasirika,au umefurahi. nk.
√kimsingi ndoto ni mlango ambao Mungu anautumia sn kusema na wanadamu tukiwa tumelala,kwasababu mchana wengi wetu hatuna uwezo wa kumsikia Mungu!
Ayubu 33:14-17(soma hapa kwa faida yako,we ni mkristo umesema).
~lkn pia mlango huo unaweza kutumiwa na shetani,kupandikiza roho,uharibifu,kufanya maagano nk (coz wengi hawajui namna ya kuombea huo mlango adui asipitishe vitu vyake,yaani utumiwe na Mungu tu !
√kuna vyanzo tofauti vya ndoto, nitataja kibiblia;-ndoto kutoka kwa Mungu:zaburi 89:19,ayubu 33:14
-ndoto kutoka kwa shetani;Torati13:1-4
-ndoto kutokana na mahali unapolala(hali ya kiroho ya mahali hapo);Mwanzo 28:10-17..mfano; rahisi,ndoto unazoota ukilala kwny nyumba ya mganga wa kienyeji,kwenu,kanisani ni tofauti sbb ardhi huwa zinafanyiwa mambo mengi tu,kuwekwa wakfu(kuombewa) nk
-ndoto zinazotokana na kuwa na shughuli nyingi; kuwa busy na jambo fulani,kuliwaza sn nk;Mhubiri 5:3
~changamoto ni kujua hii ndoto chanzo chake ni nini?
~(Hiyo nimekupa tu overview ili kidogo unielewe huku mbele)
Mifano;
Soma Habari za Yesu,alipozaliwa,jinsi Yusufu alivyokuwa anasemeshwa kwenye ndoto namna ya kumkimbiza mtt!
Soma habari za Farao,Nebkadreza nk...Daniel4:1-34,mwanzo 41:7-8,Mathayo 2:22-23,1:24,2:13-18 nk
~Mungu anasema,anatupa taarifa zilizopita,zilizopo na zijazo kupitia Roho wake Mtakatifu!

√kuna wakati ukiota jiulize Jana yake ulikuwa unamuomba nn Mungu,au ulikuwa una maswali gani unajiuliza! Nk.

Ndoto za elimu kwa ujumla wake(nakupa maana soma then angalia we uko wapi,lkn pia Roho Mtakatifu yupo kukusaidia)sbb sijui maisha yako,pia ndoto zina details!(km VP inbox ipo mkuu)
√unajulishwa kiwango ulichonacho kimaandalizi,ktk fikra zako,ukilinganisha na jukumu lililoko mbele yako.
√au unajulishwa kuwa,kuna hatua mbele yako,ya kiutendaji na kimaisha,inayohitaji maandalizi ya kifikra.
√kuna jambo Fulani unatakiwa kuvuka kifikra lkn hukuweza,hujaweza kuvuka,na kwa ajili hiyo kuna eneo kwenye maisha yako ambalo limekwama kwa sbb hiyo.

√mkuu,huna maandalizi ya kutosha na utulivu kwenye jambo Fulani unalotaka kuvuka!
Kwenye maisha kuna mahali unataka kuvuka,ila bado kuna vikwazo kimaandalizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
- Mtihani kwa mtu yeyote unaleta hofu, hofu ya kufanya kulingana na matarajio.

- Kwa watu waliotumia miaka mingi shuleni hofu ya mtihani ndio hofu kubwa ambayo bongo zao zinaitambua ( feeling ya hofu ya mtihani inakua familiar), maana mitihani inafanyika kila baada ya muda mfupi.

- Katika maisha kuna mambo mengi ambayo humpa mtu hofu ya kufanikiwa, na subconsciously ubongo unaibadilisha hofu uliokutana nayo into something familiar ( feeling iliyozoeleka na ubongo, feeling ya mtihani), hapa ndipo ndoto za shuleshule hutokea.

- Naungana na aliyekushauri huko juu kuhusu kusali, unapo amini umekabidhi shida na hofu zako kwa yeye aliye na nguvu basi huwezi ota tena hizo ndoto, maana hofu hutokua nayo tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hapo sijui hali yako kiuchumi ila kiukweli kiimani hizi sio ndoto salama kabisaa katika maisha yako kiutafutaji yaani hapo malaika mlinzi anajaribu kuwakumbusha,unarudishwa nyuma kimaendeleo mwambie namtoa mada


Dah kazi kwelikweli asante sana mkuu.
 
Kwanza Mtu asikutishe hiyo haina significance yoyote na maisha yako.
Ndoto ni mind re-programming kwenye upande wa kumbukumbu.
Taarifa ( memory trace)iliyo kwenye subconscious inachotwa(retrieval) kuja kwenye ufahamu na hiyo ndiyo ndoto yako.

Ndoto mara nyingi ni unfulfilled desires na moja ya njia ya kudecode subconscious mind wakati wa kufanya psychoanalytical therapy ya magonjwa ya akili ni kumuuliza ndoto zake Mtu. Ndoto imejikita kwenye jambo unaliliwaza muda mwingi.

Mtu anaewaza pesa kwa mfano huweza kuota ndoto za hela tu either kupata au kukosa.
Mtu aliyelala usiku akasogezewa kibatali huweza kuota nyumba inawaka moto au mtu anaesikiliza redio anaweza kusikia sauti hiyo ya redio na ubongo kudecode na kutengeneza picha katika mfumo wa ndoto.

Mtu aliyelala na kamba iliyoviringishwa mguuni huweza kuota nyoka anammeza au kamba imegeuka nyoka.

Ubongo ni very sensitive ndo maana unaishi. Unauwezo wa kuchukua information ambazo hata huwezi kusihisi mfano vibrations nk

Tuliza moyo. Piga kazi. Huna haja ya kuhifadhi ndoto.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mimi nina ndoto tatu ambazo hujirudiarudia.

1. Naota niko safari lakini hata kama ni safari fupi sifiki ninakoenda.

2. Kuna mlima mmoja mrefu huko kwetu basi huu mlima huwa naota nimeuona maeneo tofautitofauti tena mbali kabisa na mahala ulipo. Huu mlima hata sijawahi kuusogelea karibu lkn ndoto sasa.

3. Naota niko zangu toilet najisaidia haja kubwa lkn cha ajabu simalizi hata saa nzima namaliza huko.

Hizi ndoto zimeshajirudia zaidi ya mara kumi kila mmoja mpaka nimeshazoea tu kuziota.

Hata za kuwa shule naota sana. Nashindwa kuelewa ni kawaida ndoto hizohizo kujirudia mara kwa mara au kuna maana zake?

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio kawaida hata kidogo kwa ndoto ile ile kujirudia mara nyingi. Ikitokea hivyo ni uthibitisho wa jambo la kiroho kujirudia katika maisha yako. Ulimwengu wa roho unatumia sana ndoto kufikisha ujumbe. Pia ndoto yaweza kumaanisha kuna jambo linaendelea katika roho liwe jambo zuri au baya..

Unayoota yanamaanisha vikwazo katika maisha yako. Wafanyakazi wa ulimwengu wa giza wamewekeza kwako na sharti ukate mirija waliyoweka kunyonya mafanikio yako.

Hakuna nanma iliyo nzuri zaidi ya kuomba kwa kutumia Jina la Yesu Kristo. Kila siku kabla ya kulala sali na kujiweka mikononi mwa Yesu Kristo. Kemea pepo, majini na wachawi. Vunja kazi zao usiku huo. Utalala kama mtoto mdogo.

Pia ingia ndani zaidi na kukata mizizi ya wachawi na wanga ili uweze kuwa huru kabisa. Hayo yote ni kwa kuwa karibu zaidi na Yesu Kristo, kutubu na kuishi utakatifu. Fanya vita ya kiroho na wachawi kwa Jina la Yesu Kristo utashinda.
 
Kuna mambo ambayo yanakutatiza lakini huna maarifa ya kutatua.

Roho wa ndoto anakuonyeaha kwamba jiandae sasa au lah unatumia sana mbeleni.

Ni tatizo lipi? Na ujiandae namna gani? hapo ndipo mtihani ulipo. mwabudu Mungu sana ili akufunulie zaidi uweze kujiandaa!!

Majority huwa ni mitihani ya kimaisha..
Yaweza kuwa maisha yako ya ndoa, kazi yako inakwenda kuisha, Biashara yako inakwenda kuporomoka nk
Uko sahihi.

Get a Bless.
 
Mkuu hapo sijui hali yako kiuchumi ila kiukweli kiimani hizi sio ndoto salama kabisaa katika maisha yako kiutafutaji yaani hapo malaika mlinzi anajaribu kuwakumbusha,unarudishwa nyuma kimaendeleo mwambie namtoa mada
Uko sahihi.

Get a Bless.
 
Ndoto za mashuleni si nzuri,nyingi ni ishala ya kuanguka ,kuwa sehemu si sahihi katika maisha yako,mfumo wa maisha yako kutokwenda vizuri,mahali ulipo hausitahili kuwepo,umekwama mahari fulani katika maisha.
Mfano ulikuwa vizuri katika masomo na hatimaye mtihani wa mwisho unapata matokeo ya chini tofauti na matalajio yako.

Kufanya kazi ambayo hukuitarajia katika maisha yako,kuishi ndoto ambazo si zako,ulitaka uishi maisha fulani ila matokeo yako unaishi maisha ambayo hukuyapenda hata tangu hujafikiria kujitegemea kiuchumi.Mambo yako kutokwenda katika mtililiko unao faa

Sent using Jamii Forums mobile app
Sad but uko sahihi.

Get a Bless.
 
~Mkuu usipuuzie ndoto yoyote unayoota! Iandike!
Ukitaka kuamini hili,angalia unapoamka,unakua na hali gani? Umekosa raha,huzuni,umefadhaika,umekasirika,au umefurahi. nk.
√kimsingi ndoto ni mlango ambao Mungu anautumia sn kusema na wanadamu tukiwa tumelala,kwasababu mchana wengi wetu hatuna uwezo wa kumsikia Mungu!
Ayubu 33:14-17(soma hapa kwa faida yako,we ni mkristo umesema).
~lkn pia mlango huo unaweza kutumiwa na shetani,kupandikiza roho,uharibifu,kufanya maagano nk (coz wengi hawajui namna ya kuombea huo mlango adui asipitishe vitu vyake,yaani utumiwe na Mungu tu !
√kuna vyanzo tofauti vya ndoto, nitataja kibiblia;-ndoto kutoka kwa Mungu:zaburi 89:19,ayubu 33:14
-ndoto kutoka kwa shetani;Torati13:1-4
-ndoto kutokana na mahali unapolala(hali ya kiroho ya mahali hapo);Mwanzo 28:10-17..mfano; rahisi,ndoto unazoota ukilala kwny nyumba ya mganga wa kienyeji,kwenu,kanisani ni tofauti sbb ardhi huwa zinafanyiwa mambo mengi tu,kuwekwa wakfu(kuombewa) nk
-ndoto zinazotokana na kuwa na shughuli nyingi; kuwa busy na jambo fulani,kuliwaza sn nk;Mhubiri 5:3
~changamoto ni kujua hii ndoto chanzo chake ni nini?
~(Hiyo nimekupa tu overview ili kidogo unielewe huku mbele)
Mifano;
Soma Habari za Yesu,alipozaliwa,jinsi Yusufu alivyokuwa anasemeshwa kwenye ndoto namna ya kumkimbiza mtt!
Soma habari za Farao,Nebkadreza nk...Daniel4:1-34,mwanzo 41:7-8,Mathayo 2:22-23,1:24,2:13-18 nk
~Mungu anasema,anatupa taarifa zilizopita,zilizopo na zijazo kupitia Roho wake Mtakatifu!

√kuna wakati ukiota jiulize Jana yake ulikuwa unamuomba nn Mungu,au ulikuwa una maswali gani unajiuliza! Nk.

Ndoto za elimu kwa ujumla wake(nakupa maana soma then angalia we uko wapi,lkn pia Roho Mtakatifu yupo kukusaidia)sbb sijui maisha yako,pia ndoto zina details!(km VP inbox ipo mkuu)
√unajulishwa kiwango ulichonacho kimaandalizi,ktk fikra zako,ukilinganisha na jukumu lililoko mbele yako.
√au unajulishwa kuwa,kuna hatua mbele yako,ya kiutendaji na kimaisha,inayohitaji maandalizi ya kifikra.
√kuna jambo Fulani unatakiwa kuvuka kifikra lkn hukuweza,hujaweza kuvuka,na kwa ajili hiyo kuna eneo kwenye maisha yako ambalo limekwama kwa sbb hiyo.

√mkuu,huna maandalizi ya kutosha na utulivu kwenye jambo Fulani unalotaka kuvuka!
Kwenye maisha kuna mahali unataka kuvuka,ila bado kuna vikwazo kimaandalizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Shukhrani sana kwa kuniongezea elimu zaidi.
 
Mimi nina ndoto tatu ambazo hujirudiarudia.

1. Naota niko safari lakini hata kama ni safari fupi sifiki ninakoenda.

2. Kuna mlima mmoja mrefu huko kwetu basi huu mlima huwa naota nimeuona maeneo tofautitofauti tena mbali kabisa na mahala ulipo. Huu mlima hata sijawahi kuusogelea karibu lkn ndoto sasa.

3. Naota niko zangu toilet najisaidia haja kubwa lkn cha ajabu simalizi hata saa nzima namaliza huko.

Hizi ndoto zimeshajirudia zaidi ya mara kumi kila mmoja mpaka nimeshazoea tu kuziota.

Hata za kuwa shule naota sana. Nashindwa kuelewa ni kawaida ndoto hizohizo kujirudia mara kwa mara au kuna maana zake?

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe una neema kubwa sana, kwa sababu ndoto zako zinakueleza shida, chanzo na jinsi ya kutatua.

Inawezekana malengo yako ya kimaisha huyafikii. Au ukianzisha kitu hakikamiliki kwa sababu ipo mizimu inafuatilia. Yawezekana yapo maagano yaliyofanyika kwenu na vizazi vilivyotangulia, maagano hayo yanakufunga mpaka wewe, na huwezi fikia malengo fulani.
Kutatua hili, inatakiwa uondokane na uovu, uchafu wote usiompendeza Mungu, uuache. Weka focus yako kujisafisha kwa kutubu kwa Mungu na kuacha njia zote mbaya.

Hapo utafanikiwa.
 
Wewe una neema kubwa sana, kwa sababu ndoto zako zinakueleza shida, chanzo na jinsi ya kutatua.

Inawezekana malengo yako ya kimaisha huyafikii. Au ukianzisha kitu hakikamiliki kwa sababu ipo mizimu inafuatilia. Yawezekana yapo maagano yaliyofanyika kwenu na vizazi vilivyotangulia, maagano hayo yanakufunga mpaka wewe, na huwezi fikia malengo fulani.
Kutatua hili, inatakiwa uondokane na uovu, uchafu wote usiompendeza Mungu, uuache. Weka focus yako kujisafisha kwa kutubu kwa Mungu na kuacha njia zote mbaya.

Hapo utafanikiwa.


Asante mkuu ni kweli kabisa kuna mambo ninayapitia mpaka ninahisi kukata tamaa.
 
Sio kawaida hata kidogo kwa ndoto ile ile kujirudia mara nyingi. Ikitokea hivyo ni uthibitisho wa jambo la kiroho kujirudia katika maisha yako. Ulimwengu wa roho unatumia sana ndoto kufikisha ujumbe. Pia ndoto yaweza kumaanisha kuna jambo linaendelea katika roho liwe jambo zuri au baya..

Unayoota yanamaanisha vikwazo katika maisha yako. Wafanyakazi wa ulimwengu wa giza wamewekeza kwako na sharti ukate mirija waliyoweka kunyonya mafanikio yako.

Hakuna nanma iliyo nzuri zaidi ya kuomba kwa kutumia Jina la Yesu Kristo. Kila siku kabla ya kulala sali na kujiweka mikononi mwa Yesu Kristo. Kemea pepo, majini na wachawi. Vunja kazi zao usiku huo. Utalala kama mtoto mdogo.

Pia ingia ndani zaidi na kukata mizizi ya wachawi na wanga ili uweze kuwa huru kabisa. Hayo yote ni kwa kuwa karibu zaidi na Yesu Kristo, kutubu na kuishi utakatifu. Fanya vita ya kiroho na wachawi kwa Jina la Yesu Kristo utashinda.


Asante sana mkuu kuna mambo nayapitia yanayoniumiza sana.
 
Back
Top Bottom