Hizi ndoto zinanitesa sana jamani

Hizi ndoto zinanitesa sana jamani

Marco Polo

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2014
Posts
13,214
Reaction score
20,988
1. Naota ghafla naingia kwenye chumba cha mitihani ya mwisho alafu hakuna nilichosema

2. Siku nyingine naota nimechelewa kuingia chumba cha mtihani muda unaisha sijajaza answer sheet kabisa na nakuwa nahangaika kwelikweli

3. Mara naota kuna mtihani nafika shule nimechelewa nafika ubaoni kujua jina langu liko room gani inanichukua muda mrefu kugundua, ile nafika chumba cha mtihani zimebaki dk chache muda wa mtihani kuisha, najikuta naingiwa na stress kisha nashindwa kujibu swali hats moja kisha nashtuka ndotoni nikiwa tafrani

NOTE: Nimepita pita shule mpaka elimu ya chuo na huko kote nilikuwa napita bila shida yeyote, msaada wakuu maana nakosa amani kabisa na zimekuwa zikijirudia mara kwa mara.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
2.Ndoto za elimu hasa shule za msingi
mambo ya kuzingatia ulikuwa na Nani? , mnafanya nini?, somo au mtihani gani ulikushinda?
Maana zake ni

.Jambo ulilolikusudia kufanya na kiwango cha maandalizi kifikra etc haviendani.

.kuna kitu umepungukiwa kwenye msingi WA kufikiri, misingi ya kufikiri imeharibika.

.kuna jambo linalokusumbua Sasa limekosa msingi mzuri wa kufikiri.

. Kupungukiwa maarifa, maono, ufahamu na fikra.






Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiota shule zilizopita kama shule ya msingi au hata sekondari wakati wewe ulishamaliza na upo chuo kikuu au hata kikuu ulishamaliza siku nyingi ni ishara ya kurudiswa nyuma katika ulimwengu wa roho. Sasa hivi kuna mambo yanayoendelea kutaka kukurudisha nyuma. Kuna kazi za wachawi wakishirikana na roho chafu yaweza kuwa majini/mapepo n.k.

Unachopaswa kufanya ni kuishi maisha safi, acha madhambi yoyote. Pili fanya maombi kila siku kabla ya kulala na unapoamka. Usiache mwanya kwa ulimwengu wa giza kukurudisha nyuma eti kwasababu tu umeshindwa kusali kwa dakika 5 kila siku.

Unapoomba omba KWA JINA LA YESU siyo vinginevyo manake hutapata msaada wa kweli wa kuchinda nguvu za giza isipokuwa KWA JINA LA YESU KRISTO.

Hayo yote yalikuwa kwenye maisha yangu lakini siku hizi nipo kwenye full control na ninasambaratisha wachawi na mapepo vibaya sana KWA JINA LA YESU KRISTO. Hakuna dawa nyingine mtu asikudanganye hata kidogo.
 
Hii Niliiona mahali huko mjini instagram emb jaribu kufuatiliahiyo page
IMG_20200514_124122_784.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
2.Ndoto za elimu hasa shule za msingi
mambo ya kuzingatia ulikuwa na Nani? , mnafanya nini?, somo au mtihani gani ulikushinda?
Maana zake ni

.Jambo ulilolikusudia kufanya na kiwango cha maandalizi kifikra etc haviendani.

.kuna kitu umepungukiwa kwenye msingi WA kufikiri, misingi ya kufikiri imeharibika.

.kuna jambo linalokusumbua Sasa limekosa msingi mzuri wa kufikiri.

. Kupungukiwa maarifa, maono, ufahamu na fikra.






Sent using Jamii Forums mobile app
Sio shule ya msingi ni secondary na chuo hasa mitihani ya mwisho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Naota ghafla naingia kwenye chumba cha mitihani ya mwisho alafu hakuna nilichosema

2. Siku nyingine naota nimechelewa kuingia chumba cha mtihani muda unaisha sijajaza answer sheet kabisa na nakuwa nahangaika kwelikweli

3. Mara naota kuna mtihani nafika shule nimechelewa nafika ubaoni kujua jina langu liko room gani inanichukua muda mrefu kugundua, ile nafika chumba cha mtihani zimebaki dk chache muda wa mtihani kuisha, najikuta naingiwa na stress kisha nashindwa kujibu swali hats moja kisha nashtuka ndotoni nikiwa tafrani

NOTE: Nimepita pita shule mpaka elimu ya chuo na huko kote nilikuwa napita bila shida yeyote, msaada wakuu maana nakosa amani kabisa na zimekuwa zikijirudia mara kwa mara.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana.

Ndoto mara nyingi hutumia ishara badala ya picha halisia ya mambo. Hivyo usichukulie unayoyaona ndotoni kama uhalisia bali ishara.

Ndoto za kurudi shule/mitihani zina maana moja kuu na zingine ndogo ndogo kulingana na "details" zilizopo kwenye ndoto yenyewe; wahusika pia mpangilio wa matukio.

HOFU
Shule na mitihani imechukua sehemu kubwa ya maisha ya wasomi. Wazee wa zamani walikua wakiota kuhusu kilimo na mifugo haswa haswa; mimea kuharibiwa au mavuno kiduchu pia waliota mifugo kufa ama kushambuliwa na wanyama wakali.

Ndoto za kurudi shule hususani kuingia katika chumba cha mitihani bila ukiwa umechelewa pia hujasoma hushabibia "self confidence" kushuka.

Akili huamua kutumia taswira ya shule na mitihani kwasababu ndio wakati pekee katika maisha yako ulipokuwa na hofu ya kushindwa na ndio sehemu pekee ya maisha unapokua "under pressure". Ukiwatafuta vipanga wa darasani walikua wanaongoza mitihani yote, hutokuta wanaota ndoto kama zako.

Sikudharau lakini kulingana na ndoto zako inaonyesha elimu yako ulipitia misukosuko mingi na ufaulu wako ulikua wa kati au chini ukilinganisha na matarajio yako pia "jinsi ujianavyo na kujitambua"

Hivyo ndoto zinaonyesha unapitia wakati mgumu unaokupa wasiwasi wa maisha na hofu kutokana na "mental pressures" za maisha. Na jinsi ya kuzishinda/kubadilisha ndoto hizo ni mtizamo wako wa maisha. Ongeza kujiamini, jichanganye na watu pia punguza mitazamo hasi ya maisha (kuwa optimistic) maana hizo ndoto zinasema wewe ni pessimist.

Labda kama unajiuliza nikupe jibu, waliokua wakiongoza darasani hususani kwenye mitihani huwa na ndoto tofauti zinazowasumbua ukilinganisha na walio chini. Kwasasa "your concern should be that of yourself not others" maana nikikwambia wanachoota utashaanga zaidi na kuuliza kwanini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee hata mimi huwa naota hizi ndoto, ila mie ni tofauti na wewe kidogo,

Mie kidato cha 6 nilizingua, kipindi nipo kidato cha 5 mwishoni nilitia mimba mabinti fulani wawili(mmoja yupo kkoo, mwingine kinondoni) kipindi hicho nipo hostel kalita magomeni, natwanga shule Azania pale, mmoja mimba yake iliharibika km miezi miwili hivi, nikabaki na kasheshe huku, so 6 sikuisoma kwa raha wala amani kabisa mzee, sababu kidogo ile familia ilikuwa mtihani, mara binti wamfukuze, anipigie katimuliwa yupo mtaani hiyo saa 6/7 usiku,mara wanipigie simu za mikwara, mara nipigiwe simu wako njiani kwenda kwetu, uzuri bibie alikuwa hawapeleki mtaani kabisa, anazuga kapasahau! Iliwachukua kama miezi mi4/5 kupafahamu maskani, hapo nina km wiki 2 mbele nipoge pepa la mwisho, nakumbuka mpaka namaliza pepa, niliogopa hata kwenda home, ilibidi nijifungie kinondoni kwao rafiki yangu(wa damu) wiki kama 3 hivi mpaka mama aliponipigia simu kuwa nirejee tu nyumbani, kifupi sikusoma kwa amani km sio kusoma kabisa form 6, waliobahatika vibaya kupata majanga kama haya wanaelewa.(story ni ndefu kidogo) baada ya pepa km wiki 3 mbele ndio mwanangu akazaliwa.
Baada ya matokeo kuwa hovyo moyo ukafa ganzi kabisa na kitu shule nikaombwa nikasome hata diploma nikagoma kabisa nikaamua nifanye biashara zangu tu mtaani, baada ya mwaka kidogo nikatulia ile hamu ya school ikarudi tena nikaenda pale DIT kwa matokeo ya form 4, kupiga telecom nikasoma semister ya kwanza fresh! Ya pili nafsi ikaanza unyonge nikitizama wenzangu walipo na mie nilipo , nikajikuta semister ya pili ada yake nafanyia mambo mengine nikawa naenda kama ushahidi tu pale, nikapiga pepa nafsi ikagoma kabisa kurudi kusoma.

Na ubaya ama uzuri class nilikuwa vizuri, toka niko mdogo(primary) o level nilikuwa nikiishi najua mimi ni engineer wa baadae. Jamaa zangu wengi sasa ni ma engineer.

Hii kitu huwa naota saana, mara nyingi naota nipo zangu napiga pepa ya namba nacheza na zile namba km sina akili nzuri, au ndio hivyo nipo class, ama napiga pepa halafu vitu vinashuka tu easy, nacheki matokeo na vitu kama hivyo.
Ni ndoto ambazo naziota mnoo.
Sometimes natamani nirudi kusoma hata nikamilishe tu ndoto zangu, hata kama sintakifanyia kazi kile nitakachosomea, naimani nafsi itatulia, kama sio mwaka huu hata mwakani nikishafaniliwa kuoa inshaallah nitajaribu kusoma tena.

Sasa sijui kwa wewe ndoto hizo zinachagizwa na nini kwa kweli.
 
Mzee hata mimi huwa naota hizi ndoto, ila mie ni tofauti na wewe kidogo,

Mie kidato cha 6 nilizingua, kipindi nipo kidato cha 5 mwishoni nilitia mimba mabinti fulani wawili(mmoja yupo kkoo, mwingine kinondoni) kipindi hicho nipo hostel kalita magomeni, natwanga shule Azania pale, mmoja mimba yake iliharibika km miezi miwili hivi, nikabaki na kasheshe huku, so 6 sikuisoma kwa raha wala amani kabisa mzee, sababu kidogo ile familia ilikuwa mtihani, mara binti wamfukuze, anipigie katimuliwa yupo mtaani hiyo saa 6/7 usiku,mara wanipigie simu za mikwara, mara nipigiwe simu wako njiani kwenda kwetu, uzuri bibie alikuwa hawapeleki mtaani kabisa, anazuga kapasahau! Iliwachukua kama miezi mi4/5 kupafahamu maskani, hapo nina km wiki 2 mbele nipoge pepa la mwisho, nakumbuka mpaka namaliza pepa, niliogopa hata kwenda home, ilibidi nijifungie kinondoni kwao rafiki yangu(wa damu) wiki kama 3 hivi mpaka mama aliponipigia simu kuwa nirejee tu nyumbani, kifupi sikusoma kwa amani km sio kusoma kabisa form 6, waliobahatika vibaya kupata majanga kama haya wanaelewa.(story ni ndefu kidogo) baada ya pepa km wiki 3 mbele ndio mwanangu akazaliwa.
Baada ya matokeo kuwa hovyo moyo ukafa ganzi kabisa na kitu shule nikaombwa nikasome hata diploma nikagoma kabisa nikaamua nifanye biashara zangu tu mtaani, baada ya mwaka kidogo nikatulia ile hamu ya school ikarudi tena nikaenda pale DIT kwa matokeo ya form 4, kupiga telecom nikasoma semister ya kwanza fresh! Ya pili nafsi ikaanza unyonge nikitizama wenzangu walipo na mie nilipo , nikajikuta semister ya pili ada yake nafanyia mambo mengine nikawa naenda kama ushahidi tu pale, nikapiga pepa nafsi ikagoma kabisa kurudi kusoma.

Na ubaya ama uzuri class nilikuwa vizuri, toka niko mdogo(primary) o level nilikuwa nikiishi najua mimi ni engineer wa baadae. Jamaa zangu wengi sasa ni ma engineer.

Hii kitu huwa naota saana, mara nyingi naota nipo zangu napiga pepa ya namba nacheza na zile namba km sina akili nzuri, au ndio hivyo nipo class, ama napiga pepa halafu vitu vinashuka tu easy, nacheki matokeo na vitu kama hivyo.
Ni ndoto ambazo naziota mnoo.
Sometimes natamani nirudi kusoma hata nikamilishe tu ndoto zangu, hata kama sintakifanyia kazi kile nitakachosomea, naimani nafsi itatulia, kama sio mwaka huu hata mwakani nikishafaniliwa kuoa inshaallah nitajaribu kusoma tena.

Sasa sijui kwa wewe ndoto hizo zinachagizwa na nini kwa kweli.
vipi huyo binti still upo naye?? baharia a baharia haahaaaa!! mimi nilikuwa nasoma Al muntazir nilikuwa napiga sana pale azania

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tukio kama la kwako lilikuwa linanitokea mara kwa mara kipindi nipo kidato cha nne karibia na mtihani wa taifa mara kadhaa nilikuwa naota nipo katika chumba cha mtihani.nakumbuka mara ya kwanza nikiwa nafanya mtihani wa kwanza ambao ulikuwa english mara najikuta sijaandika namba ya mtihani ukurasa hata mmoja katika booklet kitendo ambacho kilinipa hofu na kujilaumu kutokana na kutojaza namba kwenye booklet.mara ya pili nakumbuka nilikuwa na fanya math somo ambalo nilikuwa nimelipa kipao mbele na nilikuwa nalitegemea pia mpaka muda wa mtihani unaisha sijafanya swali hata moja na karatasi zinakusanywa.mara ya tatu nikaota nipo nafanya mtihani wa biology ambapo nilichelewa kuingia kwenye chumba cha mtihani.binafsi nadhani kuweka fikra kwa kiwango kikubwa katika jambo fulani huweza kusababisha uwe unaota ndoto za kile kitu mara kwa mara pia kuna muda automatic utakuta unaota ndo juu ya mtu fulani au eneo fulani kwa zaidi ya usiku mmoja au mara moja
 
Back
Top Bottom