Wakati huo ilikuwa mabaki ya matairi ya tractor, yakifanywa laisoni (raise-on).
Bakhresa (hili ji tajir
La sasa) alikuwa ana kaduka kakushona viatu Uhuru, si hivi vya laisoni.
Suruali vitambaa vya krimplin.
Dawa za mswaki Maxim za kichina, ukipigia kutwa nzima mdomo hauna uwezo wa kupata test ya sukari.
Sukari yenyewe kuipata ilikuwa mpaka upange foleni upatiwe kilo moja kwa wiki kwa kaya.
Ukitaka kula Nyama, mpaka ukapange foleni kwenye mabucha.
Ukipanda Teksi mkipita kwenye vidimbwi vya maji inabidi unyanyue miguu na ilhali umo ndani ya gari, la sivyo unarowesha bugaluu. Teksi zenyewe pijo fo not fo (404) ndio za maana.
Ma-jinsi ya lee na levis mpaka utembelee Mombasa kwenda kuyanunuwa au mitaani kwa bei mbaya (shilin sabin na tano)
Duhhhh, nyerere alitupatia kweli.
And you wont believe but in not more than five years this fashion will be back.
Duh!msela huyo!!
Hawa wa sasa na hizi Kata-K zao duh....