Hizi Mbinu, Polisi walijifunzia wapi?

Andindile

JF-Expert Member
Mar 18, 2009
304
16
Polisi wamweka rumande mtoto babake ajitokeze http://www.majira.co.tz/index.php?v...okeze&format=pdf&option=com_content&Itemid=57 http://www.majira.co.tz/index.php?v...nt&print=1&page=&option=com_content&Itemid=57 http://www.majira.co.tz/index.php?o...rZXplJm9wdGlvbj1jb21fY29udGVudCZJdGVtaWQ9NTc= Sunday, 10 May 2009 09:58 Na Glory Mhiliwa, Arusha

JESHI la polisi Mkoa wa Arusha linamshikilia mtoto wa miaka tisa aitwaye Richard Grayson mkazi wa Shangarai ili kumshinikiza baba yake anayetuhumiwa kuhusika katika matukio ya ujambazi ambaye anadaiwa kukimbia kusikojulikana kujisalimisha.

Tukio hilo lilitokea juzi alfajiri majira ya saa kumi na moja baada ya askari polisi wakiwa na gari aina ya Land Rover Defender kwenda nyumbani kwa mtuhumiwa huyo ambapo walipomkosa waliamua kuondoka na mtoto huyo.

Mtuhumiwa huyo Grayson Mollel (34),Jeshi hilo linadai kuwa linamtafuta kutokana na tuhuma za ujambazi zinazomkabili. Hata hivyo halikuwa tayari kutaja baadhi ya matukio ya ujambazi ambayo mtuhumiwa huyo anadaiwa kuhusika nayo.

Akizungumza na Majira Jumapili kuhusiana na tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Bw. Basilio Matei alisema kuwa taarifa za mtoto huyo kushikiliwa ili kumshinikiza baba yake kujisalimisha hazijawasilishwa kwake.

‘Mimi ndio kwanza nasikia kutoka kwenu lakini naahidi kufuatilia ili kujua ukweli wa tukio hilo kama kweli mtoto huyo alikamatwa na kulazwa rumande kwa kosa ambalo linamhusu baba yake nitawapatieni taarifa kamili’ alisema Basilio.

Aidha mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi ya Moivo wilaya ya Arumeru anadaiwa kutiwa nguvuni na askari polisi wakiwa na silaha baada ya kuvamia nyumbani kwao eneo la Shangarai wilaya ya Arumeru.

Hata hivyo askari hao baada ya kumchukua mtoto huyo walimwamuru wamweleze baba yake alipo ambapo aliwaelekeza nyumba ya mama yake mdogo ambae ni mke mdogo wa baba yake anayeishi Sanawari. Hata hivyo hawakufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo na ndipo walipoamua kumkamata na mama huyo pia. Aidha mama huyo aliyefahamika kwa majina ya Georgina Grayson alikamatwa na kuswekwa rumande kama ilivyo kwa mwanae

Hatua ya mtoto huyo mwenye umri wa miaka tisa aliyekuwa ametoka hospitali ya wilaya ya West Meru alipokuwa akiuguza kifua baada ya kuanguka kwenye mti kumetafsiriwa na wananchi kuwa jeshi la polisi linakiuka haki za mtoto. Bi Neema Florence ambae ni mkazi wa Shangarai anasema kuwa mtoto huyo ni mdogo sana
kulazwa mahabusu ya watu wazima tena kwa kosa alilofanya baba yake.

Mtoto kakosa nini?
 
Polisi wamweka rumande mtoto babake ajitokeze Sunday, 10 May 2009 09:58 Na Glory Mhiliwa, Arusha

JESHI la polisi Mkoa wa Arusha linamshikilia mtoto wa miaka tisa aitwaye Richard Grayson mkazi wa Shangarai ili kumshinikiza baba yake anayetuhumiwa kuhusika katika matukio ya ujambazi ambaye anadaiwa kukimbia kusikojulikana kujisalimisha.

Tukio hilo lilitokea juzi alfajiri majira ya saa kumi na moja baada ya askari polisi wakiwa na gari aina ya Land Rover Defender kwenda nyumbani kwa mtuhumiwa huyo ambapo walipomkosa waliamua kuondoka na mtoto huyo.

Mtuhumiwa huyo Grayson Mollel (34),Jeshi hilo linadai kuwa linamtafuta kutokana na tuhuma za ujambazi zinazomkabili. Hata hivyo halikuwa tayari kutaja baadhi ya matukio ya ujambazi ambayo mtuhumiwa huyo anadaiwa kuhusika nayo.

Akizungumza na Majira Jumapili kuhusiana na tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Bw. Basilio Matei alisema kuwa taarifa za mtoto huyo kushikiliwa ili kumshinikiza baba yake kujisalimisha hazijawasilishwa kwake.

‘Mimi ndio kwanza nasikia kutoka kwenu lakini naahidi kufuatilia ili kujua ukweli wa tukio hilo kama kweli mtoto huyo alikamatwa na kulazwa rumande kwa kosa ambalo linamhusu baba yake nitawapatieni taarifa kamili’ alisema Basilio.

Aidha mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi ya Moivo wilaya ya Arumeru anadaiwa kutiwa nguvuni na askari polisi wakiwa na silaha baada ya kuvamia nyumbani kwao eneo la Shangarai wilaya ya Arumeru.

Hata hivyo askari hao baada ya kumchukua mtoto huyo walimwamuru wamweleze baba yake alipo ambapo aliwaelekeza nyumba ya mama yake mdogo ambae ni mke mdogo wa baba yake anayeishi Sanawari. Hata hivyo hawakufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo na ndipo walipoamua kumkamata na mama huyo pia. Aidha mama huyo aliyefahamika kwa majina ya Georgina Grayson alikamatwa na kuswekwa rumande kama ilivyo kwa mwanae

Hatua ya mtoto huyo mwenye umri wa miaka tisa aliyekuwa ametoka hospitali ya wilaya ya West Meru alipokuwa akiuguza kifua baada ya kuanguka kwenye mti kumetafsiriwa na wananchi kuwa jeshi la polisi linakiuka haki za mtoto. Bi Neema Florence ambae ni mkazi wa Shangarai anasema kuwa mtoto huyo ni mdogo sana
kulazwa mahabusu ya watu wazima tena kwa kosa alilofanya baba yake.

Mtoto kakosa nini?

Jeshi la polisi halina mamlaka ya kumzuia mtoto huyo. Hakuna sheria inayosema hivyo, pili kama wanamtuhumu mtoto huyo basi walitakiwa wamfungulie mashtaka. What a crap!
 
Hii imenisikitisha saana kwani ni ukiukwaji wa haki za binadamu, labda kama mtoto pia anashiriki au wanahisi kafundishwa. Lakini kama bado basi tayari wamemuharibu mtoto kwa kuanza kumfundisha na sitashangaa kama hawajamfinya kengere zake
 
This is a tort of false imprisonment and the young boy deserves to be compensated, he should be encouraged to go to Court and claim. In that way the police force will start working according to principles and not threats and intimidation.
 
Mbaya zaidi ni wa miaka 9! What an inhumane hehavior?

Tunategemea wanasheria na wapenda haki za binadamu watalivalia njuga

suala hili na kuhakikisha kwamba mtoto huyo anaachiliwa mara moja na

kwenda shule.

Huko rumande anaishiishi vipi! Kwa umri huo anafundishwa tabia mbaya na

chafu sana bila sababu yoyote. Je jeshi letu limeishiwa mbinu za kumsaka

mhalifu kabisa na kufikia kugundua sayansi mpya hii ya utafutaji

watuhumiwa?
 
Back
Top Bottom