Aiseee...yawezekana hata huo muda usiwepo ehhhh?!Ngoja nisubirie penzi tamu kama asali labda na mie ntaona ni kwa kiasi gani umuhimu wa marafiki unaweza kushuka!Unapoingia kwenye ndoa na ikawa tamu, marafiki wa jinsia tofauti hata kama walikuwa karibu kiasi gani huanza kupukutika wenyewe na mwisho utaishi kama hujawahi kuwa nao vile. Hata wakiendelea kuwasiliana nawe mawasiliano yatakuwa ya kawaida sana na hakuna atakayehoji urafiki wenu. Tatizo la marafiki wa jinsia tofauti ni kwamba ukaribu wao huongezeka kadri ndoa inavyozidi kuingia uchungu. Ndiyo maana watu huanza kuhoji na mwishowe hufikia hatua migogoro ikawa mikubwa hata kuvunja ndoa.
Lizzy tazama mfano huu: Unamzimia jamaa m1 ile mbaya, jamaa naye hataki ukae mbali na mwisho mmeamua kuoana. Mshikaji huyu ndiyo kila kitu kwako, hujisikii raha akiwa mbali, hapiti popote akitoka kutafuta kabla hajakuona wewe pia (kama unatafuta). Mkiwa home mnasaidiana mambo mengi na raha mnapeana. Mnataniana mnadekezana na usiku ukijigeuza anashtuka. Simu ikiita kwa pamoja mnasonya kwa kuwa imeingilia privacy yenu. Swali linakuja: Mapenzi yakiwa yamekolea na nyie kufanya maksudi yasichuje nafasi ya rafiki zako wa zamani tena wa jinsia tofauti unaupata wapi.
Ninavyojua mimi penzi likiwa tamu hata JF itaonekana inakupotezea muda wa kukaa na mwandani wako. Sijui wewe unakuwa vipi ukiwa penzini!
Aiseee...yawezekana hata huo muda usiwepo ehhhh?!Ngoja nisubirie penzi tamu kama asali labda na mie ntaona ni kwa kiasi gani umuhimu wa marafiki unaweza kushuka!
Katika maisha marafiki wana nafasi yao hata uwe kwenye penzi tam kama nini!
Una maanisha aanacheka na kugonga na nyumba ndogo?kidumu?Minafikiri sio mwisho wa urafiki na jinsia nyingine tofauti, ila ni mwanzo wa social distance kati yenu,manake watu wengine bwana utamkuta stori sana vicheko,kugonga,outing na mme au mke wa mtu lakini akifika jimboni mwake hayafanyi haya we unafikiri urafiki wa aina hii utaeleweka kweli jimboni?? Naongea na LIZZY ripoti hii usipuuze:glasses-nerdy:
Una maanisha aanacheka na kugonga na nyumba ndogo?kidumu?
Mimi mke wangu marafiki zake wote ni wanaume kwa visingizio kuwa wafanyakazi wenzake, wanapiga deals pamoja, tangu kuzaliwa amezoea wanaume kuliko wanawake amabao yeye anawita wambea. Sasa tatizo kila akibeba mimba lazima aitoe kwa visingizio mbali mbali kama vile kwa sasa nina kazi nyingi siwezi kupewa likizo ya uzazi, au sijisikii kuzaa kwakweli sasa hivi nk, nk.
Ana uhuru wa kutosha kurudi nyumbani muda anaotaka kwa kile anachosema alikuwa na evening talks na marafiki zake hao wa kiume!!
Je mpaka hapo kuna usalama katika urafiki huo ( manake mimi siulizi hata akirudi saa 6 usiku namfungulia mlango, manake siku hizi utaambiwa ni mfumo dume kumnyima uhuru au kumuuliza anatoka wapi muda huo!!) sasa mimba anazotoa si ni kuogopa zisijekuwa zinafanana na urafiki wake huo???