Hivi yupo Mwanamke ambaye ana amani miaka 35 bila Mtoto?

Hivi yupo Mwanamke ambaye ana amani miaka 35 bila Mtoto?

Surya

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2015
Posts
9,751
Reaction score
15,545
Mimi naamini duniani lolote linaweza kutokea hata bibi wa miaka 90 kuzaa Mtoto,

Je tuna wanawake ambao wapo Tayari Kufikisha 35 years bila kuwa na mtoto na ukawa na amani kusubiri zaidi Siku yako ?

Au ndio tunafikiri Mungu ni Mungu wa Yes kila kitu ?
 
Mimi nadhani hayo ni masuala ya mtu binafsi kwa kadri ya mtazamo wake na alivyoamua kuyaendesha mambo yake kwenye maisha yake!!!!

Ni jambo la ajabu kwa watu wazima kukaa kujadili utashi , machaguo na maamuzi ya watu wengine!!!

Awe na furaha au anahuzunika nadhani sio jambo kujadili!!

Maisha Yana changamoto na heka heka nyingi zinazowapitisha watu kwenye mapito mbali mbali yanayowapelekea kufanya maamuzi yao au hata kubadilisha hatma zao!!!
 
Ukose Amani Kwa sababu Huna mtoto???? huo Ni utaahira!!
Upweke ndo husababisha kukosa Amani. Kama huna mtoto na huna upweke hakuna tatizo. Changamoto ni umri umeenda, wanaokuzunguka wote Wana Familia zao, wewe ukirudi kwako upo pekeyako, ukiumwa hakuna wa kushtuka kuwa unaumwa, huna wa kufarahi nae akafurahi wala huna wa kuhuzunika nae akahuzunika. Hapa ndipo utakapokosa amani.
 
Mimi naamini duniani lolote linaweza kutokea hata bibi wa miaka 90 kuzaa Mtoto,

Je tuna wanawake ambao wapo Tayari Kufikisha 35 years bila kuwa na mtoto na ukawa na amani kusubiri zaidi Siku yako ?

Au ndio tunafikiri Mungu ni Mungu wa Yes kila kitu ?
Mtu aliyeamua kwa hiari yake kutokuwa na mtoto kwanini akose amani?
 
Upweke ndo husababisha kukosa Amani. Kama huna mtoto na huna upweke hakuna tatizo. Changamoto ni umri umeenda, wanaokuzunguka wote Wana Familia zao, wewe ukirudi kwako upo pekeyako, ukiumwa hakuna wa kushtuka kuwa unaumwa, huna wa kufarahi nae akafurahi wala huna wa kuhuzunika nae akahuzunika. Hapa ndipo utakapokosa amani.
Nimekupata vyema shida sio mtoto exactly Tatizo Ni upweke!!
 
Back
Top Bottom