Hivi Yanga wanatumia fomesheni gani?

Hivi Yanga wanatumia fomesheni gani?

Lupweko

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2009
Posts
25,122
Reaction score
27,235
Just curious, naombeni mnifahamishe maana kila nikijaribu kuchunguza mechi zao naona kama wanapeleka tu mpira mbele ili mradi purukushani izae goli.
 
Mkuu huu mwaka 2012, eti unauliza formation katika mpira wa Yanga au Simba uoni haibu? Kwa taarifa yako hizi timu ni timu zinazoua mpira wa kibongo pamoja na wadhamini wao. Katika mechi ya juzi, je uliona ujuzi wowote wa kutafuta magoli zaidi ya kuvunjana miguu? Hili ndilo tatizo la kuwa na wachezaji wachawi wasiofundishika. Ukiendelea kufuatilia mpira wa Simba na Yanga haki ya Mungu utajiua kwa pressure, mpira gani mwaka nenda mwaka rudi yale yale tu, butua butua tutapata goli Mungu akipenda.
 
Just curious, naombeni mnifahamishe maana kila nikijaribu kuchunguza mechi zao naona kama wanapeleka tu mpira mbele ili mradi purukushani izae goli.

Haruna Moshi "Boban" himself anatumia mfumo gani?,ile style ya juzi ni ya mfumo gani?
 
Just curious, naombeni mnifahamishe maana kila nikijaribu kuchunguza mechi zao naona kama wanapeleka tu mpira mbele ili mradi purukushani izae goli.

mi nadhani tumualike Minziro Jamvin labda ye atatuambia
 
Timu zote za Bongo zinatumia formation ya" twende pale Mpira ulipo"
Formation za 442, na nyinginezo ni nadharia tu ya mdomoni na practically n wote tunaufuata Mpira ulipo.
 
kwani wewe unafahamu formation za namna gani?
4 5 1 Bahanuzi akibakia kama lone striker ndio mfumo niliouona juzi.
Tatizo lenu vijana wa 90 s hamjui mpira mnaishia kusikia story za kina Dr leak na kibonde
 
Just curious, naombeni mnifahamishe maana kila nikijaribu kuchunguza mechi zao naona kama wanapeleka tu mpira mbele ili mradi purukushani izae goli.

Na Simba yako je...wanatumia fomesheni gani??

Katika mechi ya Yanga v Simba, kipindi cha kwanza Simba walipata goli lao wakiwa na ball possession ya 59% v 41% ya Yanga. Kipindi cha pili, Yanga walisawazisha goli wakiwa na ball possession ya 69% v 31% ya Simba.

So, sijui Yanga wanatumia fomesheni gani wala Simba. Lakini based on head-to-head statistics hizo hapo juu, Yanga ilipata goli kwa kumiliki mpira zaidi (therefore more entertaining) kuliko Simba walivyomiliki wakati wa kupata bao lao.

Nimekutafunia, meza!
 
Na Simba yako je...wanatumia fomesheni gani??

Katika mechi ya Yanga v Simba, kipindi cha kwanza Simba walipata goli lao wakiwa na ball possession ya 59% v 41% ya Yanga. Kipindi cha pili, Yanga walisawazisha goli wakiwa na ball possession ya 69% v 31% ya Simba.

So, sijui Yanga wanatumia fomesheni gani wala Simba. Lakini based on head-to-head statistics hizo hapo juu, Yanga ilipata goli kwa kumiliki mpira zaidi (therefore more entertaining) kuliko Simba walivyomiliki wakati wa kupata bao lao.

Nimekutafunia, meza!

goli la simba la movie la yanga la penalt,unalo?
 
Kama ndio hivyo,ball possesion ya nin kuzungumzia?! Tunataka goli na ushindi hzo entertainment ni kwa Barcelona labda...
 
Haruna Moshi "Boban" himself anatumia mfumo gani?,ile style ya juzi ni ya mfumo gani?
dah! we na Boban, Boban na wewe; nina wasiwasi na mtoto utakae zaa kama hawatafanana sijui.
 
5-4-1 and still they ship in goals like a rugby team


Mchawi hafundishiki kucheza mpira hata iweje. Mpira ni kipaji, na ukiwa na wachezaji wenye vipaji ndipo unaweza kusema una timu lakini si hawa wa Simba na Yanga. Mchawi anatumia formation? Huyo mchawi wa wapi mleteni hapa tumjue na tumuulize anafanyaje fanyaje. Mkitaka formation angalieni mipira ya nje, hapa Bongo mtajipa pressure bure au la kama mna hela na muda wa kupoteza sawa, angalieni.
 
Back
Top Bottom