Hivi vijana wengine mnaharakisha nini kuoa?

Hivi vijana wengine mnaharakisha nini kuoa?

NIMPENDENANI

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2014
Posts
6,114
Reaction score
5,397
Habari za asubuhi wana Jamii Forums.

Mwenzenu kuna jambo linaniumiza kichwa naomba fikra zenu.Kuna mtoto wa shemeji yangu tunamlea tangu wazazi wake wafariki miaka 14 ilopita kijana sasa yuko chuo mwaka wa pili.

Jana jioni amekuja kuniomba anataka kuongea na mimi nikamwambia sawa, kikubwa kwenye maongezi nikutaka kuoa
Nikamuliza amejipanga vipi sababu bado anasoma kwanini asimalize chuo ndio akafikiria kuoa.

Nimemwambia kwa roho safi tuu sababu yeye anaishi kwangu na wadogo zake ndugu za wazazi wao waliwakataa nimewalea mimi na hakuna kitu sija wapa nimejitahidi kadri ya uwezo wangu wasijisikie wanyonge.

Cha ajabu amekwenda kumwambia mume wangu kua simpendi na sitaki akae kwangu na mume anashikilia muache aoe eti mtoto akililia wembe mpe,imeniuma yule mtoto kusema hivi sababu hakuna nisicho jitahidi kwao yeye na wadogo zake.

Hata chuo school fees nalipa mimi leo nimekua simpendi, nimemwambia fikiria tena unachotaka kufanya.
huyo mke akiolewa nyumba yakukaa hana inabidi aje tena kukaa nyumbani.

Sielewi waungwana hebu nisaidieni, jee kumwambia subiri ni sawa au nimekosea.
 
kijana amevurugwa huyo n'a huyo mumeo sijui anataka afanye majaribio gani wakati kila kitu kipo wazi! kiufupi mama upo sahihi sanah penggine kilichobaki muulize sasa kama wote mtaridhi yeye kuo je yeye amejiandaa andaaje kua baba wa familia? potelea mbali wazazi mnaweza kumlipia mahali lakini yeye ana mmipango gani kuhudumia familia?
kingine hapa sijaone swali la kwamba anataka kuoa lin? waweza kuta anawaelezea mipango yake ya miaka 5 ijayo ikibidi mpeni nafasi ya kwenda kushauriwa n'a vjana wenzie ili apewe uhalisia wa maisha maana navyojua mimi vjana wa leo kuo ni mzigo kwao n'a hawapo tayar kuharakia

mama mimi nimeona hayo kwa sasa naimani yatajenga kidogo kwenye hilo!!
 
wewe ni mlezi mwema, simamia msimamo wako,,, kaa na mmeo mshauriane kwa upole na amani, atakusoma tuu...pole kwa majukumu.
 
halmashauri ya bichwa lake imeshaamua kuoa hata ukimpinga vip utakuwa unajisumbua tu badala yake utaanza kupokea maneno machafu ya kuwa unampangia maisha au unamwonea wivu

mwache aoe kama alivyosema babaake ila kaa naye muelezee ugumu atakaokutana nao
 
Hata usipate shida, hapo umepata house girl bila kutafuta kama watakuja kukaa kwako, tena hakikisha kama una dada wa kazi mrudishe kwao akapumzike kwa kua house girl atakuwa kijileta, yeye aoe ila cha moto atakiona. Wanawake nasi kuona jamaa yupo chuo yeye kajua jamaa ndio kamaliza kila kitu, hajui kuna kupambana nakutafuta ajira, haya ngoja tuone.
 
huyo mume wako nadhani hampend huyo kijana kama anashauri aoe. Kwa uwezo gan alonao aoe au atamtunza yeye na mke wake
 
Huyu kijana na mpenzie wote mburura yani jamaa hata chuo ajamaliza achilia hilo ujana bado anao unampa tabu alafu unakubali kuolewa na mtu wa hivyo kasi kweli kwel ...mama weee mweleze kama mlezi akilazimisha toa mahari aoe alafu kaa pembeni mtu akiongeza familia jua anauwezo wa kutunza sitaki kuamini kama upo timamu ujaweza kujilea alafu unaongeZa mtu ...nikae kimya tu labda anaona mnafaidi sana
 
Anadhani kuoa is all about kutekenyana kitandani!We umetimiza wajibu kadri uwezavyo,muache achague maisha anayotaka!
 
kijana amevurugwa huyo n'a huyo mumeo sijui anataka afanye majaribio gani wakati kila kitu kipo wazi! kiufupi mama upo sahihi sanah penggine kilichobaki muulize sasa kama wote mtaridhi yeye kuo je yeye amejiandaa andaaje kua baba wa familia? potelea mbali wazazi mnaweza kumlipia mahali lakini yeye ana mmipango gani kuhudumia familia?
kingine hapa sijaone swali la kwamba anataka kuoa lin? waweza kuta anawaelezea mipango yake ya miaka 5 ijayo ikibidi mpeni nafasi ya kwenda kushauriwa n'a vjana wenzie ili apewe uhalisia wa maisha maana navyojua mimi vjana wa leo kuo ni mzigo kwao n'a hawapo tayar kuharakia

mama mimi nimeona hayo kwa sasa naimani yatajenga kidogo kwenye hilo!!
Anataka harusi mwezi wa 5 mwaka huu akapose na harusi mwezi 9 yani amekuja na list nzima mie nimechoka nafsi yangu
na kinachoniuma nikua haoni kama namtakia mema yeye...
 
Nimpendenani pole sana kama ID yako inavojieleza apo watu hawapendeki so kama ndo anachotaka mpe tu sa utafanyaje mama
 
Anadhani kuoa is all about kutekenyana kitandani!We umetimiza wajibu kadri uwezavyo,muache achague maisha anayotaka!
Nimdogo sana he is just 21 anaoa nini? kazi hana analishwa anavishwa pesa ya matumizi pia anapewa huyo ni mumekweli?
 
yaan ukimruhusu aoe ujiandae kumtunza yeye na mke ikiwemo kumsomesha amalize shule yake au kumwacha aishi maisha yake mwenyewe atakayokuwa amechagua. Endelea kumshauri lakin ataelewa labda. Yawezekana hako kadada kameng'ang'aniza akaoe nae hataki kukapoteza
 
Nimpendenani pole sana kama ID yako inavojieleza apo watu hawapendeki so kama ndo anachotaka mpe tu sa utafanyaje mama
Siwezi kumpa tuu am sure hajui anachofanya amekuja kutoka chuo likizo sijui kaonjeshwa nini yani amekolea vibaya mno
yani katika mtoto anaenipenda na kunisikiliza ni huyu lakini jana ameniacha HOI....mpaka nimelia....
 
inawezekana huo ndio wakati wake mwache.
 
Siwezi kumpa tuu am sure hajui anachofanya amekuja kutoka chuo likizo sijui kaonjeshwa nini yani amekolea vibaya mno
yani katika mtoto anaenipenda na kunisikiliza ni huyu lakini jana ameniacha HOI....mpaka nimelia....

Mh au kashawekwa kwenye chupaaa,tafuta ata mchungaji kama we ni mkristo au wazee wa ukoo wakae waongee nae ndoa sio mchezo
 
Back
Top Bottom