Hivi unakumbuka nini ukiona picha hii??

Hivi unakumbuka nini ukiona picha hii??

Enzi hizo radio ni Am tu, Rtd vipindi twendeni shambani, saa sita mchana unatega kusikia nyimbo za nje kupitia external
 
Zamani kaseti hizo zilikuwa zinatumika katika vibanda vya pombe ya kienyeji. Muuza pombe alikuwa anachukua hiyo tape alafu anarekodi vipindi vyote hadi taarifa ya habari, wateja wakishafika kuanza kulewa usiku unapozidikuwa mwingi anachukua redio yake na kutia tape, ngoma inaanza kulia taarifa ya habari ya saa mbili usiku, kwa kuwa pombe imesha controll celebrum walevi hudhani saa mbili usiku kweli na kuendelea kulewa.
Jindal unatisha....
 
20120428154447.jpg
Hizo enzi hizo unazipata kwenye maduka ya RTC tu na lazima upewe na chumvi au vikombe vya kioo....
 
Nnachokumbuka ni kwamba kwangu nilikuwa najiskia raha sana ikiimba huku naitazama kuliko kucheza.

Swala lililokuwa linanichanganya ni kwanini wakati flani tairi moja kwenye kanda linazunguka speed sana kuliko lingine.
 
mie nakumbuka enzi hizo nyimbo kama imeisha unataka kusikiliza tena inabidi utumie peni kurewind kama rewinder ya radio imekufa... hahahaha
Hiyo rewinder kwetu ilikuwa marufuku kuitumia, eti inamaliza betri.
 
Longtime sana Aurlus mabere dally kimoko Diblo Dibala machine gun Nnene chaku soukuos star Yondo sister Sama ngwana franco Akiwa na Tp ok jazz Papa wemba akiwa Viva la musica Extra musica Awilo longomba Mbilia bell Tabu ley Kandabongoman Lucien Bokilo koffi olomide Wenge musica Bcbg na wengineo wengi enzi za disco Vumbi
 
Hapo ushafungwa khanga ya kiuno(kibwebwe) alaf mpo kama watano hivi mnashindania sh 5 imewekwa mezani... Inde moniiii.. Ni viuno tu
 
Mwaka 1998 nilirekodi mazungumzo yetu mimi na mchumba wangu kwa kutumia Radio yangu aina ya HITACHI. Ule mkanda (cassete) ulikuwa na muziki wa bingwa wa Soukous Alain Kounkou wa Zaire(Congo DR) sote tulikuwa tukipenda sana kusikiliza rekodi zake huyu nguli. Mchumba alikasirika kwa kurekodiwa bila ridhaa. Niliamua kununua mkanda mwingine kama ule tena, na ule wenye sauti yake nikauhifadhi ktk shubaka la makorokoro ambayo kwa kawaida si muhimu sana wala si takataka, Hayatupwi. Mwaka 2000 tuliowana na kuj'aliwa mtoto. Kwa mapenzi yake MUNGU mke wangu alifariki mwaka 2011 akiwa mjamzito wa mapacha wawili na niliwapoteza wote. MUNGU ni mwema mke wangu aliniachia Bint yetu wa kwanza aliyezaliwa mwaka 2006 na wakati mama yake anafariki alikuwa na miaka mitano sawia. Juzi huyu bint yangu ametimiza miaka 10, niliamua (sijui kwa nini) kumuuliza kama anakumbuka chochote kuhusu mama yake akasema hakumbuki vema. Niliamua kuchukua ile Radio na ile cassete na kumuomba tuisikilize. Tulilia sana! Ubarikiwe mtoa mada.
 
Nnachokumbuka ni kwamba kwangu nilikuwa najiskia raha sana ikiimba huku naitazama kuliko kucheza.

Swala lililokuwa linanichanganya ni kwanini wakati flani tairi moja kwenye kanda linazunguka speed sana kuliko lingine.
Ule upande ambao "Mkanda" wa kaseti ndio upo full tairi huzunguka pole pole na ule upande ambao ni empty huzunguka kwa Spidi zaidi, yaani kama una play kaseti From side A kwenda side B basi side B tairi litazunguka kwa spidi zaidi,ni kwaajili ya "Load" tu.
 
Mwaka 1998 nilirekodi mazungumzo yetu mimi na mchumba wangu kwa kutumia Radio yangu aina ya HITACHI. Ule mkanda (cassete) ulikuwa na muziki wa bingwa wa Soukous Alain Kounkou wa Zaire(Congo DR) sote tulikuwa tukipenda sana kusikiliza rekodi zake huyu nguli. Mchumba alikasirika kwa kurekodiwa bila ridhaa. Niliamua kununua mkanda mwingine kama ule tena, na ule wenye sauti yake nikauhifadhi ktk shubaka la makorokoro ambayo kwa kawaida si muhimu sana wala si takataka, Hayatupwi. Mwaka 2000 tuliowana na kuj'aliwa mtoto. Kwa mapenzi yake MUNGU mke wangu alifariki mwaka 2011 akiwa mjamzito wa mapacha wawili na niliwapoteza wote. MUNGU ni mwema mke wangu aliniachia Bint yetu wa kwanza aliyezaliwa mwaka 2006 na wakati mama yake anafariki alikuwa na miaka mitano sawia. Juzi huyu bint yangu ametimiza miaka 10, niliamua (sijui kwa nini) kumuuliza kama anakumbuka chochote kuhusu mama yake akasema hakumbuki vema. Niliamua kuchukua ile Radio na ile cassete na kumuomba tuisikilize. Tulilia sana! Ubarikiwe mtoa mada.
Pole sana Mkuu.
 
Umenikumbusha mbali sana wakati huo betrii zikiisha hazitupwi. [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Zinaanikwa juani, na hasa wakati wa mechi kubwa ya soka kama vile kati ya Simba na Yanga...Duh aise radio zenyewe zilikuwa chache na kama ni shuleni (kwa wa mikoani na hata kwa hapa Dar) mnakusanyika karibu watu 50 au zaidi kusikiliza matangazo hayo...
 
Mimi baba alikuwa anasema ukitumia rewinder ya radio ku rewind wimbo unaoupenda, betri zinaisha zaidi...full kutumia pen
 
Back
Top Bottom