Hivi sheria/taratibu zingine huwa zinawekwa za nini??

Sangarara

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
13,100
5,649
Najua zipo nyingi, leo nitatoa mbili
KWANZA, Kuna hii ya Cheque inayozidi 10M haiwi processed through BOT clearing house, lakini unakuta mtu anaandika cheque mbili anamlipa mtu yuleyule mmoja, tarehe ile ile, za Milioni Saba Saba, zinaenda BOT na zinapita? Najua BOT wameiga regulation hii kutoka somewhere uko nje? Kwa nini hawakuuliza mantiki yake kabla ya kuja kupest huku kwetu?

PILI, kuna hii ya kwamba Mgeni haruhusiwi kufungua kampuni hadi awe na shareholder mmoja wa kibongo, ama sivyo kampuni hiyo haitaweza kufungua account Bank. Kampuni inafunguliwa na wamiliki wawili, Patel with Canadian Nationality na Advocate Sangarara with Tanzanian Nationality, Signatory wa Accounts zote za Kampuni ni Mr Patel Peke Yake, Kampuni hii inafungua Bank Account, BOT wanareview na kuendorse kwamba taratibu zote zimefuatwa? hivi hawa Ma Banker wetu wanaelewa mantiki ya kuweka taratibu kama hizi?

Tujadili.
 
Back
Top Bottom