Sasa hivi nchini kwetu kumekuwa na rushwa za waziwazi sana bila hata chembe ya aibu. Ninakumbuka nilikwenda TRA ile ofisi wanayotoa leseni. kwa bahati mbaya wakati nakabidhi viambatanisho ili niweze kupewa leseni nikasahau cheti cha macho. Yule mama (muhusika) akanirudishia kwa ghadhabu akasema kama hujui waulize wenzako, mmoja akanivuta pembeni akaniambie weka na shs 2000 (juu ya ile ada halisi ya kulipia leseni). Kwakuwa nilikuwa na cheti cha macho nikaambatanisha sikumpa yule mama ile pesa. Ila akaniadhibu indirect kwa kuniweka muda mrefu. Hivi tutafika tunapokusudia?