Hivi nyoka na binadamu, nani hampendi mwenzie?

Hivi nyoka na binadamu, nani hampendi mwenzie?

BABA SANIAH

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2013
Posts
4,770
Reaction score
6,242
Habari za muda huu wadau,

Nimetoka nje hapa ofisini kwetu, nikiwa nimesimama chini ya mti wa muarobaini kwa bahati mbaya nyoka wa kijani akaniangukia kichwani sikumuona, akaruka chini na kuondoka haraka sana.

Sasa nimekaa na kujiuliza, kati ya nyoka na sisi nani mkorofi? Hivi mimi ningeanza kumuona si ningemuua? Mbona yeye kaniona kakimbia?

Tuchangie kwa umakini wadau..
 
Mimi ninavyoona kama utakuwa umetulia usipokuwa na hofu basi nyoka hawezi kuleta madhara. lakini pale unapokuwa na hofu ukapandisha hormones basi na nyoka anajihami kwa mashambulizi.
 
Kuna nyoka wa aina nyingi na tabia zao ni tofauti sana kuna nyoka wengine hawana muda na binadamu wala hawana sumu.

Ungejua kama kati ya binadamu na nyoka na mkorofi ungeangukiwa na Cobra au Chatu sasa hivi ingekuwa msiba hapo nyumbani.

Kuna nyoka wengine wana sumu kali sana kila kitachotoktea mbele yake anagonga tu.
 
Mimi ninavyoona kama utakuwa umetulia usipokuwa na hofu basi nyoka hawezi kuleta madhara. lakini pale unapokuwa na hofu ukapandisha hormones basi na nyoka anajihami kwa mashambulizi.
Mkuu kuna nyoka yeye akimuona binadamu ni vita tu msome huyu.


The most venomous snake known in the world, a few milligrams is strong enough to kill 1000 people! Less than 1/4 of bites will contain venom, and they are relatively docile. Fisherman are usually the victims of these bites, as they encounter the species when they pull nets from the ocean. Found throughout waters off South East Asia and Northern Australia.
 
Binadamu ndiyo mkorofi na siku zote ogopa binadamu kuliko mdudu au mnyama.
 
Huyu nyoka ni mkorofi mno usimbe ukutane nae.

The feared Black Mamba is found throughout many parts of the African continent. They are known to be highly aggressive, and strike with deadly precision. They are also the fastest land snake in the world, capable of reaching speeds of up to 20km/h. These fearsome snakes can strike up to 12 times in a row. A single bite is capable of killing anywhere from 10-25 adults. The venom is a fast acting neurotoxin. Its bite delivers about 100–120 mg of venom, on average; however, it can deliver up to 400 mg. I

f the venom reaches a vein, 0.25 mg/kg is sufficient to kill a human in 50% of cases. The initial symptom of the bite is local pain in the bite area, although not as severe as snakes with hemotoxins. The victim then experiences a tingling sensation in the mouth and extremities, double vision, tunnel vision, severe confusion, fever, excessive salivation (including foaming of the mouth and nose) and pronounced ataxia (lack of muscle control).

if the victim does not receive medical attention, symptoms rapidly progress to severe abdominal pain, nausea and vomiting, pallor, shock, nephrotoxicity, cardio toxicity and paralysis. Eventually, the victim experiences convulsions, respiratory arrest, coma and then death. Without antivenin, the mortality rate is nearly 100%, among the highest of all venomous snakes. Depending on the nature of the bite, death can result at any time between 15 minutes and 3 hours.
 
Usitegemee koboko akufanyie hivyo......ukikutana nae kimbia tu.
 
Ukikutana na nyoka gafla ukiwahi kumtemea mate nyoka ataenda kufa!
 
Mungu alishaweka uadui baina ya kizazi cha Nyoka na Mwanadam!! atatugonga kisigino lakini tutampnda kichwaa
 
Hawapendani, ila ukiwa mtulivu nyoka hakudhuru.
 
Leo nimekaa ofisini kuna mauwa mengi sana naona nyoka anaingia ndani ameshapanda ngazi me nikapiga kelele kumuita mwenzangu alf me nimekimbia chumba kingine mate anafika nyoka amesepa kwenye maua hatujamuona tena
Nyoka ndio adui ndio maana amekimbia sauti tu
 
Black MAMBA ndio nyoka mkorofi,huyo ukikutana naye tafuta pa kujificha.
Kwa nyoka wengine ukimuacha Chatu, ajitangulia kukuona wewe hauoni kama ww ni adui...uadui unautengeneza ww baada ya kumuona kama yupo karibu yako anaweza kukugonga kwa ajili ya kujihami tu.

Mwanadamu akimuona nyoka hushtuka,unaposhustuka mwili wako hutoa harufu fulani ambayo ikimfikia nyoka anajua ww ni adui...ndio sababu jwa watoto wadogo wasiojua nyoka ni hatari unaweza mkuta anacheza na nyoka ukashangaa.
 
Nyoka wenye sumu sio wakorofi kama tunavyofikiri kwa kuwa kisayansi kutengeneza sumu nyingine mara baada ya kutumia ya kwanza ni gharama kubwa sana kwake. Sumu hasa ni kwa ajili ya kuwindia tu ingawa hatoacha kuitumia mara atakapokutana na adui ni lazima ajilinde.

Na ndio maana mara nyingi huwa yeye wa kwanza kumkimbia binadamu hasa anapokuwa kwenye umbali sahihi wa kujilinda kabla ya kulazimishwa kutumia sumu yake.
 
Ushauri mzuri ni kuwa makini kwa kutohamaki hovyo mara unapokutana na nyoka tulia na acha papara za kutafuta fimbo au kitu chochote ili umdhuru ingawa binadamu huwa tunashindwa kustahimili hilo.
 
Back
Top Bottom