Hivi nini source ya senene??

Hivi nini source ya senene??

kwa wakwe zangu bukoba wako wengi sanaaa ila me huwa sili kabisa wale wadudu.makabila mengine haya basi tu tumeolewa but wanakula vitu vya ajabu mara sijui kahawa za kutafuna jaman!!!

We msichana vitu vya ajabu ni vipi. Hujaolewa huko, maana ukiolewa huko lazima uonje na ukionja utawaiba kutoka kabatini nakwambia msichana!
 
Hawa wadudu wanapatikana katika mwambao wa ziwa victoria, huko ndiko humea, wanapokuwa na mabawa husambaa kimakundimakundi pembezoni mwa ziwa, radi ikipiga huruka juu sana kwahofu na husafiri umbali mrefu ili kutafuta sehemu iliyo salama, basi ikitokea wakaona mwezi unaangaza, huruka kuufuata na hatimaye baada ya kufika juu sana, huona mwangaza mwingine kwa chini ambao ni human made, hubadili uelekeo badala ya kwenda katika mwezi huruka hadi katika taa zinazoangaza chini nasi ndo tunapata wasaa wa kuwaokota na kuwatafuna. Kula nyuma wanakuwa wameacha Mayai na tunutu ambavyo navyo baadae huwa ni senene kamili. Kama hakuna kitu chakuwashtua huwa wanatulia tu ndo maana huwa tunawaona misimu ya masika ikikaribia.
 
Turejee sayansi/bailojia. Wadudu hupitia hatua za yai, lava, pupa na mdudu kamili. Ule wakati ambao senene hawaonekani huwa katika hatua hizo za awali. Ni wazi wale wakubwa huwa walishataga mayai na halafu kuliwa au kufa. mzunguko unaendelea.
 
Wanatoka ama kwa Masilingi au Ana Kajumulo Tibaijuka! Just a joke. Sijui!
 
Asili ya senene ni mavi. Huwa wanaishi chooni kwa muda then wakisha komaa wanakuja nje kutafuta majani ndipo baadhi ya watu wenye uchu wa kula wadudu wala mavi wanawavuna. Hivyo kama una mapenzi ya kula senene, basi huenda ulishakula mavi yangu pia. Pole.
 
Ukijua nzige wanatoka wapi, basi hata senene itakuwa hivyo hivyo. hawana tofauti sana.
 
Back
Top Bottom