Hivi ni kweli uchawi upo Duniani ?

Olivia olivia

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2024
Posts
1,653
Reaction score
3,903
Hii imekaaje jamani...

Leo usiku majira ya sa 8 kasoro niliamka na kutoka nje

Kuna kitu nilisahau nilienda kuchukua hapo nje ( ndani ya fence)

Nilivyofika kwenye varanda la nje sijui nini kilitokea

Mimi nilianguka sehemu ambayo hata mtoto mchanga anayejifunza kutembea hawez kuanguka

Nilianguka ( sikujitambua nikiwa nimelala hapo chini sikua na fahamu yeyote) baada ya dakika kama 30 nilianza kupata fahamu na kujiona nimelala chini varanda la nje

Nilishangaa nimelalaje mahali pale nikakumbuka nilitoka kufata kitu ...sasa kila nilipotaka kuamka nilishindwa as if nakandamizwa chini

Sikua na nguvu kabisa nililegea na kuchoka

Badae sana nikaweza kuamka na kurudi ndani

Kichwa kilikua kizito

Kinauma

Nasikia kizungu zungu na kutapika

Hadi sasa bado najiuliza ilikuaje kuaje bado sijaelewa

Na bado mwili haujakaa sawa

Hii itakua ni nini jamani ?
 
Uchawi Uliopo ni Sayansi ambayo hutengeneza vitu vyakuonekana kama Simu, ndege, magari, Mitambo n.k

Nje na hapo huo ni ujinga wa kuaminishwa ujinga.

Eti mtu anapaa na Ungo , au chuma ulete, sijui kalogwa kawa kichaa, yaani utaira tuu.
 
Mkuu pole sana. na tatizo la kiafya au kuna kitu hakipo sawa kwenye mwili wako. Huu siyo uchawi.
 
Iombee hilo eneo
 
Kwa hili swali tu wewe unamatatizo mawili!, kwanza unahitaji elimu juu ya kuzingatia afya maana kwa hilo lililokupata ulitakuwa uwe umeshaenda hospitali kama haujaenda bado!, pili inatakiwa elimu yakufuta hayo mawazo ya kuwaza uchawi hayo mambo yakiimani ni ubatili mtupu!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…