Hua nawasikia sana watu wakijaribu kulinganisha utajiri wa Mo na Sheikh Bakhressa, watu wanasema Bakhressa kamwacha mbali sama Mo. Nakaa nacheka tu.
Huyu jamaa nilikutana nae mwaka jana ofisini kwake pale Golden Jubilee Tower, aisee huyu Mo ni kichwa, tena kichwa cha motooo. Kila anachozongumza kinarelate 1 kwa 1 na biashara. Tofauti na sisi ambao muda wote tuko kwenye simu, nilivyokua nae alitumia calculator mara nyingi zaidi ya simu.
Huyu Mo ana MBA ya Georgetown University, na alikuwa president of students' Organization (tena mwafrika wa kwanza kushika hiyo nafasi pale Georgetown). Hii inaonesha jinsi gani jamaa alivyo smart. Nakumbuka kwenye interview yake 1 na CNBC alisema yeye ndio largest producer na trader wa sisal duniani. Yani sisal anayoproduce kwa siku anaweza kuizungusha na ikafunika dunia mara 3 hivi.
Dewji kwa E. Africa yeye ndio trader mkubwa zaidi wa commodities in and out. Huyu jamaa ananunua korosho huko Mtwara kwa $1 kwa kilo then bei ya korosho ktk global market ni $12, ona hapa anavyopiga pesa ya wazi - na huko wamakonde msimu wa korosho niliwakuta wameneeka haswa, watu wamegonga mamilioni kwenye mashamba ya Korosho, TPDC walikua wanawanyenyekea vibarua wa kuchimba mifereji ya bomba la gesi, maana watu walikua na pesa ya korosho huwezi kuwa convince kufanya vibarua kwa ujira wa buku 3 kwa metre 1.
Ana export peagon peas, mbaazi, choroko, ufuta, mtama, nk kwa tones kwa tones... Huyu jamaa alinunua viwanda vingi sana vya serikali ambavyo vilishaanza kufa, akauziwa kwa bei ya dagaa, karenovate saivi anazalisha karibia kila kitu, sabuni, viberiti, chumvi, baking powders, karibu kila kitu.
Kiufupi huyu Mo yuko very smart, kazaliwa anamuona baba'ke mzee Gulam Dewji anafanya biashara, kakulia kwenye biashara, kaenda best schools hapa duniani kusomea biashara. Yani hafanyi vitu kwa mazoea, anafanya vitu kwa modern trend, na yeye ndio anaintroduce hizo modern trends hapa Bongo, so rivals wake kina Zacharia, Bakhressa wote wanakua wanacheza ngoma yake.
Kuna watu wanasema jamaa ni kwamba alikuta tyr home kuna utajiri so yeye akaendeleza... ukweli ni huu - Dewji alikuwa wall street ndio Mzee wake akamuomba arudi Bongo kurun business, mzee alishaona kazidiwa vby na kina Bakhressa, wakati huo MeTL ina utajiri wa $30 mil. Sasa huyu kichaa akapewa rungu. Ndani ya miaka 11 akabadilisha $30 mil kuwa $1.1 bil. Kitu ambacho hakuna Mwafrika anaweza kukifanya, labda tu Dewji aanze upya. Nakumbuka Dangote alikopeshwa pesa na mjomba ake (ambae alikua the richest man in W. Africa back then) pesa hiyo kwa kipindi hiko ingeweza kununua luxury Mercedes Benz 550... lkn ilimchukua dangote miaka 30 kukamata $1 bilioni - tofauti na Mo ambae ilimchukua decade 1 tu.
This boy is a Beast!!