tang'ana
JF-Expert Member
- Apr 3, 2015
- 12,055
- 16,509
Tangu kuanza kwa drama za watu waliokatwa na wasiotakiwa ndani ya chama kuhama na wengine kutishia kuhama chama..naona ccm wako kimya tu,ukimya wao utakua unaashiria nini?
Tokea siku ya Jumatatu pale ambapo makao makuu ya CCM mtaa wa Lumumba walipewa taarifa za mhshimiwa Lowasa kuhama chama na kutimkia UKAWA.
Kwa kuwa vijana wa masuala ya propaganda chini ya katibu mwenezi Nape Mnauye walidhani ulikuwa utani au masihara wakapuuzia onyo hilo sasa imekuwa ngumu kutoa taarifa ya kupokea uamuzi huo.
Katika ulimweigu wa sasa wanasiasa nao wakiwa kama binadamu wengine nao wana utashi na moja ya matunda ya utashi huo ni kuweza kufanyamaamuzi na kuyatakeleza.
Pia katika nchi mbalimbali duniani vyma vya siasa vinakuwa na washauri wao ambao moja ya kazi zao ni kujaribu kuoanisha taarifa zinazopishana kuhusu sera, itikadi na suala Zima la mbinu na mikakati.
Lakini Chama cha Mapinduzi wamekuwa kimya hata baada ya kuona kwenye mitandao kwamba Tumaini Makene, mkuu G Sam na wengine walikuwa wakifanya kazi usiku na mchana, na Nape Nnauye akawa hajajiandaa angalu kujibu uamuzi huo wa mzee Lowasa kuhama CCM.
CCM si chama lelemama na kipo kinatawala nchi hii tangia ilipokuwa TAA, TANU hadi CCM ilozaliwa tarehe 5 mwezi wa 7 mwaka 1977.
CCM mtaa wa Lumumba vipi mmekaa kimya au Nape Nnauye bado ametahayari?
CCM mtaa wa Lumumba isiwaache vijana wasofahamu siasa kuja jamii forums kujaza taarifa za kizushi kuhusu UKAWA na Dr Slaa, au mjinga mmoja anakuja na kichwa cha habari kinachosema Dr Slaa is dead!.
"Spin Doctors" wa CCM wapo wapi?