Hivi mapenzi huwa yanachuja?

Hivi mapenzi huwa yanachuja?

juvenile davis

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2015
Posts
4,752
Reaction score
4,475
Habari za siku nyingi wana MMU?

Nisipoteze muda nije kwenye mada kuna mwanamke nimetokea kumpenda sana, namfahamu kama miaka minne iliyopita lakini sikuwahi kumtongoza na wala hatukuwa na mazoea wala salamu.

Baada ya miaka miwili nikaamua nianze kumpa salamu akipita maeneo yangu au tukionana njiani.nilitaka kwanza anizoee ili siku nikitupa nyavu nisiwe ni mtu mgenikwake.akawa anaitikia salamu vizuri bila wasiwasi .sasa baadae nikashangaa ghafla hataki salamu yangu na nikimsimamisha hataki hata kusimama.

Na mimi sikukata tamaa kumsalimia na kumsimamisha.mwaka huu nikaongeza bidii ya kumuomba anisikilize shida yangu.ndipo kuna siku akasimama akanipa namba yake ya simu.tukaanza mawasiliano katika simu lakini akanichomolea. Baadaye aliponizoea akaniambia jambo ambalo limeniduwaza sana,akaniambia alinipenda sana kuanzia siku ya kwanza aliponiona na alikuwa anatamani nimwite nimtongoze ila mimi sikuwa na time nae wala mazoea naye.

Akaniambia aliponizoea kuniona mapenzi kwangu yakafa akawa hanipendi wala havutiwi tena na mimi.ananiambia kwa sasa ananiona wa kawaida tu so hana feelings na mimi kabisa.sasa nijiuliza je mapenzi huwa nayo yanaexpire kiasi kwamba inawezekana ukawa unamuona mtu ni mzuri ila after a few days ukaanza kumuona ni wa kawaida tuu?
 
Habari za siku nyingi wana MMU?

Nisipoteze muda nije kwenye mada kuna mwanamke nimetokea kumpenda sana, namfahamu kama miaka minne iliyopita lakini sikuwahi kumtongoza na wala hatukuwa na mazoea wala salamu.

Baada ya miaka miwili nikaamua nianze kumpa salamu akipita maeneo yangu au tukionana njiani.nilitaka kwanza anizoee ili siku nikitupa nyavu nisiwe ni mtu mgenikwake.akawa anaitikia salamu vizuri bila wasiwasi .sasa baadae nikashangaa ghafla hataki salamu yangu na nikimsimamisha hataki hata kusimama.

Na mimi sikukata tamaa kumsalimia na kumsimamisha.mwaka huu nikaongeza bidii ya kumuomba anisikilize shida yangu.ndipo kuna siku akasimama akanipa namba yake ya simu.tukaanza mawasiliano katika simu lakini akanichomolea. Baadaye aliponizoea akaniambia jambo ambalo limeniduwaza sana,akaniambia alinipenda sana kuanzia siku ya kwanza aliponiona na alikuwa anatamani nimwite nimtongoze ila mimi sikuwa na time nae wala mazoea naye.

Akaniambia aliponizoea kuniona mapenzi kwangu yakafa akawa hanipendi wala havutiwi tena na mimi.ananiambia kwa sasa ananiona wa kawaida tu so hana feelings na mimi kabisa.sasa nijiuliza je mapenzi huwa nayo yanaexpire kiasi kwamba inawezekana ukawa unamuona mtu ni mzuri ila after a few days ukaanza kumuona ni wa kawaida tuu?
ndio ivo,hata mke utataman akuondokee ubaki pekeako
 
Mwanaume mwenye pesa hachujiiii hata akiwa mzee bado ni msweet sweet anang'aa yaan raha tupu
 
Sifa ya Binadamu, huzaliwa, huishi, hufa.

Kabla ya kufa kuna kitu kinaitwa "utility" Wahasibu na Wana uchumi wananielewa kuwa "kadri ya kitu chochote kinavyozidi kutumika ndivyo hupunguza ubora wake wa asili"

Sasa unategemea Babu wa miaka 60 atawika vizuri kwenye mapenzi moto moto kivitendo hususani kujamiiana kuliko kijana wa miaka 16 au 18?

Ndivyo jinsi ilivyo hivyo hiyo inshu ya kuchuja kwa mapenzi na si mapenzi tu bali hata inshu zingine kimaisha.
 
Nenda kwa mganga mfanyie factory reset atarudi kwa spidi ya ajabu..😂
 
Sifa ya Binadamu, huzaliwa, huishi, hufa.

Kabla ya kufa kuna kitu kinaitwa "utility" Wahasibu na Wana uchumi wananielewa kuwa "kadri ya kitu chochote kinavyozidi kutumika ndivyo hupunguza ubora wake wa asili"

Sasa unategemea Babu wa miaka 60 atawika vizuri kwenye mapenzi moto moto kivitendo hususani kujamiiana kuliko kijana wa miaka 16 au 18?

Ndivyo jinsi ilivyo hivyo hiyo inshu ya kuchuja kwa mapenzi na si mapenzi tu bali hata inshu zingine kimaisha.
hapo umenena njoo chukua pesa ya soda
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom