Hivi Lissu ana dini kweli?

jijiletublog

Member
Joined
Jul 23, 2020
Posts
31
Reaction score
74
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu amewashangaza Watanzania kuhoji uwezo wa Mungu katika uponyaji wa janga la corona nchini.

Kauli hiyo ya Lissu pia imeenda mbali zaidi alipowashangaa Waislamu na Wakristo kwenda kanisani na misikitini kuombea corona huku akiwaita ni wajinga.

Lissu ametoa kauli hizo tata zinazozidi kutoa tafakari ya afya yake ya akili akihojiwa na Radio Maisha ambapo amesema Mungu kwamba hawezi kuponya magonjwa na hana muda wa kuhangaika na wajinga.

“Kama alivyosema rais mwenyewe hii kitu dawa yake ni kwenda msikitini na makanisani kuomba Mungu, katika karne ya 21 rais anayesema ana PHD katika Kemia kuamini kwenye mambo kwamba unaweza kutibu ugonjwa kwa maombi ya Mungu,” amesema Lissu.

Mtangazaji wa kipindi hicho alimuuliza Lissu; “Kwa hiyo hujapendezwa kabisa kwa namna rais anavyoshughulika na hii ishu ya covid19 pale nchini?”

Lissu akajibu: “Mungu ana mambo mengi sana hana muda wa kuhangaika na wajinga.”

Kauli hii ya Lissu inaacha maswali kwamba je; ana dini? Kama kweli angekuwa na dini basi angekuwa na hofu ya Mungu.

Lissu anasahau kama ni Mungu amemponya na kumfikisha hapo alipo leo badala yake alianza kutukana watu kama vile haitoshi amehamia kwa muumba na watumishi wa wake.

Your browser is not able to display this video.


 
Katika uchaguzi huu ni lazima watu waiite maji "ma" kwa maana spana za Tundu Lissu si za mchezo.
 
Kura za ubunge na uraisi zitasafirishwa kwenda kuhesabiwa jimboni, hazitahesabiwa kwenye vituo vya kupigia kura

Kura za udiwani zitasafirishwa kwenda kuhesabiwa makao makuu ya kata (katani)

Wapinzani hampati kitu.

Kuweni makini
 
Kanisani huwa anaenda kufanya nini kama anaamini Mungu hawezi kusikiliza maombi yetu?
Kwani yeye isingekuwa Mungu kumponya leo hii angekuwa hai?

Sisi Wakatoliki ( Lissu akiwemo) katika kila misa baada ya mahubiri na kurudia kukiri imani yetu hufuata maombi ambapo waamini humuomba Mungu mambo mbalimbali ikiwemo kutuponya na magonjwa na majanga mbalimbali nk. Sasa yeye inaonyesha kuna mambo hakubaliani nayo. Mimi nadhani pengine aliishaacha kwenda kanisani ila sababu ya uchaguzi imebidi aende kanisani kama geresha ili wakristo wasimstukie; baada ya uchaguzi ataacha kwenda. Ni kama vile huko nyuma alipokuwa anamtukana Nyerere lakini kwa ajili ya kugombea urais akaanza kumsifia Nyerere ili watanzania wampe kura.

Watanzania wakiingia mkenge wampe kura watajuta.
 

Yes yuko sahihi kabisa
Kilichotumika ni uponywaji wa kisaikologia

Mungu huyu huyu awauwe Mpaka taifa ambalo alilitamka kwenye kitabu chake kuwa ni taifa teule Israel kwa Korona then Tanzania iachwe?

Mpaka Ibada ya hija maca ilisitishwa because ya korona
 

Siku yake ya kufa ilikuwa haijafika,
Kama siku yako imefika hata ukijikwaa tu unakufa
 
Raisi ajaye!.
Corona haikuiathiri afrika kwa sababu za kijografia siyo Tanzania tu. Nchi nyingi za afrika hazikuathirika,
tumuache Mungu apumzike
 
Usaliti wa Nchi ni laana kwa Taifa, ndicho kinachimkabila huyu jamaa
 
Jomba wewe watanzania huwajui wewe... anaweza kukuchekea saa hizi then baadae akakuchinjilia mbali... hapo ndipo napopapendea kwa watanzania...
 
Lissu ni mtu wa kuhurumia sana ameanza kuugua maradhi mabaya sana
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…