Hivi kweli Serikali na Bunge hazikuona upungufu wa kuondoa Tozo ya Mafuta? Hakika Pengo la Tundu Lissu halijazibwa

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
84,004
142,038
Jaribu kufikiria, Waziri wa fedha anapeleka mswada wa Tozo ya mafuta bungeni na bunge zima linapitisha.

Baadae Waziri wa Nishati anatangaza kuziondoa Tozo hizo ili kuwapa wananchi unafuu wa bei lakini halihusishi bunge.

Wabunge wote wanapata taarifa kwa sababu wote wana magari ya mkopo na wananunua mafuta. Lakini hakuna mbunge hata mmoja aliyeshtuka kwamba utaratibu umekosewa.

Hata wale wabunge 25 wa upinzani yaani Chadema, ACT Wazalendo na CUF nao wakapiga kimya.

Hadi Rais ndio kaona kuna hayo mapungufu na kuirejesha.

Nchi ngumu hii na hili bunge la akina Babu Tale.

Enzi za Tundu Lisu hili lisingewezekana asilani, angempinga Waziri January pale pale anapotangaza kufuta Tozo.

Maendeleo hayana vyama!
 
Tulidanganywa Mama katuonea huruma na ametoa punguzo la 100/ leo ana wakana na kuzirudisha. Duhhh, Ccm ni tatizo kuu.
 
Tulidanganywa Mama katuonea huruma na ametoa punguzo la 100/ leo ana wakana na kuzirudisha. Duhhh, Ccm ni tatizo kuu.
Lakini taarifa ya ikulu ilisema yeye ndio kaona tozo ziondolewe na baada ya kufanya vikao nao
Screenshot_20220330-143743_1.jpg
 
Umeanza vema lakini hapo mwishoni umeenda mrama. Suala lenye masilahi binafsi si CHADEMA wala Lissu walikuwa tayari kulipigania. Tukianza suala la kuongezewa Posho na mishahara kwa wabunge siku zote walikuwa wanakubaliana na CCM na hili la kupunguzwa tozo za mafuta ni suala lenye masilahi binafsi.
 
Umeanza vema lakini hapo mwishoni umeenda mrama. Suala lenye masilahi binafsi si CHADEMA wala Lissu walikuwa tayari kulipigania. Tukianza suala la kuongezewa Posho na mishahara kwa wabunge siku zote walikuwa wanakubaliana na CCM na hili la kupunguzwa tozo za mafuta ni suala lenye masilahi binafsi.
Lisu alikuwa anahoji kila kinachovuruga kanuni na sheria!
 
Back
Top Bottom