EeeenHeeee!
Nacheka huku nikilia machozi kwa nchi yangu Tanzania.
Tunatoka kwenye kikaango tunaangukia kwenye makaa ya moto mkali.
Mungu Ibariki Tanzania.
Ahsante sana kwa uteuzi Mheshimiwa Rais, vijana mkapige kazi, mmeaminiwa na rais msimuangushe.
Pastor masanja mkandamizaji apewe UDED wa dar,,kajitahidi sana kutetea chama.Halafu kwa uelewa wangu, nilikuwa najua ma DED angalau ni wale waajiriwa wa serikali wenye uzoefu, mfano wakuu wa idara katika halmashauri. Kwa sababu mkurugenzi anaenda kusimamia uchumi wa halmashauri. Ngoja tusubiri tuone.
hapa atakuwa analengwa Nikki wa pili na ChipongaKwa namna ulivyoteua ma-DC sioni kama uko serious. Nafasi ya u-DC inashuka hadhi kila kukicha, kwa sababu inaonyesha kila mtu anaweza kitu ambacho si kweli.
DC ni mtu ambaye anatakiwa atoe dira ya maendeleo ya wilaya yake lakini kwa baadhi ya hawa uliowateua ni sawa na wapiga debe wa daladala! DC ni mtu ambaye anatakiwa kumshauri RC kudumisha amani ndani ya wilaya yake lakini hawa ni ma-DJ watakaokesha katika kumbi za starehe. DC ni mlezi wa vijana katika wilaya yake lakini hawa ni comedians.
Kwa kifupi hakuna uongozi katika wilaya, hakuna mlezi, hakuna busara uliyopeleka wilayani bali kuna washereheshaji! Tafadhali Rais Samia hebu kuwa serious kidogo wananchi tupate imani! Nalilia nchi yangu inavyoangamia! Hawa vijana wako angalau wangepewa orientation ya uongozi!
Mungu ibariki Tanzania!
Ni sawa lakini kwa mujibu wa sheria zetu DC anaweza ku-overule maamuzi ya DED na Baraza la madiwani. DC ana nguvu ya ushawishi na maamuzi katika masuala mbalimbali ya kijamii. Hivyo kuwa na DC kilaza katika wilaya ni mzigo!Dira ya maendeleo iko na DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR siyo DC. DC majukumu yake ni kuhamasisha utendaji kazi, kuratibu shughuli za kiserikali kama mapokezi ya viongizi, kuzuia migogoro ya kivikundi. Ni majukumu ambayo yanaweza kuwa embedded kwa DED.
DC ni nafasi iliyorithiwa kutoka mfumo wa kikoloni wa indirect rule. Katiba mya ya wananchi rasimu ya Warioba ilipendekeza nafasi kama hii kufutwa. Viongozi wa watu wanapaswa kutokana na watu wenyewe kama walivyo kwenye nchi jirani ya Kenya.
Kwangu mimi na watu makini nafasi hii imekuwa ikitumika kama shukrani kwa baadhi ya watu ambao wamemsaidia Mteuzi au Chama Tawala.
Ningeona vizuri tupaze sauti KUFUTA nafasi za ma DC kuliko kuanza kuangalia nani kapewa u- DC.
Nimekusoma hapa mkuu...; halafu na hapa chini!Mimi nimelia sana nikamkumbuka magufuli, huku tunakopelekwa mmh
Nikawaza..., kumbe wewe ni DC mteule?Mwachen mama afanye kazi , Mama 50 tena
Umeongelea nguvu ya "ushawishi", Ina maana hana nguvu "kisheria". Basi tena hakuna ulichonipingaNi sawa lakini kwa mujibu wa sheria zetu DC anaweza ku-overule maamuzi ya DED na Baraza la madiwani. DC ana nguvu ya ushawishi na maamuzi katika masuala mbalimbali ya kijamii. Hivyo kuwa na DC kilaza katika wilaya ni mzigo!
Kifungu gani hicho cha Sheria? Kiweke hapa tukioneSoma vizuri nimeandika kwa mujibu wa sheria zetu DC anaweza ku-overule maamuzi ya DED na Baraza la madiwani.
Uadilifu gani?Kwani kukosa uadilifu maana yake ni kucheza picha za ngono?
Halafu mimi nakapenda sana basi tu ubavu sina. Hivi kamehamishiwa wapi vile?
Halafu kwa uelewa wangu, nilikuwa najua ma DED angalau ni wale waajiriwa wa serikali wenye uzoefu, mfano wakuu wa idara katika halmashauri. Kwa sababu mkurugenzi anaenda kusimamia uchumi wa halmashauri. Ngoja tusubiri tuone.
So unajua baba angu ndo baba akoKamuulize baba yako labda utaelewa!
Nimecheka kama mazurina bado mtalia sana. Mlikua mnamwaga sifa mkidhan mtabebwa pyeeep
to be honest imebidi nicheke tu maanaMwachen mama afanye kazi , Mama 50 tena
Huyu mtu wala hujamwelewa aiseee,labda umemsoma Leo Leo.Nimekusoma hapa mkuu...; halafu na hapa chini!
Nikawaza..., kumbe wewe ni DC mteule?
Lakini huwa sipendi utani au unafiki kwenye mambo ya msingi kama haya.
Kwa hiyo nikaona nikupe stahiki yako: watu kama nyinyi ndio maadui wakubwa wa Tanzania kuliko hao wanaotutawala.
Siku tukifanikiwa kupata njia za kuwashughulikia nyinyi taifa letu litapona.
Baada ya hayo, nichukulie vyovyote uonavyo inafaa kwako.
Mi nimesoma haya aliyoandika..., na ndio msingi wa niliyoyaandika kumhusu yeye.Huyu mtu wala hujamwelewa aiseee,labda umemsoma Leo Leo.
Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app